MTUNZA AMANI
Senior Member
- Jun 2, 2012
- 187
- 21
Mwenyekiti wa yanga fc amesema wanaelekea Rwanda kuitikia mwaliko wa Rais wa Rwanda Paul kagame,na amesema wakiwa huko wataweka kambi ikiwa pamoja na kufungua Tawi la yanga nchini Rwanda kwa sababu ya ushirikiano mzuiri uliopo kati ya yanga na Rwanda. Tawi hilo litashughulika na soka ikiwa ni pamoja na kuanda wachezaji kabambe katika tawi hilo. Aliongeza kuwa wakiwa huko wataweza kucheza mechi kadhaa za kirafiki ili kujiimarisha kwa ajili ya michuano ya ligi kuu inayotarajia kuanza hivi karibuni. Hii ni habari nzuri kwa wapenzi wa maendeleo ya soka na wapenzi wa club ya yanga.