mukizahp2
JF-Expert Member
- Jul 28, 2012
- 705
- 378
Wote weziBy the way huwezi kumlinganisha Ombeni na Kinana. Kinana ni namba nyingine
Wote weziBy the way huwezi kumlinganisha Ombeni na Kinana. Kinana ni namba nyingine
Kinana ataendelea sana kudumu hadi 2017. Ila wasaidizi wake akina Nape, Luhwavi, Asha Rose na Zakhia Meghji hawana muda kwenye sekretarieti mpya
Pamoja na kazi nzuri ya Nape chamani, hili la yeye ama wengine waliokwisha teuliwa na kupewa kazi nzito za kitaifa kama uwaziri sidhani kwamba wanatakiwa kuwemo kwenye secretariat. Katika hotuba yake nilimsikia Mwenyekiti mpya akizungumzia hilo la mtu mmoja kuwa na vyeo vingi bila sababu wakati wapo wengine wenye uwezo wa kushika nafasi husika.Nape yupo saana tu.Kazi aliyoifanya wakati ule wa kampeni ilikuwa kubwa sana.
Uwezekano wa kumuondoa Kinana kwenye nafasi yake soon ni mkubwa. Huwezi ondoa safu ya uongozi yote at the same time. But Kinana should know. He has NO future in CCM under Magufuli. Mark my words.
Kwa silka na hulka ya utendaji wa Mwenyekiti mpya wa CCM, Dkt Magufuli, na hasa kwa kutowakubali, (yawezekana kwa kutowaamini), wateule na watendaji wakuu wa Mtangulizi wake, sioni dalili za Uteuzi wa Ndg Kinana kuwa Katibu Mkuu Mpya wa CCM, kudumu kwa muda hata wa siku 100.
Licha ya sifa kemkem alizopewa Dodoma, kuna uwezekano mkubwa yale yaliyomkuta aliyekuwa katibu mkuu kiongozi Ndg Sefuwe, yakamkuta Kinana, tukaishia kuambiwa, "ATAPANGIWA KAZI NYINGINE"
Muda haudaganyi Tusubiri.