Waberoya
Platinum Member
- Aug 3, 2008
- 15,169
- 10,786
Umenena vyema...sasa kama wote ni walewale kwa nini wengine wachafu hawasemwi..ili silaha na vita iwe kali na hatimaye CCM itoke madarakani kirahisi...Bwana/Ndg Mjengwa kama kawaida yako umeandika article nzuri lakini yenye prophecies nyingi kuliko majibu.
Kitu nataka nikuambie damu ya kumsafisha Lowassa bado haijaumbwa au kutengenezwa. Wenye kuchafua jina wanazo silahanyingi wanazoweza kutumia pindi zitakapohitajika. To start with wanaweza wakatafuta faili la kambarage.
Kinachotokea sasa ni kwamba anakosekana mtu msafi wa kumtunga kidole Lowassa. Wote ni walewale. Subili ile siku atakayokutana ana kwa ana na wana CDM. Ndiyo siku yake ya kulia na kusaga meno. Sisi yetu macho na kupiga kura.
Maggid hana makosa, kama tunataka ukweli tuwachonganishe..usije ukakuta kuna siku mtu anahama nchi!
Yaani kwa Maggid kuandika makala hii...si ni kiberiti au msukumo tosha wa wengine kutoa hizo silaha? kwanini?