Yanga Staff vs Wasanii; Huyu Golikipa H. Kidiaba JR anaujua. Anatokea wapi?

Shark

JF-Expert Member
Jan 25, 2010
29,462
29,159
Kwema Wakuu?

Hii mada kila nikipost jana iliikua inakataa. Jana siku ya Wananchi nilikua naangalia matukio mbalimbali na washikaji wa kitaa ambao tunakuaga nao pamoja siku zote kwenye michezo (mipira, ndondi etc). Sasa mojawapo ya mechi za jana kwenye siku ya Wananchi ni mechi kati ya Staff wa Yanga v/s Wasanii mbalimbali.

Yanga waliwakilishwa na staff mbalimbali wakiwemo waliowahi kuichezea hapo kabla kama Mtwa Kiwhelo, Sekilojo Chambua, Fred Mbuna, Bakari Malima, Mohammed Hussein "Mmachinga", Abdi Kassim "Babi", pia staff wa kawaida kama Eng. Hersi, Ally Kamwe, Abeid Mvuma, CPA Haji Mfikirwa, Wakili Patrick Simon na wengineo.

Wasanii waliwakilishwa na KR Mula, Barafu, Foby, Golikipa H. Kidiaba JR, na wengineo siwakumbuki majina sababu siwafuatiliagi sana. Sasa hii mechi kwa kuiangalia tu utaona Yanga walipaswa washinde nyingi sababu angalau walikua na watu waliowahi kucheza mpira hata kama ni zamani wakati Wasanii wengi hatujui mpira walichezaga au wanachezaga wapi.

Lakini mechi iliisha kwa suluhu ya bila kufungana, kikwazo kikubwa akiwa Golikipa wa wasanii H. Kidiaba JR alieokoa michomo mingi. Sasa unaweza ukaidharau hii mechi sababu ilikua ya kujifurahisha na hata Wachezaji wa Yanga hawako katika ubora wao wa miaka hiyo, wengi tayari miili ishakua mizito (vitambi) ila Golikipa wa wasanii anaujua kiasi chake.

Nimeona nisiache kumpa maua yake huyu jamaa na kama hana timu basi akikazana atapata timu. Aliokoa michomo mingi ya karibu, ya mbali na hata ya krosi. Nimejaribu ku Google nione taarifa zake lakin zinakuja za Kidiaba wa DRC (TP Mazembe) aliekuja kua Waziri. Sijui anatokea wapi huyu jamaa. Msanii mwengine alieisumbua Yanga ni Foby, nae sijui ni Msanii wa nini ila hakua vibaya pia.
 
Kuna moment alijarbu kuruka kama kidiaba yule wa congo. Nkajua ni mtoto wa yule jamaa.
 
Uyu golikipa ata mm nimemuona, ni mzuri ligi kuu anacheza yule
Anacheza kabisa aisee, ni Golikipa mzuri. Sijui kama ni msanii kweli mpaka nimewaza ni Golikipa alieazimwa kutoka mahali
 
Kidiaba, yule foby na nacha wako vizuri.. hata lile li barafu kuna mali aliizuia na mguu wa kulia kwenye box kisha akashoot na mguu wa kushoto ni kistriker kabisa.

Funga kazi ni yule rais wao yanga, jamaa anajua boli kabisa.
 
Alikuwa anacheza na mastriker gani??hilo ndo liwe swali la msingi,watu wenyewe kina barafu sjui unasema kuna nyanda pale
 
Foby aliwahi kucheza ligi kuu kama sio daraja la kwanza aliacha baada ya kuvunjika mguu ..
 
Kwema Wakuu?

Hii mada kila nikipost jana iliikua inakataa. Jana siku ya Wananchi nilikua naangalia matukio mbalimbali na washikaji wa kitaa ambao tunakuaga nao pamoja siku zote kwenye michezo (mipira, ndondi etc). Sasa mojawapo ya mechi za jana kwenye siku ya Wananchi ni mechi kati ya Staff wa Yanga v/s Wasanii mbalimbali.

Yanga waliwakilishwa na staff mbalimbali wakiwemo waliowahi kuichezea hapo kabla kama Mtwa Kiwhelo, Sekilojo Chambua, Fred Mbuna, Bakari Malima, Mohammed Hussein "Mmachinga", Abdi Kassim "Babi", pia staff wa kawaida kama Eng. Hersi, Ally Kamwe, Abeid Mvuma, CPA Haji Mfikirwa, Wakili Patrick Simon na wengineo.

Wasanii waliwakilishwa na KR Mula, Barafu, Foby, Golikipa H. Kidiaba JR, na wengineo siwakumbuki majina sababu siwafuatiliagi sana. Sasa hii mechi kwa kuiangalia tu utaona Yanga walipaswa washinde nyingi sababu angalau walikua na watu waliowahi kucheza mpira hata kama ni zamani wakati Wasanii wengi hatujui mpira walichezaga au wanachezaga wapi.

Lakini mechi iliisha kwa suluhu ya bila kufungana, kikwazo kikubwa akiwa Golikipa wa wasanii H. Kidiaba JR alieokoa michomo mingi. Sasa unaweza ukaidharau hii mechi sababu ilikua ya kujifurahisha na hata Wachezaji wa Yanga hawako katika ubora wao wa miaka hiyo, wengi tayari miili ishakua mizito (vitambi) ila Golikipa wa wasanii anaujua kiasi chake.

Nimeona nisiache kumpa maua yake huyu jamaa na kama hana timu basi akikazana atapata timu. Aliokoa michomo mingi ya karibu, ya mbali na hata ya krosi. Nimejaribu ku Google nione taarifa zake lakin zinakuja za Kidiaba wa DRC (TP Mazembe) aliekuja kua Waziri. Sijui anatokea wapi huyu jamaa. Msanii mwengine alieisumbua Yanga ni Foby, nae sijui ni Msanii wa nini ila hakua vibaya pia.
Fobby alikua anacheza mpira na ndio ilikua ndoto yake,ila alipovunjika mguu ndio akaanza mziki
 
Foby aliwahi kucheza ligi kuu kama sio daraja la kwanza aliacha baada ya kuvunjika mguu ..
Fobby alikua anacheza mpira na ndio ilikua ndoto yake,ila alipovunjika mguu ndio akaanza mziki
Anhaa,
Alikua vizuri nae. Aliwasumbua staff wa Yanga kwa chenga zake na mguu wake wa kushoto. Lakini bado nauliza yule akipa anatokea wapi? Ni msanii nae?
 
Kidiaba, yule foby na nacha wako vizuri.. hata lile li barafu kuna mali aliizuia na mguu wa kulia kwenye box kisha akashoot na mguu wa kushoto ni kistriker kabisa.

Funga kazi ni yule rais wao yanga, jamaa anajua boli kabisa.
Barafu ule kweli, Dan.
Ila hiyo scenario niliiona
 
Alikuwa anacheza na mastriker gani??hilo ndo liwe swali la msingi,watu wenyewe kina barafu sjui unasema kuna nyanda pale
Huyo kipa na barafu walikua timu moja ya waaanii
 
Na barafu apunguze mwili, akili inavitu vitu ila mwili hautaki. Jana alitoa vituko sana yule mzee.

Yule kipa wao sijui walimtoa wapi, japo alikua anacheza na vibonde ila jinsi anaanzisha mpira na anavyotokea mashambulizi yakimfikia ilikua poa sana
 
Back
Top Bottom