WITO: Watanzania turudi vijijini

WITO: Watanzania turudi vijijini

Rose Mayemba

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2012
Posts
721
Reaction score
1,017
Napenda kuchukua fursa hii kutoa wito kwa watanzania wenzangu popote pale mlipo na haswa mijini, kuhakikisha ya kwamba tunarudi katika vijiji tulivyotoka kila tunapoweza. Sisi tulioko mijini na ambao tumeshuhudia moja kwa moja udhalimu wa Serikali hii ya CCM, tuna wajibu kwa ndugu zetu kufanya safari za kwenda huko vijijini ilimradi kuwatoa ndugu zetu kwenye giza totoro la kifikra ambalo chama tawala kiliweka, kinaweka na kitazidi kuweka miongoni mwa wananchi wengi hasa wa vijini. Ni wajibu wetu sisi ambao tumeweza kung'amua wizi huu unaofanywa na wachache wenye nafasi dhidi ya walipa kodi wengi ambao ndio walala hoi, kupinga na kuwasaidia hawa ndugu zetu wengine kupinga hali hii. Baada ya kuangalia clip ya video ambayo ilimuonyesha Nape akihutubia wananchi wa Makambako (wengi akina mama) na kushuhudia uongo unao enezwa na hawa jamaa kwa makusudi kabisa ilimradi kuwachanganya watu, nimeona nitoe wito huu. Ndugu zangu CCM ya sasa haina hata chembe ya uchungu kwa ajili ya wananchi wake zaidi ya kuendeleza propaganda zinazolenga kuisaidia kubaki madarakani. Kila kinachofanywa na serikali hii kinafanywa 'statergicaly' kuiwezesha CCM kubaki madarakani at the expense of the majority na sana sana kuhakikisha kwa makusudi kuwa raia wa kawaida haelimiki ipasavyo ilimradi waendelee kubaki gizani. Tukatae wizi huu. UFIKE MUDA SASA KILA MMOJA KWA NAFASI YAKE ASEME BAAAAS! YATOSHA! ENOUGH IS ENOUGH & TO HELL WITH CCM.

It begins with you
Comrade
Rose Mayemba
 
Napenda kuchukua fursa hii kutoa wito kwa watanzania wenzangu popote pale mlipo na haswa mijini, kuhakikisha ya kwamba tunarudi katika vijiji tulivyotoka kila tunapoweza. Sisi tulioko mijini na ambao tumeshuhudia moja kwa moja udhalimu wa Serikali hii ya CCM, tuna wajibu kwa ndugu zetu kufanya safari za kwenda huko vijijini ilimradi kuwatoa ndugu zetu kwenye giza totoro la kifikra ambalo chama tawala kiliweka, kilinaweka na kinazidi kuweka miongoni mwa wananchi wengi hasa wa vijini. Ni wajibu wetu sisi ambao tumeweza kung'amua wizi huu unaofanywa na wachache wenye nafasi dhidi ya walipa kodi wengi ambao ndio walala hoi, kupinga na kuwasaidia hawa ndugu zetu wengine kupinga hali hii. Baada ya kuangalia clip ya video ambayo ilimuonyesha Nape akihutubia wananchi wa Makambako (wengi akina mama) na kushuhudia uongo unao enezwa na hawa jamaa kwa makusudi kabisa ilimradi kuwachanganya watu, nimeona nitoe wito huu. Ndugu zangu CCM ya sasa haina hata chembe ya uchungu kwa ajili ya wananchi wake zaidi ya kuendeleza propaganda zinazolenga kuisaidia kubaki madarakani. Kila kinachofanywa na serikali hii kinafanywa 'statergicaly' kuiwezesha CCM kubaki madarakani at the expense of the majority na sana sana kuhakikisha kwa makusudi kuwa raia wa kawaida haelimiki ipasavyo ilimradi waendelee kubaki gizani. Tukatae wizi huu. UFIKE MUDA SASA KILA MMOJA KWA NAFASI YAKE ASEME BAAAAS! YATOSHA! ENOUGH IS ENOUGH & TO HELL WITH CCM.

It begins with you
Comrade
Rose Mayemba
Asante kwa ushauri, naomba unitumie nauli kwenye mpesa 075461285512.
 
Ni wazo zuri lakini utapingwa na wafuasi wa magamba kwa nguvu zote!!!
 
Rose usiwe na wasiwasi tumeisha anza kazi hiyo! tumechoka sana na propaganda za magamba wakati hali ya maisha inazidi kuwa duni.
 
Kuna watakaokwambia "Nirudi kijinini mjini nimwachie nani?"
 
Ndugu yangu hilo ni wazo jema. Hoja yako ina mantiki sana!!! La msingi ni wananchi kuiondoa CCM madarakani na kisha serikali mpya kubadidili mfumo mzima wa kiutawala!!! Tofauti na hapo watanzania tutakuwa tunajitumainisha kwa kubahatisha mambo mithili ya watu wanaopiga ramli..
 
Asante kwa ushauri, naomba unitumie nauli kwenye mpesa 075461285512.

Hiyo namba uliyoandika umekosea au ndio Teknolojia imekuwa, Naona tarakimu zimezidi zile TBS.

Hata hivyo njoo usaidie kuwaerevua waliolala, Tumia hata zile ulizotaka kumfadhili yule rafiki yako unaesemaga analeta fujo na maneno ya porojo kuja UK kufuta aibu zake.
Pamoja tutalijenga Taifa letu
 
Mtu kazi yake fundi friji. Kijijini kwao hakuna umeme. Arudi akafanye shughuli gani?
 
Mjini shule huko kijijini shule itatoka wapi?
 
Napenda kuchukua fursa hii kutoa wito kwa watanzania wenzangu popote pale mlipo na haswa mijini, kuhakikisha ya kwamba tunarudi katika vijiji tulivyotoka kila tunapoweza. Sisi tulioko mijini na ambao tumeshuhudia moja kwa moja udhalimu wa Serikali hii ya CCM, tuna wajibu kwa ndugu zetu kufanya safari za kwenda huko vijijini ilimradi kuwatoa ndugu zetu kwenye giza totoro la kifikra ambalo chama tawala kiliweka, kinaweka na kitazidi kuweka miongoni mwa wananchi wengi hasa wa vijini. Ni wajibu wetu sisi ambao tumeweza kung'amua wizi huu unaofanywa na wachache wenye nafasi dhidi ya walipa kodi wengi ambao ndio walala hoi, kupinga na kuwasaidia hawa ndugu zetu wengine kupinga hali hii. Baada ya kuangalia clip ya video ambayo ilimuonyesha Nape akihutubia wananchi wa Makambako (wengi akina mama) na kushuhudia uongo unao enezwa na hawa jamaa kwa makusudi kabisa ilimradi kuwachanganya watu, nimeona nitoe wito huu. Ndugu zangu CCM ya sasa haina hata chembe ya uchungu kwa ajili ya wananchi wake zaidi ya kuendeleza propaganda zinazolenga kuisaidia kubaki madarakani. Kila kinachofanywa na serikali hii kinafanywa 'statergicaly' kuiwezesha CCM kubaki madarakani at the expense of the majority na sana sana kuhakikisha kwa makusudi kuwa raia wa kawaida haelimiki ipasavyo ilimradi waendelee kubaki gizani. Tukatae wizi huu. UFIKE MUDA SASA KILA MMOJA KWA NAFASI YAKE ASEME BAAAAS! YATOSHA! ENOUGH IS ENOUGH & TO HELL WITH CCM.

It begins with you
Comrade
Rose Mayemba

Elimu ni kwa wote si mjin wala vijijini,hata mjini kuna baadhi ya watu bado hawajui haki zao.
 
mtaji wa CCM ndiyo huo; wananchi wanadanganywa mchana kweupe pee!! Nilicheka wakati jamaa eti anasema Msigwa kasomba watu mtaani kuwapeleka waandamane -- lah jamaa ni noma kwa urongo!!
 
Kurudi kijijini siwezi kama Bomba la gesi bado linaelekezwa Mjini!
 
Napenda kuchukua fursa hii kutoa wito kwa watanzania wenzangu popote pale mlipo na haswa mijini, kuhakikisha ya kwamba tunarudi katika vijiji tulivyotoka kila tunapoweza. Sisi tulioko mijini na ambao tumeshuhudia moja kwa moja udhalimu wa Serikali hii ya CCM, tuna wajibu kwa ndugu zetu kufanya safari za kwenda huko vijijini ilimradi kuwatoa ndugu zetu kwenye giza totoro la kifikra ambalo chama tawala kiliweka, kinaweka na kitazidi kuweka miongoni mwa wananchi wengi hasa wa vijini. Ni wajibu wetu sisi ambao tumeweza kung'amua wizi huu unaofanywa na wachache wenye nafasi dhidi ya walipa kodi wengi ambao ndio walala hoi, kupinga na kuwasaidia hawa ndugu zetu wengine kupinga hali hii. Baada ya kuangalia clip ya video ambayo ilimuonyesha Nape akihutubia wananchi wa Makambako (wengi akina mama) na kushuhudia uongo unao enezwa na hawa jamaa kwa makusudi kabisa ilimradi kuwachanganya watu, nimeona nitoe wito huu. Ndugu zangu CCM ya sasa haina hata chembe ya uchungu kwa ajili ya wananchi wake zaidi ya kuendeleza propaganda zinazolenga kuisaidia kubaki madarakani. Kila kinachofanywa na serikali hii kinafanywa 'statergicaly' kuiwezesha CCM kubaki madarakani at the expense of the majority na sana sana kuhakikisha kwa makusudi kuwa raia wa kawaida haelimiki ipasavyo ilimradi waendelee kubaki gizani. Tukatae wizi huu. UFIKE MUDA SASA KILA MMOJA KWA NAFASI YAKE ASEME BAAAAS! YATOSHA! ENOUGH IS ENOUGH & TO HELL WITH CCM.

It begins with you
Comrade
Rose Mayemba

Haki ya Mungu kama kuna mtu kijijini kwetu atashabikia CCM kunako 2015 basi huyo ni gendaheka, maana kule nimewalisha ndugu zangu pamoja na wakazi wa pale habari kamili jinsi hii nchi inavyoharibiwa na CCM. Nikawapa mifano iliyo hai ya kuwa toka tumepata uhuru sasa ni miaka 50, CCM imefanya nini pale kijijini na si pale tu bali nchi nzima. Watu walifunguka macho na kunibeba, wazee wa pale nyumbani waliniomba nigombee udiwani au hata ubunge na wakanihakikishia kunibeba kwa gharama zozote zile. Wakanitemea mate kichwani kunibariki na kunitakasa dhidi ya laana za CCM, hivyo hapa nipo ngangari kusubiri uchaguzi kunako 2015 na safu yangu ya mawaziri tayari nimeshaipanga, huku waziri wangu wa afya akitokea hapa hapa JF.
 
Uko sahihi Rose, ccm wametumia rasilimali za watanzania kujinufaisha wao kwa miaka 50 bila kuboresha maisha ya wananchi wao.

Mimi napendekeza richa ya sisi wenyewe kwenda vijijini kuwahamasisha wananchi, upinzani watumie makundi ambayo yana migogoro na serikali ya ccm yaliyopo vijijini kuipinga ccm watafanikiwa zaidi. Kwa mfano, kundi la walimu ni rahisi kuwahamasisha wanafunzi wapeleke ujumbe majumbani mwao wa kuikataa ccm 2015.

Walimu ni wengi na wanaheshimika sana vijijini hivyo ni rahisi kukubalika pia ukizingatia wana migogoro na serikali ya ccm ni rahisi kushawishika.

Mimi sio mwanasiasa na sifungamani na upande wowote, lakini ubabe unaotumiwa na ccm kuwakandamiza wanachi wake umefikia wakati tuupinge na tuseme basi inatosha!

Wameshindwa hata kuboresha masilahi ya kundi dogo la watumishi wa serikali yake ambapo vyanzo vya mapato ya kufanya hivyo vipo.

Ngoja nikomee hapa nisije nikaharibu!
 
Back
Top Bottom