atabadilishaje kadi asipolipa kodi au akimuuzia mtu mwingine si lazima alipe hizo kodi?
Mkuu wa mkoa wa Mwanza, mteule wa JK mh. ABASI KANDORO, amefanya kufuru ya mwaka kwa kujiuzia gari la kifalme lililogarimu wavuja jasho zaidi ya milion 300/= ambalo wanaharakati tumekuwa tukiyapigia kelele kwa pesa za kitanzania Tsh. 2,000,000 tu.
Gari hilo ni VX TOYOTA LANDCRUISER, LENYE SPEED MITA 240, namba za usajili STK 3643 lililonunuliwa na mtangulizi wake kwa matummizi ya OFISI YA MKUU WA MKOA wa Mwanza.
Gari hilo lililonuliwa na mkuu wa mkoa kabla ya Kandoro bado ni mpya na hali yake ni nzuri sana, wala halijamaliza hata miaka 10 likitumika.
Baada ya kandoro kufika mwanza, alilikataa kulitumia na kusema kuwa halifai kuwa la mkuu wa mkoa na hivyo alitenga fedha la kununua gari lingine la kifahari zaidi LANDCRUISER V8, BEI MILLION 400/= speed mita 260 ambalo ndilo analolitumia mpaka sasa.
Baada ya kununua gari hilo la kifalme, gari la awali lilipewa namba za serikali STK 3643 na kupaki kwenye ofisi za mkoa na mara chache sana kutumika mkoani.
Ndipo Mh. Abasi kandoro akaunda mbinu za kujiuzia gari hilo alilolikataa kwa madai kwamba halifai kuwa la mkuu wa mkoa, akijiuzia kwa Tsh. 2,000,000/= milion mbili pesa za kitanzania.
Kwa sasa yuko kwemnye hatua za mwisho za kupata kibali, ili aondoe hiyo STK, na kubandika namba za kiraia anze kula maisha na gari hilo la kifahari lililogarimu pesa za walipa kodi karibu au zaid ya 300,000,000/= na kuuzwa kwa bei ya kifisadi 2,000,000 tu.
Nawasilisha tafadhali.
mtoto wa mama ..... Wewe unajua nini zaidi ya kula na kulala bure ...... Ha haaa haaaaa
Watanzania tupunguze majungu tufanye kazi. Kila taasisi ina kitu kinaitwa "Disposal Policy" kwamba gari likifikisha Kilometer/miaka flani linauzwa linanunuliwa lingine. Wengi hutumia Kilometer 250,000 au miaka mitano. Hata kama gari lilinunuliwa kwa 300 million baada ya kutumika miaka mitano thamani yake haitabaki kuwa 300 milion tena kutokana na uchakavu ambao utakuwa umekadiriwa kuwa 60 million kwa mwaka kama Policy yao ni miaka mitano.
Ila kwa swala la kuuzwa 2 million, kama ndio bei iliyopatikana kwa ushindani "Tender process" bado mtu hawezi kuhoji. Ila kabla ya kutangaza tender ilitakiwa gari hili lifanyie "valuation" kujua market value na hivyo lisingeweza kuuzwa chini ya "market value
Kandoro si wa kwanza kufanya hivyo huo ni utaratibu wa kawaida tu kwa viongozi wengi hasa wa serikali kuu na Taasisi mbalimbali kujiuuzia magari ya thamani kubwa kwa bei sawa na bure.
Tena hizo milioni 2 za kandoro ni nyingi sana kuna watu wananunua GX kwa laki tisa (900,000/=) tu, yaani ufisadi ni mkubwa sana serikali kuu na kwenye taasisi za serikali ila chakushangaza watu wanapiga kelele kuwa halmashauri zinaongoza wakati sio kweli, asilimia kubwa ya wizi kwenye halmashauri ni chini ya milioni 10 tu.
Mkuu, fafanua hapo kweye red, onesha formula unayotumia kukokotoa! au unaongea tu kama mtoto mdogo? SHAME ON YOU!Nyambala, hakika tuko pamoja! Huyo mtoa taarifa atujuze hilo Landcruiser la 300m ni toleo la mwaka gani? Maana taarifa inadai kuwa halijafikisha hata miaka 10 likitembea, kwa maana kwamba angalau limetembea miaka zaidi ya 5. Ikumbukwe kuwa kwa viwango vya magari hususani Toyota, gari likitembea miaka 5 be it in Tanzania or elsewhere, thamani yake inashuka almost to 0.
Sina nia ya kumtetea Mhe. Kandoro, ila lazima nasi tujaribu kuwa makini na baadhi ya habari zinazowekwa hapa jamvini na tuchangie bila ushabiki wa kiitikadi....
lini kama siyo sasa kwa sababu we will die anyway kama si kwa maboom kama gongolamboto basi kwa treni, na kama si hivyo kwa meli hawa watu bora kupambana nao sasa kwa mapanga tuu! Utaona mnaniita mchochezi eeeti!kuna siku watakuja kulipa ipo siku tuu,wasidhani ccm itakaa madarakani milele
yaani huyo ni zero kabisaa!mkuu, fafanua hapo kweye red, onesha formula unayotumia kukokotoa! Au unaongea tu kama mtoto mdogo? Shame on you!
Kuna siku watakuja kulipa ipo siku tuu,wasidhani CCM itakaa madarakani milele
mulika mwizianyang'anywe na ashitakiwe!
|
| |||||||||
|
| |||||||||
|
| |||||||||
|
| |||||||||
|
| |||||||||