Yanga ikichapwa Mbeya Mkwasa asilaumiwe

Kamgomoli

JF-Expert Member
May 3, 2018
1,865
3,802
Wengi walipoona GSM akifanya usajili wa dirisha dogo walizani neema imerudi Yanga na ni mwendo wa shangwe km lote. Nilipomsikiliza Nugaz akihojiwa wasafi Radio kwenye Sport Arena nilithibitisha bila shaka kuwa pale Yanga kuna shida kubwa.

Nilishangaa aliposema wachezaji wote wa Kizanzibar waliokuwa Cecafa hawajaambatana na timu kwa ajili ya michezo 2 migumu ya Mbeya. Pia wachezaji Yondani na Juma Abdul nao hawajaambatana na timu. Mlisho Ngasa nae hatokuwepo kutokana na family matters. Jumla Yanga itawakosa wachezaji 7 muhimu.Kinyume chake wachezaji wa Simba wote waliokua na timu ya taifa wametakiwa kuripoti kambini kujiunga na wenzao mara moja. Zanzibar walitolewa mapema sn je hayo mapumziko waliyopewa wachezaji wa Zanzibar yana sababu gani za msingi? Mbona wenzao wa Simba tena waliocheza mpaka mwisho wameripoti kambini?

Sote tumeona Ngasa anavyolalamikia malipo yake kwenye mitandao huku Nugaz akimjibu Ngasa kwa dhihaka kana kwamba yeye si sawa na Moro alielipwa stahiki zake haraka baada ya kukimbilia kwao. Mi naamini hawa wachezaji wa Kizanzibar watakua wamegoma pamoja kwani wakiwa Uganda nazani walipata muda wa kujadili hatima yao kwa kina na kuamua kutengeneza Solidality ili kushinikiza madai yao. Nugaz anasema waliwapa mapumziko ya siku 3,na sasa ni zaidi ya wiki mapumziko gani hayo. Km ni kweli ni mapumziko basi viongozi wa Yanga watakua hawajielewi na watakua wameshakata tamaa na ubingwa.

Viongoz wa Yanga wanashughulika zaidi na matatizo ya wachezaji wa kigeni kuliko local players. GSM hana lengo la kuondoa matatizo ya Yanga bali anatumia matatizo ya Yanga kupatia umaarufu biashara zake. Ndio maana ananunua wachezaji yeye,anawapeleka kuwatambulisha kwenye ofisi zake yeye mwenyew bila hata kiongozi wa juu wa Yanga kuwepo. Pia Nugaz anajitapa kwamba yeye ndio aliyeenda kumshawishi GSM na yule bosi Sport pesa kusajili wachezaji dirisha dogo. Najiuliza je hayo ndio majukumu ya afisa Muhamasishaji? M/ kiti,Makamu M/kiti na katibu wa Yanga wako wapi na nini faida ya uwepo wao pale Yanga?

Namuona Nugaz akianza kufanya ya Zahera. Mda si mrefu utaibuka mgongano wa maslahi.

Hii ndo Yanga ya Msolwa msomi wa level ya Phd.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mm n mnaz Wa yanga ila timu yangu inatia huruma sana najiuliza ile PhD ya msolwa inazidiwa akili na poyoyo nugaz kweli? Kazi ya kuunda kamati tu kila siku sielew znasaidia nn hizo kamat ikiwa kila siku n matatzo kamat zimeenda kuongeza matatzo

Boss Wa gsm na thobias lingala Ngala wao kama nan had wasajir wachezaji na je mishahara analipa nani?

Hii hali itashusha morali ya timu sana kwan wazawa hawatapambana kwa moyo na ikumbukwe 60% n wazawa na. 40% hao wagen je watacheza hao wageni



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Msolwa msomi wa level ya Phd. akii yake ya kimichezo ndo imeishia hapo mzee wetu yuko hoi taaban
 
Mtoa mada uko sahihi kabisa! Dr. Mshindo Msolla kuna baadhi ya vitu anafanya kama siyo professional vile! Kujenga ubaguzi na mgawanyiko kwa wachezaji ni jambo lisilokubalika.

Na huyo Antonio Nugaz akimaliza huo mkataba wake wa kimangungo wa miaka miwili aliopewa, aachane na timu yetu. Majukumu anayo yafanya kwa sasa yanatakiwa yafanywe na Hassan Bumbuli.

Kuchezea hela kwa mambo yasiyo na tija huku mambo ya msingi kama ya mishahara na posho za wachezaji yakishindwa kupatiwa ufumbuzi, ni udhaifu mkubwa sana kwa viongozi wa sasa wa Yanga.
 
Hakukuwa na haja ya kuhangaika na mambo ya kutengeneza uwanja na mapungufu waliyonayo pamoja na madeni ya wachezaji kwa wakati mmoja,wangemalizana na wachezaji wawe na nafasi nzuri,timu ikifanikiwa kimichezo ndo mafanikio mengine yanafuatia
Mtoa mada uko sahihi kabisa! Dr. Mshindo Msolla kuna baadhi ya vitu anafanya kama siyo professional vile! Kujenga ubaguzi na mgawanyiko kwa wachezaji ni jambo lisilokubalika.

Na huyo Antonio Nugaz akimaliza huo mkataba wake wa kimangungo wa miaka miwili aliopewa, aachane na timu yetu. Majukumu anayo yafanya kwa sasa yanatakiwa yafanywe na Hassan Bumbuli.

Kuchezea hela kwa mambo yasiyo na tija huku mambo ya msingi kama ya mishahara na posho za wachezaji yakishindwa kupatiwa ufumbuzi, ni udhaifu mkubwa sana kwa viongozi wa sasa wa Yanga.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wengi walipoona GSM akifanya usajili wa dirisha dogo walizani neema imerudi Yanga na ni mwendo wa shangwe km lote. Nilipomsikiliza Nugaz akihojiwa wasafi Radio kwenye Sport Arena nilithibitisha bila shaka kuwa pale Yanga kuna shida kubwa.

Nilishangaa aliposema wachezaji wote wa Kizanzibar waliokuwa Cecafa hawajaambatana na timu kwa ajili ya michezo 2 migumu ya Mbeya. Pia wachezaji Yondani na Juma Abdul nao hawajaambatana na timu. Mlisho Ngasa nae hatokuwepo kutokana na family matters. Jumla Yanga itawakosa wachezaji 7 muhimu.Kinyume chake wachezaji wa Simba wote waliokua na timu ya taifa wametakiwa kuripoti kambini kujiunga na wenzao mara moja. Zanzibar walitolewa mapema sn je hayo mapumziko waliyopewa wachezaji wa Zanzibar yana sababu gani za msingi? Mbona wenzao wa Simba tena waliocheza mpaka mwisho wameripoti kambini?

Sote tumeona Ngasa anavyolalamikia malipo yake kwenye mitandao huku Nugaz akimjibu Ngasa kwa dhihaka kana kwamba yeye si sawa na Moro alielipwa stahiki zake haraka baada ya kukimbilia kwao. Mi naamini hawa wachezaji wa Kizanzibar watakua wamegoma pamoja kwani wakiwa Uganda nazani walipata muda wa kujadili hatima yao kwa kina na kuamua kutengeneza Solidality ili kushinikiza madai yao. Nugaz anasema waliwapa mapumziko ya siku 3,na sasa ni zaidi ya wiki mapumziko gani hayo. Km ni kweli ni mapumziko basi viongozi wa Yanga watakua hawajielewi na watakua wameshakata tamaa na ubingwa.

Viongoz wa Yanga wanashughulika zaidi na matatizo ya wachezaji wa kigeni kuliko local players. GSM hana lengo la kuondoa matatizo ya Yanga bali anatumia matatizo ya Yanga kupatia umaarufu biashara zake. Ndio maana ananunua wachezaji yeye,anawapeleka kuwatambulisha kwenye ofisi zake yeye mwenyew bila hata kiongozi wa juu wa Yanga kuwepo. Pia Nugaz anajitapa kwamba yeye ndio aliyeenda kumshawishi GSM na yule bosi Sport pesa kusajili wachezaji dirisha dogo. Najiuliza je hayo ndio majukumu ya afisa Muhamasishaji? M/ kiti,Makamu M/kiti na katibu wa Yanga wako wapi na nini faida ya uwepo wao pale Yanga?

Namuona Nugaz akianza kufanya ya Zahera. Mda si mrefu utaibuka mgongano wa maslahi.

Hii ndo Yanga ya Msolwa msomi wa level ya Phd.

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu mliutangazia Umma kuwa Yanga ina kikosi kipana

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Yanga izuiwe kusajil haina pesa itumie wachezaji wa ndan tu brand kubwa pesa hamna warud kwa wananchi


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Back
Top Bottom