Yamenikuta jamani!!!!!!

Yamenikuta jamani!!!!!!

Rweza79

JF-Expert Member
Joined
Feb 29, 2012
Posts
207
Reaction score
48
Habari zenu wana JF,
Miaka kadhaa iliyopita nilibaatika kukutana na msichana mmoja ambaye tulikuwa tukisoma nae miaka mingi ilyopita wakati wa shule ya msingi na kwakweli tulikuwa mabesti sana tena sana. lakini baada ya kumaliza shule ya msingi miaka hiyo kila mmoja alitawanyika kivyake mpaka miaka ya hivi karibuni tulipokutana nae, kweli upendo wangu kwake ukazidi mara dufu na ukafikia hatua ya kuwa wapenzi na hatimaye tukahamua kuoana nae. Baada ya miaka mitatu katika ndoa yetu, nikagundua mke wangu anatumia madawa fulani (phenobarbitone) na mara nilipokuwa nikimuuliza hizo dawa ni za nini alikuwa nasema huwa anatatizo la kuumwa tumbo na mara anapokunywa dawa hizo huwa anapata nafuu. lakini siku zilivyokuwa zikiendelea tatizo likazidi kujitokeza kwani akaanza kuwa anaanguka anguka na kupoteza fahamu mara kwa mara, na nilipokwenda kumuuliza dokta akasema huo ni ugonjwa wa kifafa, na akasema ni ugonjwa muda mrefu sana kutokana na vipimo alivyoviona. Dokta alishauri kuwa tusijaribu kupata mtoto kwani mara tu tutakapojaribu basi mke wangu anaweza kupoteza maisha. Sasa wanaJF, naomba ushauri wenu, kwa hali hii nifanye nini kwani raha ya maisha ni kuwa na watoto?
 
Mh! Pole sana kaka huu ugonjwa naujua,ni mbaya sana tena sana! Ushauri wewe mpe mimba! Wakati wa kujifungua ajifungue kwa oppresion,na mtoto muwekee mfanyakazi,na akuzwe kwa maziwa ya ng'ombe wa kienyeji, Muombe mungu atakusaidia
 
Ndugu yangu huku chitchat mamemba ni wapiga msuba (kasoro bishanga na mkewe The secretary) ,waliobaki ni sigara kubwa kwa kwenda mbele.Omba mods thread yako waihamishie aidha mmu au jf doctor,hapa utazenguliwa tu,tunajuana wenyewe.
 
Last edited by a moderator:
Pole mkuu wangu.
Ngoja nikuitie doctor Riwa naimani atakusaidia japo nimekusoma kama unataka alternative ya kupata mtoto.
 
Last edited by a moderator:
Phernababitone sio dawa za pumu?
Muhimu ni kutafuta matibabu kwanza kwa ajili kifafa, na uongee na daktari kuhusu hilo. Baada ya hapo mnaweza kuongea na dr wa wanawake kuhusu uwezekano wa kupata mtoto na hali hiyo.

Nikuambie kitu ndugu, mtoto ni majaaliwa ya mwenyezi Mungu. Angalia usihuzunike kwa sababu mwenzi ana kifafa ukaanza kumfanyia ubaya. Nani anajua kama wewe ni mzima? Tuchukuliane mizigo kwa upendo.
 
Pole sana mkuu Rweza 79 huyo ni mke wako japo alifanya kosa kukuficha lakini ni vyema ukamsamehe na mkaendelea na maisha ya ndoa! Siwezi kukushauri kumuacha maana hilo tatizo linaweza kumpata mtu yeyote.Pengine aliogopa kukupoteza! Hicho kinaweza kikawa kipimo cha upendo wa kweli kwake!

Habari zenu wana JF,
Miaka kadhaa iliyopita nilibaatika kukutana na msichana mmoja ambaye tulikuwa tukisoma nae miaka mingi ilyopita wakati wa shule ya msingi na kwakweli tulikuwa mabesti sana tena sana. lakini baada ya kumaliza shule ya msingi miaka hiyo kila mmoja alitawanyika kivyake mpaka miaka ya hivi karibuni tulipokutana nae, kweli upendo wangu kwake ukazidi mara dufu na ukafikia hatua ya kuwa wapenzi na hatimaye tukahamua kuoana nae. Baada ya miaka mitatu katika ndoa yetu, nikagundua mke wangu anatumia madawa fulani (phenobarbitone) na mara nilipokuwa nikimuuliza hizo dawa ni za nini alikuwa nasema huwa anatatizo la kuumwa tumbo na mara anapokunywa dawa hizo huwa anapata nafuu. lakini siku zilivyokuwa zikiendelea tatizo likazidi kujitokeza kwani akaanza kuwa anaanguka anguka na kupoteza fahamu mara kwa mara, na nilipokwenda kumuuliza dokta akasema huo ni ugonjwa wa kifafa, na akasema ni ugonjwa muda mrefu sana kutokana na vipimo alivyoviona. Dokta alishauri kuwa tusijaribu kupata mtoto kwani mara tu tutakapojaribu basi mke wangu anaweza kupoteza maisha. Sasa wanaJF, naomba ushauri wenu, kwa hali hii nifanye nini kwani raha ya maisha ni kuwa na watoto?
 
Last edited by a moderator:
Hapana kingasti sio dawa ya pumu, hi inatumika kutibu maradhi yanayoathiri mfumo wa ubongo mfano epilepsi yani kifafa, au wangonjwa wa madawa ya kulevya.. Etc
 
Jaribu kwenda kw madoctor wa neurology, anaweza kuchange dawa akapawa ambayo haiwezi kumuathiri mtoto tumboni (less or non teratojenic drug) , ithink dr amesema hawezi kuzaa kutokana na dawa anazotumia,,ataweza kuzaa inshaAlah
 
Hapo ndipo pa kumuonyesha upendo mwenzio au hukuapa kile kiapo cha 'till death do us part'
Jaribu kuwa-consult wataalam..sidhani kama watu wa namna hii huwa hawaruhusiwi kabisa kuzaa!,nadhani iko namna ya kushughulikia cases kama hizi...pole sana ndugu yangu!!
 
Pole bwana, pagumu hapo ukizingatia moja ya mavuno ya ndoa ni watoto, ila uckate tamaa endelea kuhangaika kwa njia zote zitakazowezekana.
 
Broda pole sana kama usha waona maDr basi fuata ushauri wao usilazimishe mambo pia ningependa umkabithi Mungu hili jambo naamin kwake hakuna kitu kinacho shindikana.Amani ya Bwana iwe nawe mkuu...
 
Phernababitone sio dawa za pumu?
Muhimu ni kutafuta matibabu kwanza kwa ajili kifafa, na uongee na daktari kuhusu hilo. Baada ya hapo mnaweza kuongea na dr wa wanawake kuhusu uwezekano wa kupata mtoto na hali hiyo.

Nikuambie kitu ndugu, mtoto ni majaaliwa ya mwenyezi Mungu. Angalia usihuzunike kwa sababu mwenzi ana kifafa ukaanza kumfanyia ubaya. Nani anajua kama wewe ni mzima? Tuchukuliane mizigo kwa upendo.

hapana ni dawa za kifafa kweli
 
Funzo hapa, vijana mnaotafuta msivamie tu bila kujua kinachomsibu mwenzako, familia yake etc ili kama unakubaliana nayo ujipange. Nakupa pole ndugu yangu, i feel the problem as i meet them in my daily activities
 
Pole sana mkuu kwa tatizo hili ambalo limekukuta.Cha msingi ni kufuata ushauri wa kitaalamu wa Doctor aliokupa ili mkeo aweze kuishi salama.Ukiforce kumpa ujauzito,hali inaweza kuwa mbaya zaidi
Ushauri kwa Wengine ambao hawajaingia kwenye ndoa
Ni vema kushirikishana na mwezio matatizo ya kiafya ambayo unayafahamu ili unapofanya maamuzi ya kufunga ndoa uwe unajua fika tatizo alilonalo mchumba wako.Katika hatua hii ni vema wote muwe wawazi ili mbele ya safari isijeonekana ulifanya makusudi kutoweka wazi tatizo lako na kuwa kikwazo kwa mwenzio.Hapo zamani baba zetu walikuwa wanazingatia sana hatua ya kuchunguza matatizo ya kiafya kabla ya kufikia uamuzi wa kuruhusu ndoa ifungwe.Kizazi hiki kwakuwa tuna uhuru wa kufanya mambo wenyewe,basi tusisahau kushirikishana matatizo ya kiafya au kufanya basic Health Check up kabla ya ndoa.
 
mwenzio hakupenda awe hivyo. hayo ni matatizo katika dunia hii iliyojaa uchafu wa kila aina katika ulimwengu wa roho. jambo la kwanza la msingi onyesha upendo kwa huyo mkeo kwani anahitaji upendo wako na kujali kwako!

jambo la pili wewe na mwenzio mkubalini Bwana Yesu awe mwokozi wenu. mpeleke mkeo akafanyiwe maombezi ili hilo pepo kifafa limtoke na atakuwa mzima wa afya. watoto mtapata na maisha yenu yatakuwa ushuhuda kwa wengine wenye tatizo kama la mkeo.
 
Ndugu yangu RWEZA97 umenikumbusha mbali sana.wifi yangu alikaa miaka tisa kwenye ndoa bila ya mafanikio ya mtoto lakini hata siku moja mume wake hakumuonyesha kuwa hilo linamkwaza.Aliendelea kumuheshimu na kumthamini kama mke huku akiamini kuwa siku moja Mungu atawajalia watoto na sio mtoto.Kikubwa ni kumwamini Mungu na kupata ushauri/tiba kwa daktari.Mtoto katika ndoa ni majaliwa ya mwenyezi Mungu na ili maisha yenu katika ndoa yasimame imara, yakupasa kumuonyesha mkeo mapenzi ya dhati katika mapito hayo.Kuna mambo yanayotokea huku duniani ili binadamu adhihirishe kipimo cha imani yake kwa Mwenyezi Mungu.Kumbuka hilo ni jaribu na inakupasa kulishinda.Mungu akupe nguvu ya kuomba ili siku moja uweze kushuhudia ukuu wake.Kumbuka huo ni ugonjwa.Mimi binafsi naamini uponyaji kupitia dawa,hivyo ni maombi na tiba maana hata dawa zililetwa na mwenyezi Mungu.
 
Mshukuru Mungu kwa yote,pili waone madaktari watakupa ushauri,ili kumbuka uliapa kwamba si dhiki wala magonjwa vitakavyokutenganisha na mkeo........Mpende na mlinde mkeo huku ukimpa moyo wa faraja.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom