Wizi Tengeru jijini Arusha



Mkuu sio Tengeru ya sasa unayoongelea. Tengeru inahistoria hiyo na sio ilivyo kwa sasa. Kiujumla ongezeko la watu kuja limebadi sana tabia za wameru. Wameru ni kabila ambalo sio maarufu sana kwa watanzania ambao hawajafika Arusha.

Watu wengi wamewafahamu wameru baada ya kufika Arusha. Ni watu wenye asili ya ukorofi, ubabe, wakabila (hawapendi sana watu kuja) ila mazingira yamewabadili kwa lazima.

Wenyewe wanaonaga fahari kusifiwa wababe na wakorofi lakini mbali na hayo hawana sifa chanya nyingi zaidi ya kujifia kutoa mkuu wa majeshi (Sarakikya) na kutuma muwakilishi wao wenyewe kudai uhuru wa wameru kwa malkia Uingereza enzi za ukoloni.

Wameru wa sasa jeuri yao inaishia mto nduruma kama unaenda mjini na Usa kama unaelekea Moshi. Hiyo ndio teritory yao ya kujidai.

Nakuaga bar moja inaitwa Sumni hapa Tengeru. Vijana ni wapole kabisa siku hizi hawana matata. Uhalifu ni wa kawaida tu kama wa maeneo mengine sio ule wa zamani uliokuwa distinguished kwa Tengeru pekee.
 
Habari? Kwanza nikuambie pole kwa aliyekupa historia ya Siku za nyuma si sasa, Tengeru ni sehemu salama kama ilivyo sehemu nyingine. Wengi walisema usiku hapakuwa salama ila sasa hata ukifika kituo cha basi usiku utakuwa salama. Vijana wa bodaboda wamechangia sana kuleta utulivu na hawapo tayari kuona biashara yao ikiharibiwa.
Pamoja na maelezo yote hayo haina maana usiwe makini utembeapo sehemu yoyote na hii haina maana usifunge mlango kwa kuwajaribu. Jukumu la kwanza la ulinzi wa Mali zako ni wewe mwenyewe.
Ikumbukwe siku za masoko kila mahali huwa si salama sana kwani hata watu wa kutoka sehemu nyingine wenye tabia ya wizi hufika sokoni kutafuta mtu aliyezubaa wamwibie.
 
Kama ni mgeni karibu arusha. Hayo maeneo mika nenda rudi ndio yako hivyo. and shida sio viongozi.. bali ni jamii inayoishi hapo... vijana wao ni shidah..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…