Wizi wa mitandaoni: Wamekwama kuniibia

OMOYOGWANE

JF-Expert Member
Joined
Dec 30, 2016
Posts
5,139
Reaction score
12,882
Habari wakuu,

Kuna wizi wa kimtandao unafanywa na watu wenye nia ya kutapeli watu.

Leo nimepigiwa simu na mtu mwenye namba hizo hapo juu, bahati nzuri sikuwa namsikia vizuri nikamwambia atume ujumbe wa maneno (sms),

Nilipo usoma huo ujumbe , machale yakanicheza, nikastuka kuwa anataka kuniibia .

Wakuu kuweni makini.
 
Watakuwa wanakujua hao,angalia wasije wakakuteka
 
Aisee pole sana mkuu, wenye TAMAA hapo lazima wangepigwa tu
 
Ebu elekeza vizuri huo wizi mkuu
Mkuu iko hivi,
Leo kuna mtu alinitumia pesa kutoka kwenye akaunti yake ya NMB, na huyo mtu namjua vizuri hana dhiki wala ujanja wa mitandaoni,
Baada ya nusu saa. Ndio hilo tukio likatokea ,
Maswali niliyojiuliza

Je namba yangu wametoa wapi?
Wamejuaje kama nina pesa kwenye akaunti yangu ya M PESA?

Hapa kunauwezekano nimedukuliwa au aliyenitumia pesa mawasiliano yake pamoja na akaunti yake zimedukuliwa,

Nahitaji Maoni yenu wakuu tafadhari
 
Me mwenyewe CRDB card yangu imedukuliwa afu ndio naitegemea kwenye boom


Nimeandika statement kwenye tawi lao la chuo ifungiwe mpaka watakapo rekebisha wenyewe.
 
Hawa watu n wafanyakazi wa hz kampuni za cm ambao co waaminifu huwa wanaangalia kwenye akaunti wanatuma message kwa wengi kubahatisha ukiwa na tamaa unaliwa
 
Ht m nlipigiw wakanambia nimeshinda simu smartphone na lak 1, alaf baat m sikuw maskin wa kutupwa kipind hiko nkapotezea,ilkuw mwez w 3
 
Fuata hayo maelekezo utaona hatua ya mwisho unaambiwa thibitisha kutuma kiasi cha sh..... Kwende kwa ....... Ukiwa na haraka unatuma, ila ukisoma ule ujumbe unagundua fasta kuwa unatuma pesa bila kujua.
 
eti Vodacom power nafanya sasa hiv watu wanevurugwa kabsa Mkuu aliye kutumia kwa NMB ndiyo mmoja wao hiyo inatokea sana hapo walitaka warudishe hela yao na wakuoige yako mbona ipo wazi mkuu
 
Reactions: BAK
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…