Wizi wa magari aina ya Noah washamiri Dar

Wizi wa magari aina ya Noah washamiri Dar

SERGIO

JF-Expert Member
Joined
Dec 13, 2012
Posts
348
Reaction score
145
Kumekuwepo na wimbi la wizi wa magari aina ya Noah ulioibuka hivi karibuni jijini Dar es Salaam. Magari mawili yaliibiwa usiku wa kuamkia Jumamosi iliyopita kutoka eneo la maegesho katika nyumba ya mzee mmoja maarufu mitaa ya Kimara B Temboni. Taarifa zinasema walinzi wa Kimasai wanaolinda eneo hilo pia wametoweka na haijulikani waliko. Gari moja ni la mwenye nyumba na lingine ni la jirani yake aliyekuwa anaegesha hapo kwa malipo. Taarifa zilizopatikana jana zinasema magari mengine kadhaa aina ya Noah yameibiwa siku tatu zilizopita kutoka kwenye eneo la maegesho maeneo ya Kimara. Kuna dili gani inayohusisha magari haya?
 
Sasa mwendo ni kununua magari yasiyo common ila Noah,Alteza na wenzake utalia tu
 
Hili ni tatizo la kununua magari common!!1 Kwa sasa Noah zimeshika kasi sana!! Jaribu kupita taratibu ukiwa kwenye daladala au gari yako unone ni Noah ngapi zinakupita!!! Family car hizo kwa hiyo ni rahisi sana kuibiwa na kubadilishwa mara moja. Poleni kwa walioibiwa.
 
Noah ndio daladala za routes za mipakani, namanga, sirari etc, kwaiyo ni dili sana na wamasai wana zimaind sana. hawa walinzi wa kimasai wengi wamekuja Dar kutafuta mitaji so ni wachraji dili wabaya sana. mi nashangaa kwanini bado watu wana waamini.
 
Noah ndio daladala za routes za mipakani, namanga, sirari etc, kwaiyo ni dili sana na wamasai wana zimaind sana. hawa walinzi wa kimasai wengi wamekuja Dar kutafuta mitaji so ni wachraji dili wabaya sana. mi nashangaa kwanini bado watu wana waamini.

hao walinzi wanahusika kwa sana tu kwanini wakimbie kama ulivyosema hizo gari ni dili huko mipakani nliona makala moja ikizungumzia namna wenye gari aina ya noah wanavyochota hela huko sirari....
 
Back
Top Bottom