Gazeti hili na hasa makala ya Johson Mbwambo ni za chuki za wazi kwa JK imekuwa ada kwa makala za Mbwambo kila wiki kumsema,kukejeli na kumkosoa vibaya JK.kwa muda mrefu sana hali hii inatia kinyaa na kumuona Mbwambo ni mtu asiyeaminika.Tukumbuke kuwa kabla ya kampeni za uchaguzi mtu huyu aliandika makala huku akisema kuwa Waandishi wazingatie maadili katika kipindi hiki.
Lakini mlolongo wa makala zake toka mwanzo wa kampeni umeanza kwenda kinyume na kile alichokiandika kabla ya kampeni.Umeanza kuonyesha kuwa Mbwambo amekuwa na agenda yake iliyojificha dhidi ya JK.Mara aseme kimfaacho Jk ni asasi na si urais huku akisahau kuwa ni Kikwete huyu huyu ambaye amekuwa madrakani kwa miaka mitano iliyopita huku Mbwambo akiwa kama mwananchi wake. Hili ameliandika katika makala yake ya jana 06/10/2010.Amefikia mahali akathubutu hata kuandika kuwa inafaa JK akajifunze kwa Rais Kagame wa Rwanda.Sina hakika kama alitaka JK akajifunza kutumia nchi za wengine kufadhili ghasia na kutumia nafasi hiyo kusaidia nchi yake au alimaanisha JK akajifunze jinsi ya kuwanyima wapinzani uhuru na kutishia vyombo vya habari,sijui hasa alimaanisha nini.Labda Watanzania wenzangu mtanisaidia.
Hivi Ukubwa wa Tanzania utaufananisha na Rwanda? kama kujifunza kwanini Kagame wa Rwanda asije kujifunza kwa JK KWENYE ujenzi wa Chuo kikuu cha kuigwa cha Dodoma?Mbwambo hivi Rwanda wana chuo kama UDOM? umeshindwa kumpa heko JK hata kwa jambo kama hilo?Au wewe ndo ulipanga shughuli hiyo?Maandishi ya MBWAMBO hayana tofauti na mwandishi anayetumia jina la bandia anayejiita MSOMAJI RAIA hawa ni kama mapacha na Mbwambo kuanzia mtiririko wa uandishi wao,mawazo hasi dhidi ya JK, chuki zao za wazi zisizo na sababu kwa JK .HUYU MSOMAJI RAIA kaanza kuandika toka mwaka jana kuwa Rais Jk hashauriki. Hiyo ilikuwa mwezi wa tisa 2009. mwaka huu kajisahau kaandika kuwa Rais Kikwete anasikiliza marafiki zake sana. sasa mtu ambaye hashauriki atasikiliza marafiki na watu wake wa karibu?Cha ajabu minal rahman Mbambo kawahi kuandika makala kumsifu waziri Mkuu Mizengo Pinda kama waziri makini na mtendaji ni swali je aliyemteua Pinda si ndio JK? kazi hizo zinazo mfurahisha Mbwambo ndizo za JK.anafanya kwa maelekezo ya JK. HII NI DOUBLE STANDARDS.MFANO gazeti la jumatano ya jana Mbwambo karudia habari ya World Economic Forums uliofanyika Dsm 5-7 Mei 2010.
huko nyuma aliwahi kuandika makala ya kukebehi mkutano ule kwa vile tu mgeni Rasmi alikuwa JK.imekuwa kama Mbwambo ana allergy na jina la JK.ameamua kuwa anarudia rudia maneno ya kumchafua JK.NAJIULIZA kama Mbwambo angepewa fursa ya kuambiwa ukimuombea jambo jema moja jirani basi wewe utapata mara mbili, yaani kama ukiomba jirani awe na nyumba basi Mwenyezi Mungu atakupa nyumba mbili. kwa Mbwambo angeomba yeye atolewe jicho moja ili Jk akose macho mawili.masikini maombi huombwa kwenye mambo mema tu.
Napata ugumu kujua kama Raia mwema ni gazeti la Kina Ulimwengu au ni la Padri Slaa? maana Tanzania Daima inajulikana ni la Mbowe na hili ni la Slaa?
Naishia hapa kwa sasa.
MUNGU IBARIKI TANZANIA
Lakini mlolongo wa makala zake toka mwanzo wa kampeni umeanza kwenda kinyume na kile alichokiandika kabla ya kampeni.Umeanza kuonyesha kuwa Mbwambo amekuwa na agenda yake iliyojificha dhidi ya JK.Mara aseme kimfaacho Jk ni asasi na si urais huku akisahau kuwa ni Kikwete huyu huyu ambaye amekuwa madrakani kwa miaka mitano iliyopita huku Mbwambo akiwa kama mwananchi wake. Hili ameliandika katika makala yake ya jana 06/10/2010.Amefikia mahali akathubutu hata kuandika kuwa inafaa JK akajifunze kwa Rais Kagame wa Rwanda.Sina hakika kama alitaka JK akajifunza kutumia nchi za wengine kufadhili ghasia na kutumia nafasi hiyo kusaidia nchi yake au alimaanisha JK akajifunze jinsi ya kuwanyima wapinzani uhuru na kutishia vyombo vya habari,sijui hasa alimaanisha nini.Labda Watanzania wenzangu mtanisaidia.
Hivi Ukubwa wa Tanzania utaufananisha na Rwanda? kama kujifunza kwanini Kagame wa Rwanda asije kujifunza kwa JK KWENYE ujenzi wa Chuo kikuu cha kuigwa cha Dodoma?Mbwambo hivi Rwanda wana chuo kama UDOM? umeshindwa kumpa heko JK hata kwa jambo kama hilo?Au wewe ndo ulipanga shughuli hiyo?Maandishi ya MBWAMBO hayana tofauti na mwandishi anayetumia jina la bandia anayejiita MSOMAJI RAIA hawa ni kama mapacha na Mbwambo kuanzia mtiririko wa uandishi wao,mawazo hasi dhidi ya JK, chuki zao za wazi zisizo na sababu kwa JK .HUYU MSOMAJI RAIA kaanza kuandika toka mwaka jana kuwa Rais Jk hashauriki. Hiyo ilikuwa mwezi wa tisa 2009. mwaka huu kajisahau kaandika kuwa Rais Kikwete anasikiliza marafiki zake sana. sasa mtu ambaye hashauriki atasikiliza marafiki na watu wake wa karibu?Cha ajabu minal rahman Mbambo kawahi kuandika makala kumsifu waziri Mkuu Mizengo Pinda kama waziri makini na mtendaji ni swali je aliyemteua Pinda si ndio JK? kazi hizo zinazo mfurahisha Mbwambo ndizo za JK.anafanya kwa maelekezo ya JK. HII NI DOUBLE STANDARDS.MFANO gazeti la jumatano ya jana Mbwambo karudia habari ya World Economic Forums uliofanyika Dsm 5-7 Mei 2010.
huko nyuma aliwahi kuandika makala ya kukebehi mkutano ule kwa vile tu mgeni Rasmi alikuwa JK.imekuwa kama Mbwambo ana allergy na jina la JK.ameamua kuwa anarudia rudia maneno ya kumchafua JK.NAJIULIZA kama Mbwambo angepewa fursa ya kuambiwa ukimuombea jambo jema moja jirani basi wewe utapata mara mbili, yaani kama ukiomba jirani awe na nyumba basi Mwenyezi Mungu atakupa nyumba mbili. kwa Mbwambo angeomba yeye atolewe jicho moja ili Jk akose macho mawili.masikini maombi huombwa kwenye mambo mema tu.
Napata ugumu kujua kama Raia mwema ni gazeti la Kina Ulimwengu au ni la Padri Slaa? maana Tanzania Daima inajulikana ni la Mbowe na hili ni la Slaa?
Naishia hapa kwa sasa.
MUNGU IBARIKI TANZANIA