Wizi mtandao wa Vodacom

binafsi katika mitandao ya simu ya Tanzania ninapenda vodacom, labda ni sababu sijawahi kumbwa na hayo matatizo ya wenzangu.
Ukitaka weka salio disable internet ukishajiunga na bundle enable internet maana ukiweka salio bila ku disable internet kuna apps kama whatsapp, push email n.k zinazotumia internet muda wote utakuta zimekula ela kidogo kwa ajili ya internet.
Mpesa kwangu ndiyo huduma bora compared na tigo pesa na airtel money maana nishafanya blunder mara kibao ya kukosea kutuma ela uwa nikiwapgia haraka wanapokea na wanarudisha ela yangu within 24hrs tofauti na tigo ambao kwanza kupokea hawapokei na wakipokea wanauliza kama uko kwa wakala ukijibu hapana basi ndio usahau hiyo ela hupati ng'o utapigwa dana dana mpaka ukate tamaa kila siku waambiwa utatumiwa na hutumiwi.
Internet ya vodacom iko safi kwa maeneo mengi na pia kile kifurushi chao cha buku cha internet bila kikomo ukijiunga wala internet gbs hata 8.
Jiepushe kukubari kujiunga na huduma usizozijua mimi sijiungi na huduma yoyote nisiyo ijua na uwa sijiungi na promosheni za kijinga jinga.
 
Msafara wa kenge hawakosi mijusi,Mwizi anajulikana kwa kauli zake

Haikosi huyu Senti hamsini ndio kati ya wale wenye suruali zinazotaka kuanguka ukifika kwenye ofisi za Vodacom? Maana wale jamaaa hua hawajali wateja, sijui huona km ss ni choka mbaya?
 

mkuu si kuna uzi special wa vodacom? kwanini hupeleki malalamiko yako huko?
 
Sijutii kuwa mteja wa kampuni yoyote ya simu Tanzania,HASAHASA VODACOM
Hayo matatizo munayapata kwa kutokuwa makini.
Mods futa hizi pumba muende ofisini kwao si mnapajua, mumetuchosha Arrghh
ww ndio Kenge maji kweli kweli
kwani usipochangia utaonekana ----? au kujishaua kwa genye zako

Vodaco kiasi cha chini kabisa cha bundle wamekipunguza hadi 40MB
na km ukiwakopa 900 ndio wanakupa 100MB kwa 899 na haichukui hata saa moja kweny simu ndogo ya kawaida
UPUUZI mwingine unaeza kukuta muda wa hewani umeumaliza kwa kuongea WANAFYEKA NA BUNDLE ZAO ili ukope
kuanzia sasa hawataniona kwenye Internet
 
Ni kweli voda wanaelekea pabaya. Unaweza kununua umeme kupitia LUKU saa 12.00 jioni pesa inakatwa na usipate majibu hadi kesho yake. Wenzao airtel kama huduma ya LUKU haiko vizuri hapo hapo unatumiwa ujumbe na pesa yako kurudishwa kwenye akaunti yako.
 
Mim huwa siweki hela voda,nikupokea tu,mara ya mwisho nimeweka mwezi june mpaka leo,tena niliweka jiti tatu...
 
Hivi ukihama Voda uhamie mtandao gani labda?
Maana majanga ya Tigo ni Tsunami
 

Juzi kuna habari ililetwa hapa jamvini kuwa voda imeamliwa na mahakama iilipe kampuni zaidi ya 1 Bilioni. Malipo hayo ni kutokana na voda kuvunja mkataba na hiyo kampuni. Hukumu hiyo ilikuwa ni kukazia hukumu ya awali, baada ya voda kusuasua kulipa huo mkwanja.
 
Tatizo kaka voda wana kata hela hata kama una tumia simu ya touch. Na ukuwauliza hawana majibu ya kulizisha sasa hapo kwa nn watu wasilalamike.
 
Sijutii kuwa mteja wa kampuni yoyote ya simu Tanzania,HASAHASA VODACOM

Hayo matatizo munayapata kwa kutokuwa makini.

Mods futa hizi pumba muende ofisini kwao si mnapajua, mumetuchosha Arrghh


Haikosi we senti hamsini ndio kati ya wale wenye suruali zinazotaka kuanguka ukifika kwenye ofisi za Vodacom? Maana wale jamaaa hua hawajali wateja, sijui huona km ss ni choka mbaya? Kenge kabisa.
 
Kwa taarifa ni kua wanakata pesa hadi kwa wanaotumia simu za tochi hawafai tuwahame haraka sana na nashukuru binafsi nimehamisha watumiaji 30 mpaka sasa

Ndg mm nilikatwa na kisimu changu cha tochi,yaan haya ni majizi sn.
 

TCRA si rafiki wa mlaji, nimewahi kupeleka malalamiko kadhaa kuhusu kampuni za simu CHA KUSHANGAZA sijajibiwa hata moja!
 
Vodacom mnachelewa kurudisha majibu ya LUKU.

Kuna siku mnapata Kichaa mnakataa kuunga CHEKA ya 499 wakati kwenye simu Nina 500 mnasema salio halitoshi.

Mimi hizo mbili kwangu ni KERO SANA.
 
Andika sms uitawanye kwa watumiaji wa voda, uwaambie waisambaze kwa watumiaji wote wanaowafahamu, namna wanavyoibiwa ili wapate sababu za kuhama.

Ni kweli vodacom wezi wezi wezi sana. Na isitoshe, hawana customer care nzuri. Wanatukana wateja kama hawawahitaji kabisa.

Wale watu wa customer serivices vikiona vimechemsha, mteja anaomba kuunganishwa na boss wao ambaye ni supervisor. Supervisors wale kazi yao ni ku back makosa ya wachini yao. wanatukana zaidi na kuhakikisha haki inapotea na hata ukiomba number ya mkuu wao, hawakupi. Wanaisha kukuambia, ishia kule. Hili nililishuhudia kwa mpwa wangu alikuwa akiwasiliana nao nami nikiwa nasikia.

Voda ni wezi kama ccm.

Kwa taarifa ni kua wanakata pesa hadi kwa wanaotumia simu za tochi hawafai tuwahame haraka sana na nashukuru binafsi nimehamisha watumiaji 30 mpaka sasa
 
Sijutii kuwa mteja wa kampuni yoyote ya simu Tanzania,HASAHASA VODACOM

Hayo matatizo munayapata kwa kutokuwa makini.

Mods futa hizi pumba muende ofisini kwao si mnapajua, mumetuchosha Arrghh

Yaani kwasababu wewe unaweza kuvumilia, hupatwi na tatizo wengine wasiseme?! Vodacom wenyewe wanakubali sasa cha ajabu nini hapo!
 
Exactly! Km unatumia smartphone yoyote hakikisha kabla hujaweka salio ume-SWITCH OFF MOBILE DATA. Ukiacha ON lazima ukatwe tu as internet charges.


Kweli kabisa mkuu hata huko wanakohamasishana kwenda kama hawatalifanyia kazi hili then huko nako watahama tu.
 

Ushamba wa kutumia smart phone uwe unazima Data connection kwanza ndo uweke salio
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…