Mwanakili90
JF-Expert Member
- Nov 24, 2010
- 1,568
- 246
Asante mkuu,hawa jamaa nimebahatika kuwa nao karibu kipindi bado nipo Arusha! Faza Nelly alikuwa anaaminika ndio the best Hiphop Artist ever in Arusha! Binafsi mpaka kesho naamini hivyo na ndio alikuwa kichwa wa kundi! Mafanikio ya kundi lao hayajawahi kuvunjwa rekodi na kundi lolote Tanzania hii! Ndio wasanii wa kwanza wa Hiphop video yao kurusha Channel O! At that time our video quality was extremly poor lakini hawa jamaa walikuwa level nyingine! Walikuwa wanaitwa kupiga shows Senegal,SA,USA,Holland etc while hapa Bongo walikuwa hawaitwi sababu wanyonyaji walikuwa hawawezi kuwalipa wanavyotaka! Hawa jamaa walikuwa wanakutana na kuheshimiwa na Ma legend kibao wa Mbele! Na amini usiamini hawa ndio waliofanya huko duniani kujua Tanzania kuna Hiphop! Jamaa style yao ilikuwa ni hiphop masai na walifunika sana tu ila tatizo Faza Nelly ndio alikuwa mtunzi na mbunifu sana ndio maana kama alikufa na kundi.Muulize mwanahiphop yeyote wa Arusha kuhusu Faza Nelly uambiwe! Msiba wake ni moja ya misiba iliyopata mahudhurio makubwa mno Arusha.RIP FAZA NELLY!(Faza Nelly)
From the album 'Maasai hip
hop' (Out Here records, 2004) Swahili lyrics (English intro): All my people
East Africa
Tanzania, Uganda and Kenya
Dar es Salaam, A town
Wherever you are
Piga magoti, tuombe Mungu Hii ni siasa, dini, vita, ubwana,
utwana, au kiama ghalika,
sodoma na gomora?
Simama imara, zunguka kila
kona, kila anga angaza
Kushoto, kulia, mbele, nyuma kote pitia
Na hapo ulipojishikiza
g'ang'ania, sikilizia, vumilia
baadae usije jutia Hii ni mahususi na maalum
kwa watu wangu
Walemavu, vipofu, zeruzeru na
wendawazimu
Watoto wa mitaani, fukara,
masikini na wenye akili zao timamu
Hii kamba ngumu
Mjue tunavutana na wenye
nguvu
Vitambi na mashavu
Hakuna tena fair game Refarii kauzu
Uwanja wenyewe mkavu
Ujira mgumu, malipo finyu
Kilichobaki kucheza rafu
Tumechoshwa na ukabaila,
ubepari na ubeberu
Wakati ndo huu
Ukombozi ndo huu
Na sasa naamuru mliopo chini
wote mpate divai ya vinibu
Mtetezi wenu nikaze gidamu
Nimwage sumu ya upupu juu yao
Wajikune bila aibu
Kwanza saluti kwa
waliyotangulia kuzimu
Pili tuombe Mungu
Baba yetu, utupe mkate wetu wa kila siku
Utujaze nguvu
Tupate kudumu ndani ya game
Tutakapofika kuzimu siku ya
hukumu
Utupe nafasi tupate kutubu Kwani tunajua tunatenda
maovu
Tunakula haramu
Tunatumia kila mbinu
Juju, uhalifu, upanganyifu
Ili tuweze kujikimu Lakini isiwe kisingizio kwa
wanadamu wengine
kunyimwa haki zetu
Kutuzibia riziki zetu
Kutuita makafiri, dharau na
kutukashifu Kwani nini dhambi
Chorus :
Nini dhambi kwa mwenye
dhiki,
Kipi haram, kipi halali,
Kila mmoja anaitaka hii riziki
Kitendawili, vurugu mechi Huwezi tabiri Kwa nini ?
Uliza swali, kama
sote tungekuwa wasomi,
matajiri
Ni nani angelifanya kazi za
kutisha na hatari mfano ya
mochwari Kila mmoja wetu hapa mjini
kaja kwa dili
Kila kitu, kila mahali
Na hata ngozi ya mtu dili
Wengine wachawi, waganga
feki Matapeli, wasafiri kafiri
Wakati wengine wapole kama
walokole
Mchana pirika nyingi maofisini
Kumbe night kali, kahaba
Shuga, jambazi, mengine ya kusitiri
Ah!
Wapo waliopoteza maisha
katika kufight life
Kumbukumbu zao zimebaki
makaburini Na wapo waliopoteza kabisa
tumaini la kuwini
Hao roho zao utadhani
wamezitoa rehani
Wakikutight mahali fulani
Inabidi uwakabidhi mshahara wote wa mwisho wa mwezi
(Chorus)
Kweli Bongo kutafuta braza
Utajajuta utakapojikuta huna
hata bukta
Shauri yako we tegesha tu
kama golikipa
Na hao unaowategemea mwishowe watakutosa
Huna elimu, hun fani
Lakini nguvu, hulimi, uchumi
unao unaukalia
Kumbuka
Kupata au kukosa yote ni kawaida
Sometimes unalala unaota
unakula
Unakunywa, unapiga denda
Na kula uroda na demu bomba
Ukikurupuka tu unakuta patupu
Hakuna kitu
(Chorus, Yamat singing a
traditional Maasai song)
naomba mwenye kujua jina la albam yao ya kwanza. nimeshindwa nipateje nyimbo zao hawa jamaa. Msaada jamani. Mia
USHANTA! Umenikumbusha mbali sana mkuu! Wakati Arusha ikiwa Arusha kweli na machizi wa Mbuguni!R. I. P Father Nelly kwa kwel huyu jamaa na Kundi lao la Xplastaz ni icon nzur sana kwa Hip Hop ya Bongo nawakumbuka sana na Hip Hop Masaai yao....Wimbo kama USHANTA, HAAAA HAAAAA na kadhalika kadhalika..naona sasa hivi kuna Madogo wanaliendeleza vizur kundi..
Ayaaa! Umeua chali angu! Dah!nilikuwa nakisaka kinasa,sasa nimekipata,raffu....raffu nelly ...na mneli....
wakuu hawa ndio artists wa ukweli tanzania.
Kuna rapa kutoka Xplastaz ivi karibuni alipafomu kwenye tuzo za BET ile sehemu ya freestyle battle,simpati jina..huwezi amini hawa jamaa wanafahamika nje zaidi ya bongo.
Kuna rapa kutoka Xplastaz ivi karibuni alipafomu kwenye tuzo za BET ile sehemu ya freestyle battle,simpati jina..huwezi amini hawa jamaa wanafahamika nje zaidi ya bongo.
Asante mkuu,hawa jamaa nimebahatika kuwa nao karibu kipindi bado nipo Arusha! Faza Nelly alikuwa anaaminika ndio the best Hiphop Artist ever in Arusha! Binafsi mpaka kesho naamini hivyo na ndio alikuwa kichwa wa kundi! Mafanikio ya kundi lao hayajawahi kuvunjwa rekodi na kundi lolote Tanzania hii! Ndio wasanii wa kwanza wa Hiphop video yao kurusha Channel O! At that time our video quality was extremly poor lakini hawa jamaa walikuwa level nyingine! Walikuwa wanaitwa kupiga shows Senegal,SA,USA,Holland etc while hapa Bongo walikuwa hawaitwi sababu wanyonyaji walikuwa hawawezi kuwalipa wanavyotaka! Hawa jamaa walikuwa wanakutana na kuheshimiwa na Ma legend kibao wa Mbele! Na amini usiamini hawa ndio waliofanya huko duniani kujua Tanzania kuna Hiphop! Jamaa style yao ilikuwa ni hiphop masai na walifunika sana tu ila tatizo Faza Nelly ndio alikuwa mtunzi na mbunifu sana ndio maana kama alikufa na kundi.Muulize mwanahiphop yeyote wa Arusha kuhusu Faza Nelly uambiwe! Msiba wake ni moja ya misiba iliyopata mahudhurio makubwa mno Arusha.RIP FAZA NELLY!