MaxShimba
JF-Expert Member
- Apr 11, 2008
- 35,772
- 4,054
Hesabu duru la kwanza zafungwa:Yanga 28, Simba 14
*Wanijeria Simba 'wageuka' mabondia, wajaribu kwa kocha
Na Sophia Ashery
MIAMBA ya soka nchini Simba na Yanga jana ilimaliza ngwe ya kwanza ya Ligi Kuu Tanzania Bara kwa suluhu, ambapo Yanga iliumana na Polisi Moro Uwanja wa Jamhuri Morogoro, huku Simba ikiumana na Moro United Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Kutokana na matokeo hayo Yanga imemaliza nduru la kwanza la ligi hiyo ikiwa na pointi 28 baada ya kushinda michezo tisa, suluhu mmoja na kufungwa mmoja, huku Simba ikimaliza kwa pointi 14 baada ya kushinda mechi nne, kufungwa tano na sare mbili.
Katika mechi ya Simba jana, timu hiyo ilishindwa angalau kuwapa faraja mashabiki wake, baada ya Jumapili kufungwa bao 1-0 na Yanga, ambapo jana ilipata nafasi kadhaa za kufunga, ila umaliziaji haukuwa mzuri.
Kama washambuliaji Mussa Hassan 'Mgosi', Emmanuel Gabriel, Ulimboka Mwakingwe wangetulia, huenda Simba ingeibuka na ushindi.
Lakini Moro United nayo ilipoteza nafasi kupitia kwa Amri Kiemba, Thomas Maurice na Patrick Mangunguru.
Katika hali isiyo ya kawaida, baada ya kumalizika mchezo huo, mchezaji Mnijeria Orji Obina , alimpiga kiatu Kocha Mkuu wa Simba, Mbulgaria Krasmir Bezinsk, huku akimtuhumu kwa kitendo cha kutowapanga katika mechi yeye na Mnijeria mwenzake Emeeh Izechukwu, ambaye pia alikuwa akimtolea maneno makali kocha huyo.
Hali hiyo ilizua tafrani kwa mashabiki kutaka kuwapiga wachezaji hao, hali iliyofanya askari waliokuwa wakilinda usalama kuwatawanya mashabiki waliokuwa na hasira na kisha kuwaingiza wachezaji hao kwenye vyumba vya kubadilishia nguo.
Kutoka Morogoro, Nickson Mkilanya anaripoti kuwa mashabiki waliohudhuria mchezo huo walishuhudia washambuliaji wa timu zote mbili wakishindwa kutumbukiza mipira wavuni.
Yanga ilipata nafasi nyingi, lakini Athumani Idd, Mrisho Ngassa na Maurice Sunguti, lakini walishikwa na kigugumizi cha miguu.
Nao washambuliaji wa Polisi Moro, Fredy Hagai, Ally Moshi, Imani Mapunda na Nsa Job walipoteza nafasi nyingi za kufunga.
Kutoka Mbeya, Rashid Mkwinda anaripoti kuwa Prisons jana iliifunga Toto African mabao 2-0 Uwanja wa Sokoine mjini humo, huku mabao ya Prisons yakifungwa na Henry Mwalugala dakika 15 na Oswald Morris dakika ya 29.
Tuma kwa Rafiki Nakala inayochapika