Ruhazwe JR
JF-Expert Member
- Jan 31, 2011
- 3,403
- 920
UTANGULIZI
Nawasalimu wanajamvi wote na wapa poleni ya majukumu ya kusaka mkate wa kila siku.
Leo nimeona ni vema kutoa wito kwa wananchi wote kuhusiana na Bajeti ya serikali ya Mwaka 2012/2013.Wito wangu unakuja katika kipindi ambacho Bunge la Jamuhuri wa Muungano lipo bize katika kupitisha bajeti,Bajeti ambayo kwangu haina matumaini ya kukabiliana na hali ngumu ya maisha ya wananchi walionayo kwa sasa.Ninaposema hali ngumu ya maisha ni kwa wale wote ambao si mafisadi.
WITO
Wito wangu ni kwamba wananchi wote hasa wa majimboni tuungane kwa pamoja bila kujali itikadi za Vyama vyetu,Kuungana pamoja katika kujua ni mbunge gani akiwa Bungeni(Bunge linalo endelea kwa sasa)amethubutu kuchangia kwa namna yoyote ile kupita kwa bajeti hii ambaye haitakua na tija kwa wananchi.baaada ya kuw Tumewwjua tuungane pamoja kuwangoja kwenye majimbo yetu tuandamane kuwafata kuwataka kwamba ni Kwanini wasiwajibika kwa kujiudhuru nafasi zao za Ubunge kwa kuwa wameshibdwa kuwajibika kwetu wananchi kwa kupitisha Bajeti ambayo ni Takataka kwetu wananchi na ni dili kwa wajanja wachache,ambao ndio wanatufikisha katika maisha magumu ya sasa.
Nasema hivi kwakua wabunge wanachangia kupitisha madudu ambayo hayana maslah kwa sisi wananchi isipokuwa yana maslah kwa vyama vyao wanavyotoke na yana maslah kwa serikali legele ambayo ni dhaifu kwa kila lolote linalotoke.
Sitaki kamini kuwa Wabunge wetu hawajui nini wananchi tunataka,Sitaki kuaminin kuwa wabunge wetu hawajui hali ngumu ya maisha tuliyonayo wananchi.Ikumbukwe kuwa Mwanachi ndio bosi wa Mbunge,Mbunge bosi wake si serikali,wala chama anachotoke,Mbunge bosi wake ni yule ambaye amempeleka bungeni hivyo anapaswa kujua nini mwananchi anataka na ndicho anapaswa kupitisha Bungeni.
Serikali imetia pamba mskioni hataki kusikia kilio cha watanzania walio wengi,Serikali imevaa miwani ya Mbao haitaki kuona mateso na taabu tuliyo nayo wananchi wake,kufanya hivyo nathubutu kusema serikali inakiuka katiba kwa kuto kuja na Bajeti ambyo si bajeti yenye mwendelezo wa bajeti iliyopita ya 2011/2012 pamoja na maadhimio yaliyopitishwa na Bubge kuusu mikakati ya maendeleo ambayo labda ingeweza kubadilisha maisha haya magumu kwa Watanzania.Kwa mujibu wa katiba Ibara ya nane,mwananchi ndiye mwenye mamlaka dhidi ya serikali.
Naomba sana wananchi wote tuungane kuwafata wabunge wetu ambao kwa namna moja au nyingie watakua wamethubutu kusema "Naunga mkono Bajeti",lazima wabunge hawa wawajibike.
HITIMISHO
Najua kuna watu watakuja na hoja za vyama,Hoja yangu ni Bajeti mbovu kwa mwanachi na uwajibikaji wa wabunge katika kuipitisha Bajeti.Kumbuka Dunia ni yako,Tanzania ni yako,chagua kudai haki bila woga kwkua Haki haiombwi bali hudaiwa.
Nawasilisha
Ruhazwe JR
jimmyjrtz@yahoo.com
Nawasalimu wanajamvi wote na wapa poleni ya majukumu ya kusaka mkate wa kila siku.
Leo nimeona ni vema kutoa wito kwa wananchi wote kuhusiana na Bajeti ya serikali ya Mwaka 2012/2013.Wito wangu unakuja katika kipindi ambacho Bunge la Jamuhuri wa Muungano lipo bize katika kupitisha bajeti,Bajeti ambayo kwangu haina matumaini ya kukabiliana na hali ngumu ya maisha ya wananchi walionayo kwa sasa.Ninaposema hali ngumu ya maisha ni kwa wale wote ambao si mafisadi.
WITO
Wito wangu ni kwamba wananchi wote hasa wa majimboni tuungane kwa pamoja bila kujali itikadi za Vyama vyetu,Kuungana pamoja katika kujua ni mbunge gani akiwa Bungeni(Bunge linalo endelea kwa sasa)amethubutu kuchangia kwa namna yoyote ile kupita kwa bajeti hii ambaye haitakua na tija kwa wananchi.baaada ya kuw Tumewwjua tuungane pamoja kuwangoja kwenye majimbo yetu tuandamane kuwafata kuwataka kwamba ni Kwanini wasiwajibika kwa kujiudhuru nafasi zao za Ubunge kwa kuwa wameshibdwa kuwajibika kwetu wananchi kwa kupitisha Bajeti ambayo ni Takataka kwetu wananchi na ni dili kwa wajanja wachache,ambao ndio wanatufikisha katika maisha magumu ya sasa.
Nasema hivi kwakua wabunge wanachangia kupitisha madudu ambayo hayana maslah kwa sisi wananchi isipokuwa yana maslah kwa vyama vyao wanavyotoke na yana maslah kwa serikali legele ambayo ni dhaifu kwa kila lolote linalotoke.
Sitaki kamini kuwa Wabunge wetu hawajui nini wananchi tunataka,Sitaki kuaminin kuwa wabunge wetu hawajui hali ngumu ya maisha tuliyonayo wananchi.Ikumbukwe kuwa Mwanachi ndio bosi wa Mbunge,Mbunge bosi wake si serikali,wala chama anachotoke,Mbunge bosi wake ni yule ambaye amempeleka bungeni hivyo anapaswa kujua nini mwananchi anataka na ndicho anapaswa kupitisha Bungeni.
Serikali imetia pamba mskioni hataki kusikia kilio cha watanzania walio wengi,Serikali imevaa miwani ya Mbao haitaki kuona mateso na taabu tuliyo nayo wananchi wake,kufanya hivyo nathubutu kusema serikali inakiuka katiba kwa kuto kuja na Bajeti ambyo si bajeti yenye mwendelezo wa bajeti iliyopita ya 2011/2012 pamoja na maadhimio yaliyopitishwa na Bubge kuusu mikakati ya maendeleo ambayo labda ingeweza kubadilisha maisha haya magumu kwa Watanzania.Kwa mujibu wa katiba Ibara ya nane,mwananchi ndiye mwenye mamlaka dhidi ya serikali.
Naomba sana wananchi wote tuungane kuwafata wabunge wetu ambao kwa namna moja au nyingie watakua wamethubutu kusema "Naunga mkono Bajeti",lazima wabunge hawa wawajibike.
HITIMISHO
Najua kuna watu watakuja na hoja za vyama,Hoja yangu ni Bajeti mbovu kwa mwanachi na uwajibikaji wa wabunge katika kuipitisha Bajeti.Kumbuka Dunia ni yako,Tanzania ni yako,chagua kudai haki bila woga kwkua Haki haiombwi bali hudaiwa.
Nawasilisha
Ruhazwe JR
jimmyjrtz@yahoo.com