Wizi wa magari Dar es salaaam, Polisi wanahusika!

Wizi wa magari Dar es salaaam, Polisi wanahusika!

keybroked

Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
28
Reaction score
15
Kumekuwa na ongezeko kubwa sana la wizi wa magari hapa jijini na ukifuatilia kwa umakini kanda ya polisi Kinondoni ndiyo inayoongoza. Magari ambayo yamekuwa yakiibiwa kwa wingi ni aina ya Hiace, Coaster na Canter hasa hizi tani tatu zinazobinua. Wezi wa magari haya wamekuwa selective sana wa maeneo katika kufanya vitendo hivi wakijua hata ukienda kuripoti issue yako haiwezi kuwaathiri. Vituo vikuu vya polisi ambavyo vinahusika kwa namna moja ama nyingine ni kituo cha polisi cha Kawe na kituo cha polisi Magomeni, ukiibiwa gari yako na ukaripoti katika vituo hivi hesabu umeliwa. Wapelelezi wa vituo hivyo watakutoa hata milioni kadhaa za fedha wakidai wanawapa informer wao na kufuatilia mawasiliano ya wezi kutoka kampuni za simu lakini mwisho wa siku utaishia kukata tamaa pale unapoujua ukweli kwamba upelelezi haujafanyika na hata hayo mawasiliano ya simu hayajafanyika.
Kinachotokea ni kwamba polisi wa vituo hivi na hata wale wa kitengo cha wizi wa magari "Central Police" wanawajua kabisa wezi wa magari lakini watakukatisha tamaa katika upelelezi hadi utaamua kuacha ufuatiliaji. Kwa wale ambao ni wabishi katika kufuatilia na at least wana undugu na Polisi wa vyeo vya juu gari zao hupatikana mara baada ya kuuzwa kwa mtu (mara nyingi ni baada ya miezi 3 hadi 6) na si kutoka kwa wezi wa magari. Na ukiona gari limepatikana kwa muda mfupi basi ujue ni la mtu maarufu na anayejulikana serikalini.
Hata kama kwa bahati njema ukafanikiwa kumpata mshukiwa wa wizi wa gari yako, kwa kuwa wapo karibu sana na Polisi hasa wapelelezi wa kesi za magari watawekwa rumande kwa muda kukuridhisha na baada ya muda wataachiwa. Wakati mwingine hawawakamati kabisa hasa wale wanaohusika moja kwa moja, ni ngumu sana kupata haki yako Polisi endapo hujuani na bosi yeyote katika sekta hiyo. Ukitaka kujua usumbufu wa Polisi pata tatizo linalohitaji msaada wao!
 
Noma polisi mwizi,mlinzi mwizi,ikulu kuna wezi sasa tumwamini nani?
 
Yaani jamani polisi wetu viazi. kuna mmoja huku Nsala inn karibu na Mbezi kwa Yusufu aliagiza konyagi nzima. baada ya kulewa akasahau simu wajanja wakasepa nayo. kesho yake akaja na wenzake kumkamata akaunta kwamba amemwibiavcimu. cha ajabu polisi mmoja wa kike sijui bibi yake aliishikia bango hiyo kesi akataka ifikishwe mahakamani bila hata kwenda kuona eneo la tukio yaani kwenye bar. bahati nzuri akaunta alitumia uzuri wake kwa wakuu fulani pale kituoni kesi ikafutwa. hatuna polisi tuna mi fisi tu.
 
Pale Kawe ni hatari, mimi mwenyewe nimepambana sana pale kwa kesi ya wizi mwaka jana.Wapelelezi wote na wakubwa zao lao ni moja.Ukimpeleka mtuhumiwa umewapa deal na mwisho hakuna wanachofanya na upelelezi mbuzi hata kwenye tukio hawafiki zaidi ya kuandika tu maelezo yenu.

IGP aingilie kati kama kweli wanataka wananchi tuamini kweli Polisi wameamua kubadilika.Nawashauri kama una kesi ya wizi usiripoti Kituo cha Polisi Kawe itakula kwako.Kuna mama alifanikiwa kupata gari lake ndani ya siku tatu tu baada ya kesi kuhamishiwa Central na hapo ni baada ya kuzungushwa sana na wapelelezi wa Kawe.

Pale Polisi Kawe pameoza IGP chukua hatua au fanya uchunguzi wa siri kwa kesi zote za wizi pale ujue kwanini malalamiko yamekuwa mengi.
 
Yaani jamani polisi wetu viazi. kuna mmoja huku Nsala inn karibu na Mbezi kwa Yusufu aliagiza konyagi nzima. baada ya kulewa akasahau simu wajanja wakasepa nayo. kesho yake akaja na wenzake kumkamata akaunta kwamba amemwibiavcimu. cha ajabu polisi mmoja wa kike sijui bibi yake aliishikia bango hiyo kesi akataka ifikishwe mahakamani bila hata kwenda kuona eneo la tukio yaani kwenye bar. bahati nzuri akaunta alitumia uzuri wake kwa wakuu fulani pale kituoni kesi ikafutwa. hatuna polisi tuna mi fisi tu.
Akaunta LOL
 
Hahaa duuu siyakucheka kwa kweli hapo wakikuuibia ni kuwatoa sadaka naenda kwetu simbawanga na mvimbisha mtu tumbo alafu hata wakija kuniomba msamaha mm nasema hata sijui kwani mliiba nyie
 
Back
Top Bottom