If I was a 'dude' maybe. . .lolz
Nwy. . Binafsi nadhani mtu anaweza akawa na zote, za mke na za girlfriend, za mume na za boyfriend. Tatizo ni kwamba wengine wakishaingia kwenye ndoa hata kama mwanzoni walikua exciting, fun, sweet, caringand wild chumbani basi wanaacha kwasababu wanaona hawahitaji tena kuwa walivyokua kwasababu ndege yupo tunduni tayari. Maisha yanaanza kurevolve around 'bills' na 'pesa za matumizi'. . Simu zikipigwa/text zikitumwa sio za 'umeshakula mpenzi? Nimekumiss!! Nakupenda!! Jana ulifanya siku yangu nzuri sana!!" ni za "Ile pesa mbona hukuacha? Hao walevi wenzako ndio muhimu ehhh? Mi naenda kwa shogangu??Sitorudi nyumbani leo! Sina pesa" n.k
Maisha yanakua stressful tena bila mtu wa kusaidia kuzipunguza kwasababu mtegemewa ndie anaesababisha. Sauti (tone) ndani ya nyumba inabadilika, unyumba leo huyu akimnyima mwenzie kesho mwingine nae anakataa, mama anamwachia kila kitu housegirl wakati kipingi cha 'upenzi' alikua analazimisha akamsafishie mwanaume chumba kila wiki na kumpikia hata weekend, mama anaona kitanda hakitoshi (kidogo anabanwa) wakati kipindi cha upenzi alikua analalamika ni namna gani anahisi upweke usiku, mwanaume akitoka kazini anaenda kupata kinywaji kwanza kwasababu kukutana na mke bila kinywaji ni mwanzo wa maumivu ya kichwa wakati kipindi cha upenzi alifanana na mtu asiyekunywa na mengine kama hayo.
Watu hua wanadai kwamba majukumu ndio yanayowabadilisha ila mimi nasema hapana. Majukumu yanaweza yakambadili mtu kidogo na sio kumfanya awe mtu mwingine kabisa kama ilivyo kwa baadhi ya watu.
Maintain a lil bit of you crazy self, your silly self, your sweet self, your charming self, your caring self, your wise/smart self, your generous self and enjoy life. That way your man/woman will enjoy having you just aswell.