Wilaya nzima (Bukoba Vijijini) Hakuna CHADEMA!

Wilaya nzima (Bukoba Vijijini) Hakuna CHADEMA!

Mkuu mimi sikuungi mkono katika wito wako wa kutaka viongozi wa CHADEMA waende sehemu kama huko Bukoba vijijini wakaanzishe mkakati wa mabadiliko, wakati wenyeji wenyewe kama huyu mleta mada ameshindwa kuanzisha lolote zaidi ya kuja humu na kulalamika tu.

Mabadiliko ya kweli hayawezi kuletwa na Viongozi wa kitaifa bali wananchi wenyewe waliochoka na utawala wa CCM.

Huyo anaongelea juu ya kufungua matawi. Usimlazimishe mtu atoe hela zake ili kuanzisha tawi. Kwanza unajuaje kama anazo hizo hela?
 
Pamoja na maneno mazuri ya faraja kuwa Tanzania karibia inakombolewa...bado napata mashaka na mbinu za Ukombozi tulizonazo. Huwezi Kuamini kinachoendelea katika baadhi ya Wilaya nchini.....ambapo yaani hata harufu ya CDM kuisikia ni kwa machale.

Nilibahatika kuingia katika kikao cha Madiwani Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba (Rural) yenye kata 29 nilisikitika kuona kuwa kati ya hizo kata 29, kata 28 zinaongozwa na CCM na kata moja tu ya Katoro inaongozwa na CUF. Yaani hapa upinzani umeoneshwa na CUF pekee japokuwa bado na yenyewe haitoshi.

Wakati kikao kianendelea Viongozi wa Vyama vya upinzani walikuwa wanakribishwa kuhudhuria kikao hicho. Waliokaribishwa ni Viongozi wa CCM na CUF kwa siku ya kwanza. Siku ya Pili alihudhuria wa CCM na NCCR Mageuzi na CUF. Ikabidi niulize; imekuwaje NCCR Mageuzi wamefika hapa wakati hawana hata Kata moja? Jibu nililopewa ni kuwa "angalau NCCR wanaonekana as chama cha Upinzani, hata kama hawana kata hata moja wao ni "ACTIVE" maeneo haya. Baada ya hapo nikajiuliza inakuwa je Chama kinachopigiwa chapuo kuchukua nchi hakina jitihada yoyote ili kijihakikishie ushindi?

Nimewahi kusema hapa kuwa CDM hapa Bukoba mjini haionekani.......hatuoni initiative zozote za kukipromote chama. Viongozi wa Mkoa wako wapi? Niliwahi kusema Chama kama chama kiitishe mkutano wa wanachama wake kioneshe mpango kazi wake kama tatizo ni la ki budget wanachama wenyewe tujipange na kukiwezesha kuwafikia wananchi lakini wapi. Ofisi au Makao makuu naambiwa ni Ijuganyondo.....pembeni mwa mji. Hata kutoonekana kwa ofisi mjini ni udhaifu........

Tatizo nini? Inawezekana kuna wilaya Nyingine CDM haina hata kata moja!! Naomba tena Uongozi wa CDM ueleze kinaga ubaga nini mpango wake wa Kukiimarisha chama Mkoani Kagera .,....Hususan Wilaya Hii ya Bukoba? Siwezi kuwasemea wengine hapa nchini. Naomba anayeona kulegalega kwa CDM mahali pake aombe ufafanuzi kwa viongozi ili watoe majibu ya pamoja. Nisipojibiwa kwa hili siongei tena.

Nasuburi maelezo hapa........tumejiuliza wengi ...tunasubiri majibu na makakati.

Nimekusoma. Ila Mimi mwenyekiti wangu wa Kijiji, Irogelo, Kata ya Kamachumu, wilaya ya Muleba ni wa Chadema
 
Siyo bukoba tu,tembelea maeneo kama Tabora vijijini,maeneo ya mkoa wa Tanga,pwani na rukwa CDM haifahamiki kabisa. Sioni mabadiliko yakija siku za karibuni,
Acha uzushi wewe.
Unapayukapayuka tu hapa
Where is Tabora vijijini?
 
Mzito Kabwela,

Vipi Wilaya za Missenyi, Muleba, Ngara, Karagwe, Ngara, huko nako Chadema hakuna kabisa, vipi kuhusu udini.
 
Last edited by a moderator:
Mkuu mimi sikuungi mkono katika wito wako wa kutaka viongozi wa CHADEMA waende sehemu kama huko Bukoba vijijini wakaanzishe mkakati wa mabadiliko, wakati wenyeji wenyewe kama huyu mleta mada ameshindwa kuanzisha lolote zaidi ya kuja humu na kulalamika tu.

Mabadiliko ya kweli hayawezi kuletwa na Viongozi wa kitaifa bali wananchi wenyewe waliochoka na utawala wa CCM.

Tatizo lako wewe ni moja. Unadhani sisi tunaomba Uongozi wa juu uje uishi Bukoba. Kama Umesoma Politics utakuwa unajua mambo ya Charisma, au kama umesoma philosophy utakuwa unajua nini maana ya mandate na ni wapi unaweza kufanya reference mtu akauelewa. Mimi hata iweje lazima asimame anayekubalika kwanza ili sisi tuendeleze moto. Usikatae kwa hilo. Wakati uongozi ukiwa nyololo si kwamba watu wa kule ni wajinga sana. Inabidi anayekubalika aanzishe kisha wengine tuendeleze mapambano hayo. Si kila shehe ana uwezo wa kutoa majini au mchungaji kutoa mapepo.

Basi sema wewe bajeti yako kiasi gani tukuchangie uje ufungue tuone mapokezi utakayopokea. Wenyewe wanaelewa. Hata kama nikiendelea lazima niwe na ratiba Uongozi utafika lini.

Kila timu ina mchezaji tegemeo japokuwa hawezi kucheza peke yake. Hata wengine ni Muhimu lakini huwezi kubeza mchango wa mchezaji tegemeo.
 
Taarifa ninazopata ni kwamba cdm watakuwa na operesheni mwezi january 2013 katika mkoa wa Kagera. Labda hiyo itasaidia
 
Taarifa ninazopata ni kwamba cdm watakuwa na operesheni mwezi january 2013 katika mkoa wa Kagera. Labda hiyo itasaidia

Ok twambie unazopata kutoka wapi ili tuanze publicity na maandalizi ya kutosha. Na inabidi itangazwe ili kila mwananchi atarajie muda wa kujua Ukweli. Hata kaka hujuma inafanyika watanzania wawe wanaelewa kuwa kinachojaribu kuzuiwa ni kipi? Sio watu tunaenda kimya kimya tukipata madahara inakuwa haieleweki nini lilikuwa lengo letu.
 
Siasa si hisabati kwamba unapokokotoa formula vizuri unahakika na jibu, kuna ambao wamelaumu CDM kwa kutokuwa na wawakilishi lakini ukweli ni kwamba nchi inaongozwa na mfumo wa vyama vingi ambavyo vipo zaidi ya kumi na kila chama kinajitahidi kuangalia uwezekano wa kuchukua majimbo/kata na ndio maana unakuta kuna sehemu CUF amechukua na CDM haipo which means CUF wamecheza karata nzuri ya kukitambulisha chama chao.Pia lazima ujua kwamba vyama vinafanya kazi na wananchi ambao kila mmoja ana utashi wake hivyo tusiwalaumu CDM sana kama wadau wengine walivyochangia wakati Ta Muganyizi amekuja na hoja ya kuwepo na way forward.

My take: Nadhani mkakati wa kwanza kwa CDM ni viongozi wa mkoa wa Kagera kwa ujumla bila support kutoka CDM taifa wafanye kampeni ya kuongeza idadi ya wanachama wapya katika wilaya husika maana kwa uzoefu wangu Bukoba kwa muda mrefu imekuwa ngome ya CUF kama chama cha upinzani maarufu hivyo imepelekea hata wilaya jirani ya Bukoba rural nayo kuwa ngome ya CUF. (Hapa Ta muganyizi atanirekebisha maana mie nilipita mitaa hiyo miaka ya 2000 - 2004 ambapo ukizungumzia upinzani unazungumzia CUF sijui siku hizi).

Mkakati wa pili ni CDM makao makuu kuangalia namna ya kusaidia viongozi wa CDM wa wilaya kifedha na kiufundi ili waweze kuwa na uwezo wa kuwafikia wananchi kwa kutumia raslimali chache zilizopo.

Mwisho, viongozi wa kitaifa kupita kama timu kupiga uhamasishaji wa nguvu na kuhubiri sera zao kwa uwazi ili waweze kufahamika kwanza kwa wananchi si unajua kama chama chenye nguvu ni CCM alafu kinachofuatia kwa umaarufu ni CUF hivyo ajenda hapa ni kupata mabalozi wazuri katika ngazi za vijiji na vitongojini (wanachama na wafuasi) ambao watasaidia kupeleka vuguvugu la siasa kwa wananchi kabla ya kuwaza ushindi katika ngazi ya kata.

Ukishakuwa na wachama na wafuasi wa kutosha inakuwa rahisi kwa chama kutambulisha vuguvugu la mabadiliko kwa wananchi kikubwa kwenye mikutano kusiwe na agenda ya siasa ya maji taka hasa kwa chama cha upinzani kilichopo eneo husika.
 
Last edited by a moderator:
Siasa si hisabati kwamba unapokokotoa formula vizuri unahakika na jibu, kuna ambao wamelaumu CDM kwa kutokuwa na wawakilishi lakini ukweli ni kwamba nchi inaongozwa na mfumo wa vyama vingi ambavyo vipo zaidi ya kumi na kila chama kinajitahidi kuangalia uwezekano wa kuchukua majimbo/kata na ndio maana unakuta kuna sehemu CUF amechukua na CDM haipo which means CUF wamecheza karata nzuri ya kukitambulisha chama chao.Pia lazima ujua kwamba vyama vinafanya kazi na wananchi ambao kila mmoja ana utashi wake hivyo tusiwalaumu CDM sana kama wadau wengine walivyochangia wakati Ta Muganyizi amekuja na hoja ya kuwepo na way forward.

My take: Nadhani mkakati wa kwanza kwa CDM ni viongozi wa mkoa wa Kagera kwa ujumla bila support kutoka CDM taifa wafanye kampeni ya kuongeza idadi ya wanachama wapya katika wilaya husika maana kwa uzoefu wangu Bukoba kwa muda mrefu imekuwa ngome ya CUF kama chama cha upinzani maarufu hivyo imepelekea hata wilaya jirani ya Bukoba rural nayo kuwa ngome ya CUF. (Hapa Ta muganyizi atanirekebisha maana mie nilipita mitaa hiyo miaka ya 2000 - 2004 ambapo ukizungumzia upinzani unazungumzia CUF sijui siku hizi).

Mkakati wa pili ni CDM makao makuu kuangalia namna ya kusaidia viongozi wa CDM wa wilaya kifedha na kiufundi ili waweze kuwa na uwezo wa kuwafikia wananchi kwa kutumia raslimali chache zilizopo.

Mwisho, viongozi wa kitaifa kupita kama timu kupiga uhamasishaji wa nguvu na kuhubiri sera zao kwa uwazi ili waweze kufahamika kwanza kwa wananchi si unajua kama chama chenye nguvu ni CCM alafu kinachofuatia kwa umaarufu ni CUF hivyo ajenda hapa ni kupata mabalozi wazuri katika ngazi za vijiji na vitongojini (wanachama na wafuasi) ambao watasaidia kupeleka vuguvugu la siasa kwa wananchi kabla ya kuwaza ushindi katika ngazi ya kata.

Ukishakuwa na wachama na wafuasi wa kutosha inakuwa rahisi kwa chama kutambulisha vuguvugu la mabadiliko kwa wananchi kikubwa kwenye mikutano kusiwe na agenda ya siasa ya maji taka hasa kwa chama cha upinzani kilichopo eneo husika.

Mungu akubariki sana
 
Huyo anaongelea juu ya kufungua matawi. Usimlazimishe mtu atoe hela zake ili kuanzisha tawi. Kwanza unajuaje kama anazo hizo hela?
*Mkuu naona hata wewe bado huijui CHADEMA vizuri.
Sidhani kama umeshawahi kufanya harakati zozote za CHADEMA katika ground field.

*Huwezi kufungua tawi bila kuwa na wanachama wa kutosha kwanza, na ufunguzi wa tawi hautaji ulazima wa kiongozi wa ngazi ya juu ya kitaifa.

*Kifupi huyu jamaa anataka mabadiliko lakini wakati huohuo hataki kuingia gharama za kufanya any Initiative bali viongozi wa kitaifa waende kumfanyia!!!!

*Nani alisema CHADEMA inahitaji pesa yake kwanza?
Kwa CHADEMA kitu cha msingi ni Dhamira njema, Nguvu na Akili yako kwanza kwa kuwa It is a risk task.
 
*Mkuu naona hata wewe bado huijui CHADEMA vizuri.
Sidhani kama umeshawahi kufanya harakati zozote za CHADEMA katika ground field.

*Huwezi kufungua tawi bila kuwa na wanachama wa kutosha kwanza, na ufunguzi wa tawi hautaji ulazima wa kiongozi wa ngazi ya juu ya kitaifa.

*Kifupi huyu jamaa anataka mabadiliko lakini wakati huohuo hataki kuingia gharama za kufanya any Initiative bali viongozi wa kitaifa waende kumfanyia!!!!

*Nani alisema CHADEMA inahitaji pesa yake kwanza?
Kwa CHADEMA kitu cha msingi ni Dhamira njema, Nguvu na Akili yako kwanza kwa kuwa It is a risk task.

Soma thread yangu vizuri........hivi ni kitu gani kinafanikiwa pasipo plan. Na ninapouliza mpango kazi na kurequest budget unaelewa nini? Mbona unakuwa REACTIVE badala ya kuwa PROACTIVE.
 
Mzito Kabwela,

Vipi Wilaya za Missenyi, Muleba, Ngara, Karagwe, Ngara, huko nako Chadema hakuna kabisa, vipi kuhusu udini.
Mkuu huko Chadema ipo lakini haina nguvu sana. Ni kama vile Tukuyu, lakini watu wanaisubiri M4C kwa hamu sana. Nimepita kote huko. Kwa Bukoba mjini mazingira ni yale yale ya udini kuchanganya na siasa.Ni kama vile Mtwara ilivyo kwa Chadema. Hilo la udini hata Chadema na CUF wenyewe wanajua kuwa linawatafuna sana. Uzuri wake kwa wadini wa CUF ni kuwa wao wana alternative nyingine, CCM.
 
Soma thread yangu vizuri........hivi ni kitu gani kinafanikiwa pasipo plan. Na ninapouliza mpango kazi na kurequest budget unaelewa nini? Mbona unakuwa REACTIVE badala ya kwa PROACTIVE.
Mkuu i am sorry if i am looked irritative to you.

Lakini ningependa nikupe mfano mdogo halisi kuhusu harakati za CHADEMA namna zinavyoweza kufanyika na kuzaa matunda ya kudumu kisiasa.

*Mwaka 2005 nikiwa Dar, mimi pamoja na vijana wachache tuliokuwa mtaa mmoja tuliamua kwa dhati kabisa kumshinikiza John Mnyika agombee ubunge jimbo la Ubungo baada ya kusikia yuko CHADEMA na kuna tetesi hizo za yeye
kutaka kugombea. Wengi walidhani anataka kugombea udiwani!!

Huyu jamaa alikuwa Streetmate wangu, na hakuwa mtu anaefahamika mtaani kisiasa mbali ya kielimu na kijamii. Kwa wengi ulikuwa ni mzaha kwani ushindani wa kisiasa ubungo ulikuwa kwa CCM, CUF, TLP na NCCR ambao walikuwa tayari wana mizizi na wagombea tena maarufu kipesa, kielimu, uzoefu. Ilifikia baadhi ya watu kudai kuwa Mnyika hakustahili kugombea hata udiwani!!
Sikumbuki kama CHADEMA walikuwa na tawi pale.

Jambo pekee tulilomwakikishia Mnyika ni kuwa sisi washikaji zake tutakuwa tunaelimisha, tunashangilia, mawakala, kupiga kura na tulifanya hivyo!!!
Hatukuwa wanaCHADEMA, hatukuwahi kufanya siasa na hatukuwa na pesa bali tulikuwa na DHAMIRA NJEMA, NGUVU na AKILI za kutaka mageuzi.
Uchaguzi ulifanyika na CHADEMA ilishindwa!!!

Kifupi mwaka 2005 CCM kwa mkoa wa DAR ilishinda majimbo yote na kata zote.
Lakini harakati hizo zimekuja kuzaa matunda 2010.

*Take that as vivid example naamini utanielewa.
 
Ta Muganyizi. Natambua uchungu ulionao kutokana na kusuasua kwa harakati za ukombozi huko Bukoba Vijijini. Nilikuwa Bkb wiki tatu zilizopita,nilijitahidi kufanya mazungumzo na watu mbalimbali,lakini ilionyesha hawana hamasa yoyote. Matatizo ya Kagera na hasa hizi wilaya zinazokaliwa na wahaya wengi ni watu kujiona wajuaji sana wakati hawana lolote. Pili,sisi wahaya siyo watu wa kupenda kujiingiza ktk changamoto ambazo mwisho wa siku jamii yetu itafaidika. Tuwa-binafsi sana. Na kwasababu hii tumeshindwa ktk mambo mengi.
 
sijui mnazungumzia wanachama au madiwani au wapenzi! ikumbikwe kura hata wanazopata ccm kwa haki hazitokani na wanachama wao bali wapenzi au wale wanaokubaliana na sera au wagombea wao. kama ndiyo hivyo hata kama huko buhaya hakuna diwani hata mmoja na mwanachama hata mmoja kama inavyotaka kudanganya. kwa hakikika wapenzi wa sera za cdm watakuwrpo na huo ndo mtaji kuliko wanachama mfu wa ccm wanaoraruana
 
CDM ni nani?Kwa nini hakuna nguvu BKB vijijini?Mjini IPO?Suala hili si rahisi.Wale watu wa kijijini wanastahili ukombozi na wakati ndiyo huu.Wa mjini wanahitaji seriousness na wakati ni huu
Mheshimiwa Slaaa,ZZK Freeman,Sugu Sillinde,Salakana,Lwakatare,ninyi ni viongozi.Kiongozi anapaswa aende pasipo na njia atengeneze njia halafu wasioona waione waipite tusonge mbele.Onesheni njia muda si rafiki yetu,2015 si keshokutwa tu?Msigombanie fito nani awe Rais,gombanieni ukombozi wa Watanzania wengi iwezekanavyo kutoka utumwa wa MISRI/CCM!
Usiongelee hta BKB je ILALA,TEMEKE,MOSHI VIJIJINI?KWA Wapare?
Pana kazi nzito,lakini mimi ninatiwa moyo na filosofi hii:safari ya maili elfu moja huanza na hatua moja!
 
Back
Top Bottom