Yanga yajiandaa kwenda Misri, safari ya Azam Tunisia yaiva

Daniel Mbega

JF-Expert Member
Mar 20, 2013
338
180
azam vs bidvest.jpg

MABINGWA wa soka Tanzania Bara, Yanga, wanaonekana katika nafasi kubwa ya kukwea pipa kwenda Misri kuvaana na National Al Ahly katika raundi ya pili ya Ligi ya Mabingwa Afrika ikiwa wataulinda ushindi wao wa mabao 2-1 dhidi ya APR ya Rwanda wakati timu hizo zitakaporudiana mwishoni mwa wiki hii.

Yanga wanahitaji sare tu katika mechi hiyo ya raundi ya kwanza ili kwenda Cairo kukabiliana na timu ya Al Ahly, ambayo mwishoni mwa wiki iliyopita ilibanwa mbavu na C.R.D. Libolo ya Angola mjini Luanda na sasa inataka ushindi wa nyumbani Ijumaa hii Machi 18.

Uchunguzi wa FikraPevu unaonyesha kwamba, timu za Afrika Kaskazini zina kawaida ya kulazimisha hata sare ugenini, lakini daima huwa na kawaida ya kugangamala nyumbani na kupata ushindi, hali ambayo ndiyo inayoonekana hata kwa Al Ahly ambayo inahitaji kurejesha heshima ya kutwaa ubingwa huo wa Afrika unaoshikiliwa na TP Mazembe ya Congo DR.
SOMA ZAIDI...
 
Umesahau miaka michache iliyopita hao wamisri walimshukuru said bahanuzi kukosa penati ya mwisho. Angefunga tu ile penati ilikua safari iishie pale tena kwenye uwanja wao wa nyumbani.

Yanga wakiamua kukamia mechi ni habari nyingine aisee!


Hahahahahha...Unaongelea NGE.....Wanaume simba wamewabikiri hao wamisri mara kadhaaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom