yusufummaka
Member
- Apr 7, 2012
- 30
- 20
Kumeibuka biashara jijini DSM ya kila kona ya jiji kuwashwa moto na kukaanga chips mitaani. Wauza chips na mishikaki hawa hawafahamiki nani kawawapa kibali bila ya kufahamu kama afya zao na mazingira ya biashara vinakidhi haja ya kuwauzia wenzao vyakula. Biashara hii inawatia wananchi kwenye hatari ya kuambukizwa magonjwa kama: typhoid, cholera, minyoo, na kuhara damu. Pia, iko hatari ya mioto hii ya holela barabarani kuunguza waendao kwa miguu kandokando mwa barabara pamoja na kuunguza nyumba zilizo karibu na majiko hayo. Hivi wizara ya afya inasubiri mabaya yawapate wananchi ndiyo ichukuwe hatua?