Wizi wafanyao polisi kituoni, wapi kwa kulalamika?

Wizi wafanyao polisi kituoni, wapi kwa kulalamika?

mchekanapori

Member
Joined
Aug 3, 2012
Posts
50
Reaction score
51
Habari wana jamvi, naomba ushauri wenu. Ndugu yangu alikuwa anakwenda benki ku deposit mamilioni kadhaa kutokana na biashara zake, alitumia usafiri wa pikipiki yake mwenyewe akiendesha, kufika eneo la benki akakutana na gari ya polisi wakamkamata na kumpeleka polisi, wakamvua kila kitu na wakachukue zile pesa na hata hawakuziandika pale kuwa amekuja na pesa kiasi gani, wakambambikia kesi ya kuandamana, kapigwa faini tena laki 3, alipouliza pesa zangu zipo wapi? Polisi wamemkatalia kuwa hajakuja na pesa kituoni, jamani hii nchi yetu inaelekea wapi, naomba msaada wenu tafadhalini.
 
Habari wana jamvi, naomba ushauri wenu. Ndugu yangu alikuwa anakwenda benki ku deposit mamilioni kadhaa kutokana na biashara zake, alitumia usafiri wa pikipiki yake mwenyewe akiendesha, kufika eneo la benki akakutana na gari ya polisi wakamkamata na kumpeleka polisi, wakamvua kila kitu na wakachukue zile pesa na hata hawakuziandika pale kuwa amekuja na pesa kiasi gani, wakambambikia kesi ya kuandamana, kapigwa faini tena laki 3, alipouliza pesa zangu zipo wapi? Polisi wamemkatalia kuwa hajakuja na pesa kituoni, jamani hii nchi yetu inaelekea wapi, naomba msaada wenu tafadhalini.

Pole! Utapata haki yako simamia kweli tu.Muone mkuu wa kituo.
 
Je alilipa faini? Kama alilipa pesa za kulipa alipata wapi wakati unasema ameporwa na polisi pesa zote? Je maandamano yana faini polisi? Kumbuka hilo ni kosa la jinai na hukumu hutolewa mahakamani tu iwe fain au jela. Maandamano ya bodaboda kama yalitokea ni yale yaliokwenda kwa chadema sasa mbona hakuna benki pale cdm tuseme alikuwa amekwenda kuweka pesa? Mbona siku ya maandamano Ya bodaboda hawakukamatwa na polisi?.mtoa mada tujulishe wanajamii intelligence ukweli halisi ili tukusaidie mawazo muafaka.
 
Nenda central arusha uone jitu linaitwa gwakisa lilivo jizi la,kutupwaaaa..linaiba mpaka shilingi mia mia ...
 
kituo gani, lini, saa ngapi na eneo gani alikamatwa naomba majibu mtoa post usaidiwe
 
...peaples power a.k.a chadema kiboko yao hao jamaa..
 
Mkuu ili isionekane kwamba wewe ni mpiga majungu taja kituo,alafu haiwezekani mtu ukawekwa lock up bila kuandikisha vitu vyako.na ukamatwe siku hiyo hiyo na court mda huohuo??
 
Habari wana jamvi, naomba ushauri wenu. Ndugu yangu alikuwa anakwenda benki ku deposit mamilioni kadhaa kutokana na biashara zake, alitumia usafiri wa pikipiki yake mwenyewe akiendesha, kufika eneo la benki akakutana na gari ya polisi wakamkamata na kumpeleka polisi, wakamvua kila kitu na wakachukue zile pesa na hata hawakuziandika pale kuwa amekuja na pesa kiasi gani, wakambambikia kesi ya kuandamana, kapigwa faini tena laki 3, alipouliza pesa zangu zipo wapi? Polisi wamemkatalia kuwa hajakuja na pesa kituoni, jamani hii nchi yetu inaelekea wapi, naomba msaada wenu tafadhalini.

Hii hadithi inaacha maswali mengi kuliko majibu....anaingia benki wakamkamata...kwa kosa gani?kisha proo kituoni?eh..kwa taratibu za kwetu unawapa taarifa nimekuja kuweka mzigo km mna shida na mm ngoja nihifadhi alafu twendeni...tena sema kwa sauti watu wengine wasikie hakuna atakae kukukatalia.Hii ilinikuta Police Mabatini k'nyama siku moja na hawakugusa hata thumni ingawa nilikuwa na mzigo wa kutosha na nilishinda selo mpk 8 usiku.kwa hiyo tupe taarifa kamili isije kuwa jamaa yako mkwapuaji(naogopa kusema Jay Mbazi) na polisi walikuwa wanamfuatilia,intejilisia ikamkamata hapo!
 
usiongee pumba wewe, ukajiona unajua kuongea sana, nani amekwambia amewekwa lockup na kupelekwa court siku hiyohiyo na muda huohuo, hujui kusoma wewe? hujui? Au huelewi ukisoma.
 
Habari wana jamvi, naomba ushauri wenu. Ndugu yangu alikuwa anakwenda benki ku deposit mamilioni kadhaa kutokana na biashara zake, alitumia usafiri wa pikipiki yake mwenyewe akiendesha, kufika eneo la benki akakutana na gari ya polisi wakamkamata na kumpeleka polisi, wakamvua kila kitu na wakachukue zile pesa na hata hawakuziandika pale kuwa amekuja na pesa kiasi gani, wakambambikia kesi ya kuandamana, kapigwa faini tena laki 3, alipouliza pesa zangu zipo wapi? Polisi wamemkatalia kuwa hajakuja na pesa kituoni, jamani hii nchi yetu inaelekea wapi, naomba msaada wenu tafadhalini.

ww ni muongo sana. hii ilikua lini na wapi ?
 
Ndugu Ejay, na wengine wastaarabu pale, hii habari imetokea ktk mji wa Mtwara, siku ya tarehe 2 J.tano, alikamatwa maeneo ya benki ya Pride alikuwa anaelekea hapo, na baadhi ya wafanyakazi wa pale pride wanaijua hii habari, kapelekwa kituo cha Polisi kikubwa pale Mtwara, akajumuishwa na waliokuwa wakiandamana wenye bodaboda, siku ya tatu yake walipelekwa mahakamani, mzee wake alimlipia faini laki tatu, walikwenda kulalamika kwa mkuu wa kituo, kawaambia hawezi kumsaidia, na baadae kaenda hadi kwa mkuu wa wilaya kuomba kusaidiwa, lakini waliomkuta pale ni msaidizi wake na kawajibu ni vigumu kuwasaidia, dogo ni mtaratibu sana na kiumri ni mdogo, alitii amri kwa kujua pesa yake itasalimika, ila kwa wale askari walitumia hiiyo nafasi ya kumfanyia dhuluma kwa kuwa hakutaka kubishana nao.
 
Ni jinsi gani unavyoukwepa ukweli. Post yako haioneshi kama ulifika mahakamani pia inavyojulikana kuwa unapopelekwa mahakamani polisi huwa wanakukabidhi vitu vyako vyote. Je kwanin akadaie mahakamani badalala ya kudai pesa yake kituoni?. Sema ukweli jamii intelligence ikusaidie kama kweli yametokea.
 
Back
Top Bottom