Pfizer
JF-Expert Member
- Mar 25, 2021
- 762
- 1,007
Wizara ya Mawasiliano na Teknolojia ya Habari nchini, imesema ili kukabiliana na kasi ya matumizi ya akili unde nchini, imekamilisha mkakati wa matumizi ya akili unde ikiwa ni katika kuelekea kuwa na miongozo kanuni na sheria zitakazo linda matumizi salama ya akili unde.
Akizungumza katika Jukwaa la Akili Unde la Tanzania ( Tanzania Artificial Intelligence Forum 2025), kaimu Mkurugenzi msaidizi kutoka Wizara ya mawasiliano na teknolojia ya Habari Mhandisi Bahati Zuberi, amesema mkakati huo utakuwa na masuala mbalimbali ikiwemo miongozo ya kupata watalaamu watakao simamia akili unde pamoja na masuala mengine ya uwezeshaji matumizi na kulinda haki miliki zitazo tokana na kazi zinazotengenezwa kupitia akili unde
Kwa upande wake Mkurugenzi wa tume ya TEHAMA Nchini Dokta Nkuwe Moses Masaga amesema, kutokana na maendeleo hayo ya matumizi ya akili unde ni wazi Tanzania ni lazima ijipange kutumia fursa pamoja na kukabiliana na changamoto zitakazo kuwepo kama vile kuweka sheria na kanuni ambazo hazitapotosha ama kuleta taharuki kwa jamii
Naye Mmoja wa watoa mada katika jukwaa hilo Jaji wa Mahakama kuu ya tanzania Dokta Adam Mambi amesema, Mahakama ikiwa ni mmoja wa taasisi zilizo nufaika na akili unde, inajivunia mafanikio iliyo yapata ikiwemo akili unde kusaidia kupunguza mlundikano wa mashauri huku akisisitiza kuongezwa kwa elimu ili kukuza uelewa wa jamii juu ya matumizi sahihi ya akili unde
Katika Jukwaa hilo kwa mara ya kwanza pia Tanzania imeendesha mashindano ya vijana Watalaamu wa kubuni na kutumia akili unde ili kutatua changanoto kwenye jamii
Katika Jukwaa hilo kwa mara ya kwanza pia Tanzania imeendesha mashindano ya vijana Watalaamu wa kubuni na kutumia akili unde ili kutatua changanoto kwenye jamii