Yako wapi magari ya Lake Oil?

Yako wapi magari ya Lake Oil?

Tutor B

JF-Expert Member
Joined
Jun 11, 2011
Posts
9,025
Reaction score
6,614
Waungwana,

Mwaka jana tulikuwa tunaona magari makubwa ya mafuta yenye chata ya Lake Oil, ila kipindi cha mwisho wa kampeini za uchaguzi magari hayo hayakuonekana barabarani tena hadi sasa.

Hivi kilitokea kitu gani kwa hayo magari, na je! Mmiliki wa magari hayo alikuwa nani? Kama anajulikana hana harufu ya watumbuliwaji?

lakeOill.jpg

Picha ya mfano wa magari ya LakeOil
 
Mimi mwenyewe nilikuwa najiuliza swali hili sana,nikajua nihapa nilipotu .
Miji yote magari haya yalikuwa yanaonekana kwa sana yakiwa barabarani .. imekuwaje yakapotea ghafla??
 
miezi michache iliyopita Takukuru ilisema inafanya uchunguzi wa kesi ya hii kampuni ya kukwepa kodi ya shilingi bilioni 8 kwa kuuza mafuta nchini mafuta ambayo yalitakiwa kupelekwa Congo badala yake yakauzwa hapa, serikali ikakosa mapato.
 
miezi michache iliyopita Takukuru ilisema inafanya uchunguzi wa kesi ya hii kampuni ya kukwepa kodi ya shilingi bilioni 8 kwa kuuza mafuta nchini mafuta ambayo yalitakiwa kupelekwa Congo
ALAFU NASIKIA VITUO VYAKE VYA MAFUTA MAUZO WALIKUWA HAWAPELEKI HELA BENK, KULIKUWA NA MAGALI LAND CRUICER NDO YALIKUWA YANAPITA NA KUKUSANYA PESA ..
 
Tena hawa jaamaa wanadaiwa pesa nyingi na serikali kwa kukwepa kodi, vipi wameshalipa au upepo ulipita tu.
 
Ile serikali ya wapigaji si imeshaondoka ,hayawezi kuwa barabarani
 
Kama yameuliwa nahisi ajira kubwa sana itakuwa imepotea
 
Back
Top Bottom