Influenza
JF-Expert Member
- Jul 1, 2018
- 1,445
- 3,403
Waziri Mkuu Mhe.Kassim Majaliwa ametoa muda wa miezi miwili na majuma mawili kwa Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo iwe imekamilisha mchakato wa Tanzania kuwa na vazi la Taifa.
Amesema Watanzania hawajaunganishwa kwa kuwa na vazi la taifa, ambalo mchakato wake umeendeshwa kwa miaka mingi na wizara hiyo bila ya kujulikana ulipofikia.
Ametoa agizo hilo katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha wakati akifunga tamasha lililojulikana kama Urithi Festival.
Amesema ifikapo Desemba 30, 2018 Watanzania waanze kupata sura ya vazi la taifa ili wadau walijadili na waamue vazi gani la Mtanzania litakalowakilisha taifa kama nchi nyingine walivyomudu kuwa na vazi la taifa.
Amesema ili kufikia azma hiyo, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo iandae tamasha maalumu kwa ajili ya kuonesha aina tofauti za nguo ili kupata vazi la Taifa.
Aidha, amewaagiza waandaaji wa tamasha la Uridhi Festival wahakikishe kuanzia mwakani kuwe na uratibu wa pamoja baina ya Tanzania Zanzibar na Tanzania Bara ili tamasha lifunguliwe upande mmoja na kufungwa upande mwingine wa Muungano.
Amesema kwa kufanya hivyo watakuwa wametoa fursa kwa walio Zanzibar kujifunza na kuona utamaduni wa bara na wa bara kujifunza ya Zanzibar, hivyo itasaidia kudumisha umoja wa kitaifa.
Amesema Watanzania hawajaunganishwa kwa kuwa na vazi la taifa, ambalo mchakato wake umeendeshwa kwa miaka mingi na wizara hiyo bila ya kujulikana ulipofikia.
Ametoa agizo hilo katika uwanja wa Sheikh Amri Abeid jijini Arusha wakati akifunga tamasha lililojulikana kama Urithi Festival.
Amesema ifikapo Desemba 30, 2018 Watanzania waanze kupata sura ya vazi la taifa ili wadau walijadili na waamue vazi gani la Mtanzania litakalowakilisha taifa kama nchi nyingine walivyomudu kuwa na vazi la taifa.
Amesema ili kufikia azma hiyo, Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo iandae tamasha maalumu kwa ajili ya kuonesha aina tofauti za nguo ili kupata vazi la Taifa.
Aidha, amewaagiza waandaaji wa tamasha la Uridhi Festival wahakikishe kuanzia mwakani kuwe na uratibu wa pamoja baina ya Tanzania Zanzibar na Tanzania Bara ili tamasha lifunguliwe upande mmoja na kufungwa upande mwingine wa Muungano.
Amesema kwa kufanya hivyo watakuwa wametoa fursa kwa walio Zanzibar kujifunza na kuona utamaduni wa bara na wa bara kujifunza ya Zanzibar, hivyo itasaidia kudumisha umoja wa kitaifa.