EMT
Platinum Member
- Jan 13, 2010
- 14,483
- 15,308
Imebainika kuwa chanzo cha miradi mingi ya barabara nchini kukwama kumalizika kwa kipindi kilichopangwa inatokana na madeni inayodaiwa Wizara ya Ujenzi, Sh. bilioni 331 kutoka kwa makandarasi hadi Februari, 2012.
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, John Cheyo, alisema mwisho wa mwaka 2009-2010 Wizara ya Ujenzi ilikuwa na madeni ya Sh. bilioni 44 na hadi kufikia Juni 30,2011 madeni yaliongezeka mpaka Sh. bilioni 420. Aliongeza kuwa kufikia Februari 30, 2012 Wizara ya Ujenzi ilipokea Sh. bilioni bilioni 384 kutoka Hazina ambayo ni pungufu ya madeni inayodaiwa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Herbert Mrango, alisema wizara hiyo haipati fedha katika muda mwafaka kutoka Serikalini, ila wamehaidiwa kupewa Sh. bilioni 317 na Serikali kulipa madeni hayo.
Akitaja miradi ambayo imesitishwa kuendelea kutokana na wakandarasi kuidai Wizara ya Ujenzi, Cheyo ni barabara kutoka Bariadi kwenda Lamadi, Ndundu kwenda Somanga yenye urefu wa kilomita 60, iliyogharimu Sh. bilioni 58.8 na Wizara imeshalipa Sh. bilioni 46 na kudaiwa Sh. bilioni 12.
Nipashe
Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali, John Cheyo, alisema mwisho wa mwaka 2009-2010 Wizara ya Ujenzi ilikuwa na madeni ya Sh. bilioni 44 na hadi kufikia Juni 30,2011 madeni yaliongezeka mpaka Sh. bilioni 420. Aliongeza kuwa kufikia Februari 30, 2012 Wizara ya Ujenzi ilipokea Sh. bilioni bilioni 384 kutoka Hazina ambayo ni pungufu ya madeni inayodaiwa.
Katibu Mkuu wa Wizara ya Ujenzi, Herbert Mrango, alisema wizara hiyo haipati fedha katika muda mwafaka kutoka Serikalini, ila wamehaidiwa kupewa Sh. bilioni 317 na Serikali kulipa madeni hayo.
Akitaja miradi ambayo imesitishwa kuendelea kutokana na wakandarasi kuidai Wizara ya Ujenzi, Cheyo ni barabara kutoka Bariadi kwenda Lamadi, Ndundu kwenda Somanga yenye urefu wa kilomita 60, iliyogharimu Sh. bilioni 58.8 na Wizara imeshalipa Sh. bilioni 46 na kudaiwa Sh. bilioni 12.
Nipashe