Wosia wa baba wa Taifa

Wosia wa baba wa Taifa

Muwazi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2014
Posts
355
Reaction score
81
Hakuna serikali yoyote duniani inayoendeshwa bila miiko. Ukipewa kazi ya nchi lazima ujiheshimu . Huwezi kupewa kazi ya nchi halafu unaishi kihunihuni. Kazi ya kihunihuni nenda kafanyie barabarani kule.
 
Wakubwa wakissema hakuna,hakuna,Unachukua mali kwa masikini unapeleka kwa matajiri?,Mfumo gani huo?,mfumo wa kiahetani huo!.
 
Kulitaja azimio la Arusha lazima uwe na moyo wa mwendawazimu!
 
Ana vigezo vyote vya kuwa rais, lakini aah, ni mkara!
 
CCM siyo mama yangu, ikiacha misingi yake ya kutetea wananchi wanyonge, naweza kuachna nayo.......

Naamini kama Mwalimu Nyerere angekuwa hai leo angeachana na CCM na kujiunga na CDM kutokana na CCM kuacha misingi yake ya kuwatetea wanyonge na kuwakumbatia mafisadi, hadi kufikia Rais wa nchi akadiriki kutoa msamaha kwa majizi yaliyokwapua mabilioni ya EPA kwa kuwaambia warejeshe tu hayo mabilioni waliyoiba ili soo iishe!!!
 
♥unawexa wewe ukawa mwaminifu kabisa lakini haitoshi inabidi uwe na uwezo wa kuwaambia rafiki na ndugu zako ikulu ni mahali patakatifu mimi sikuchaguliwa kuja kupageuza pango la wala rushwa

♥Ikulu kuna biashara gani pale? ikulu ni mzigo mie nimekaa pale miaka 20 na mi5 ukiona mtu anakimbilia ikulu muogope kama ukoma.

♥serikali corrupt haikusanyi kodi itabaki kukimbizana na wafanya biashara ndogondogo na kukumbatia wenye mali.
 
Nimesoma katiba za vyama mbali mbali vya upinzani, sijaona chama makini zaidi ya Chadema ambacho ndiyo pekee nakiona kina dalili ya kuwakomboa wanyonge wa nchi hii.....

Maneno hayo aliyatamka Mwalimu Nyerere, mwaka 1995, baada ya uchaguzi mkuu, jambo linaloonyesha Mwalimu alikuwa akipewa maono na Mungu ya yale yatakayokuja baadaye hapa TZ
 
Wakubwa wameenda Zanzubar kimya kimya na wakaamua kulizika Azimio la Arusha....

Siku zote huwa nasoma vitabu viwili, Biblia na Azimio la Arusha; nimesoma mara nyingi kitabu cha Azimio la Arusha, sijaona kipengele chochote ambacho kina kasoro...
 
Wakubwa wameenda Zanzubar kimya kimya na wakaamua kulizika Azimio la Arusha....

Siku zote huwa nasoma vitabu viwili, Biblia na Azimio la Arusha; nimesoma mara nyingi kitabu cha Azimio la Arusha, sijaona kipengele chochote ambacho kina kasoro...

Kweli angeweza kujiunga chadema kwa sababu ya hiyo biblia uliyoitaja hapo!
 
Nimesoma katiba za vyama mbali mbali vya upinzani, sijaona chama makini zaidi ya Chadema ambacho ndiyo pekee nakiona kina dalili ya kuwakomboa wanyonge wa nchi hii.....

Maneno hayo aliyatamka Mwalimu Nyerere, mwaka 1995, baada ya uchaguzi mkuu, jambo linaloonyesha Mwalimu alikuwa akipewa maono na Mungu ya yale yatakayokuja baadaye hapa TZ

Na alipewa maono pia ya kutengeneza katiba hii inayoyutesa. Pia alipewa maono ya kumnyonga mkulima mwamindi
 
Hivi hiki kipindi kipo??

Sent from my Nokia Lumia using Tapatalk
 
Nimesoma katiba za vyama mbali mbali vya upinzani, sijaona chama makini zaidi ya Chadema ambacho ndiyo pekee nakiona kina dalili ya kuwakomboa wanyonge wa nchi hii.....

Maneno hayo aliyatamka Mwalimu Nyerere, mwaka 1995, baada ya uchaguzi mkuu, jambo linaloonyesha Mwalimu alikuwa akipewa maono na Mungu ya yale yatakayokuja baadaye hapa TZ

Mnamsifia mwalimu wakati kichaa wenu ameshamtukana?
 
ccm siyo mama yangu, ikiacha misingi yake ya kutetea wananchi wanyonge, naweza kuachna nayo.......

Naamini kama mwalimu nyerere angekuwa hai leo angeachana na ccm na kujiunga na cdm kutokana na ccm kuacha misingi yake ya kuwatetea wanyonge na kuwakumbatia mafisadi, hadi kufikia rais wa nchi akadiriki kutoa msamaha kwa majizi yaliyokwapua mabilioni ya epa kwa kuwaambia warejeshe tu hayo mabilioni waliyoiba ili soo iishe!!!

tungeendelea kushonea nguo viraaka mpaka leo
 
♥unawexa wewe ukawa mwaminifu kabisa lakini haitoshi inabidi uwe na uwezo wa kuwaambia rafiki na ndugu zako ikulu ni mahali patakatifu mimi sikuchaguliwa kuja kupageuza pango la wala rushwa

♥Ikulu kuna biashara gani pale? ikulu ni mzigo mie nimekaa pale miaka 20 na mi5 ukiona mtu anakimbilia ikulu muogope kama ukoma.

♥serikali corrupt haikusanyi kodi itabaki kukimbizana na wafanya biashara ndogondogo na kukumbatia wenye mali.

Yaani ni hatari maana viongozi waliopo madarakani wengine hawajui wayatendayo kama Mizengo Pinda anadiriki kusema wapigwe tu ni jambo jambo la kushangaza na kisikitisha kwa kiongozi kama yeye kutoa kauli kama ile. Laiti angekuwa hai Nyerere sidhani kama walioko madarakani kwa sasa kama wangefanya madudu wayatendayo kwa sasa.
 
Hivi hiki kipindi kipo??

Sent from my Nokia Lumia using Tapatalk

Kipo TBC tu lakini wamechagua hotuba chache ambazo zinaipendelea ccm ndo wanazirudiarudia hizohizo kila siku. Hizo hotuba zilizonukuliwa na wadau hapo juu zimefichwa ukithubutu kukutwa nazo utaambiwa umemtukana Baba wataifa na watamwagiza kinana na nape wazunguke nchi mzima kwa kodi zetu kulaani nukuu za Baba wataifa.
 
"Hakuna dhambi kubwa kama dhambi ya ubaguzi, ukishasema sisi na wao"


Sent from my iPhone using JamiiForums mobile app
 
Kipo TBC tu lakini wamechagua hotuba chache ambazo zinaipendelea ccm ndo wanazirudiarudia hizohizo kila siku. Hizo hotuba zilizonukuliwa na wadau hapo juu zimefichwa ukithubutu kukutwa nazo utaambiwa umemtukana Baba wataifa na watamwagiza kinana na nape wazunguke nchi mzima kwa kodi zetu kulaani nukuu za Baba wataifa.

Sijawahi kuiangalia TBC toka inaitwa TVT
 
Back
Top Bottom