Wifi anachukua nafasi yangu,nifanyaje?

Fidel80

JF-Expert Member
May 3, 2008
21,947
4,445
"Nimegundua kuwa watu wanafanikiwa kuokoa mahusiano na ndoa zao kupitia blogu hii na mimi leo nimeona nichangie tatizo langu ili kupata ushauri wa watu wengine na zaidi kutoka kwako kaka Fidel.

Mimi ni mdada mtu mzima tu nimeolewa miaka si chini ya mitano, nina watoto wawili. Nimekuwa nikishindana na wifi yangu ambae ni dada wa damu wa mume wangu, ushindani wetu ni kama mtu na mke mwenzie lakini si hivyo.

Kabla sijaolewa na huyu mwanaume tulikuwa kwenye uhusiano wa mbali kwani mimi nilikuwa nasoma Ireland na yeye alikuwa Tanzania. Kipindi chote hicho hakukuwa na matatizo yeyote kati yangu na dada yake.


Baada ya kumaliza masomo nilihamia England kufanya kazi ambako ndiko tunaishi mpaka sasa. Ndoa yetu ilifungiwa Tanzania na Mume wangu akanifuata huku na baada ya muda tukasaidiana na kumleta dada yake ambaye ndio wifi yangu huyu mwenye vituko kila kukicha ambavyo vinahatarisha ndoa yangu.


Imefikia hatua wifi yangu kuchagua nini kifanyike ndani ya nyumba yangu, aina gani ya vifaa vinunuliwe ikiwa tunafanya marekebisho hapa ndani, wapi tuende au tusiende, tukamtembele nani nalini na kinachonikasirisha zaidi ni kaka mtu kumsikiliza dadake na sio mimi mkewe.


Ikitokea mimi na mume wangu tumejadili jambo la kufanya kwa ajili ya familia yetu ndogo mume wangu anachukua simu na kumwambie kila kitu mdogo wake na kitakachosemwa na mdogo wake basi ndio kitakachofanywa na sio mimi hata kama sehemu ya jambo hilo pesa zangu zinahusika. Yaani imekuwa kama akili ya mume wangu haifanyi kazi basi anatumia ya dada yake kufanya maamuzi.


Kitu kingine kinachoniumiza roho na kunipa donge ni pale ninapotoka kazini jioni au siku za mwisho wa wiki wote tuko nyumbani, badala mume wangu atumie muda huo na mimi yeye atakuwa kwenye simu na dada yake wakiongea maongezi yasiyoisha tena kwa kilugha chao na kucheka.


Nimevumilia sana na nimefanya vikao na ndugu wa pande zote mbili na hata kuzungumza na mume wangu lakini hakuna mabadiliko yeyote, nimekuwa mkiwa ndani ya ndoa yangu na sijui nini cha kufanya, japokuwa nampenda mume wangu lakini kama suluhisho ni kutoka kwenye hii ndoa basi nitatoka ili kutafuta amani na furaha kwingine lakini sio ndani ya ndoa hii.


Wifi yangu huyu ni mkubwa zaidi ya mume wangu, ameolewa na anawatoto kadhaa wote wako Mkoani Kagera Tanzania.
Naombeni ushauri ndugu zangu"
 
Wadau karibuni tumwokoe mwenzetu katika familia yake.
 
Pole dada kwa yanayokusibu. Kabla sijachangia lolote kwa ushauri ningependa kujua je huyo wifi yako, una uhakika kuwa ni ndugu wa mumeo wa toka nitoke?
- Umesema mlijitahidi mkampeta huyo wifi huko Majuu, mnaishi naye nyumba moja au yuko kwake?
 
Pole dada kwa yanayokusibu. Kabla sijachangia lolote kwa ushauri ningependa kujua je huyo wifi yako, una uhakika kuwa ni ndugu wa mumeo wa toka nitoke?
- Umesema mlijitahidi mkampeta huyo wifi huko Majuu, mnaishi naye nyumba moja au yuko kwake?

Yeah toke ni toke tumbo moja na baba mmoja.
Yeah wanaishi pamoja hapo hapo kwao lakini yeye anafamilia yake hukooo TZ.
 
Yeah toke ni toke tumbo moja na baba mmoja.
Yeah wanaishi pamoja hapo hapo kwao lakini yeye anafamilia yake hukooo TZ.

Mh kama ni hivyo haikawii wifi alishamtafutia kaka chuma kingine so wakiwa wanapiga soga kikwao huwa wanasimuliana utamu wa huyo bi mdogo. Mwanaume gani huyo?
 
Mh kama ni hivyo haikawii wifi alishamtafutia kaka chuma kingine so wakiwa wanapiga soga kikwao huwa wanasimuliana utamu wa huyo bi mdogo. Mwanaume gani huyo?

Huyu mwanaume wa Kagera....kwao nikawaida kupiga soga na dada zao kucheka mpaka kukumbatiana wenye mioyo migumu kama wewe unaweza ukarusha ngumi.
 
Mh kama ni hivyo haikawii wifi alishamtafutia kaka chuma kingine so wakiwa wanapiga soga kikwao huwa wanasimuliana utamu wa huyo bi mdogo. Mwanaume gani huyo?
Pole sana ndugu yangu. Inabidi mume wako awe jasiri.Familia yake(ile ya ndani kabisa) ni wewe na watoto wanu. Nyie ndio wa kupewa kipa umbele cha mwanzo kabisa. Kwa taratibu na hulka zetu Waafrika na aendelee kumhudumia na kumshuhulikia kwa karibu Ndugu yake. Lakini lazima afahamu hivyo. Labda uongee naye na umuulize jee kama shilingi inabadili upande na wewe ukawa na ndugu yako wa Kiume hapo ambaye ukampa kipa umbele kuliko yeye -angejihisi vipi?
 
Uwe makini dada. Eti umesema watoto wa wifi wako Kagera. Je hao jamaa ni wahaya au ni wifi aliolewa na mhaya na watoto kaacha bukoba akakimbilia ulaya??? Kwanza kama mama hafai!! Pili kama ni kutoka Bukoba uwe makini sana. Wanaitaka kaka na dada lakini is the other side of the coin. Ni sawa na kuoa mwanamke wa Bukoba, utakutana ana mshikaji wake wa kihaya wa zamani au mpya halafu ukimkuta naye anaku introduce huyu ni kaka yangu, na huyu ni mume wangu ili uridhike!!!! Be very carefully, and put it clear to your hubby that hukuolewa na familia nzima, inlcuding the so called wifi bali uliolewa naye.
Eti umesema unampenda, huyo hakupendi kabisa kwani angekuwa anakupenda angekuweka mbele katika maamuzi yote. Simama imara na hatoki mtu hapo, yaani mimi ningezipiga tu acha liwe mbaya kabisa. Huwezi kuingilia ndoa yangu nikae kimya. Wewe uache familia yako Tz uje ughaibuni kuharibu yangu, thubutu.
 
Bonnie kwani wewe ni wa nyumbani? kama ni kweli please Tusaidie kumdefine huyu kaka yako maana tusijemjudge vibaya kumbe kikwetu ni kitu cha kawaida kabisa.
 
Mmhh jamani ni dada yake kweli au dada wa watu alidanganywa?Napata wasiwasi kuamini kuwa huyo ni wifi,na si wifi tu yawezekana ni mke mwenza kabisa,haiwezekani aingilie mambo yote ya familia kuna jambo hapo linaendelea nyuma ya pazia,na pia kwa kabila hilo wala sishangai hawana tofauti na warangi unatambulishwa kuwa huyu ni dada yangu kumbe mke au mjomba kumbe mumu mwenzio,cha muhimu hapo huyo dada ajaribu kufanya uchunguzi wa siri na anaweza kugundua kilichojificha.
 
Uwe makini dada. Eti umesema watoto wa wifi wako Kagera. Je hao jamaa ni wahaya au ni wifi aliolewa na mhaya na watoto kaacha bukoba akakimbilia ulaya??? Kwanza kama mama hafai!! Pili kama ni kutoka Bukoba uwe makini sana. Wanaitaka kaka na dada lakini is the other side of the coin. Ni sawa na kuoa mwanamke wa Bukoba, utakutana ana mshikaji wake wa kihaya wa zamani au mpya halafu ukimkuta naye anaku introduce huyu ni kaka yangu, na huyu ni mume wangu ili uridhike!!!! Be very carefully, and put it clear to your hubby that hukuolewa na familia nzima, inlcuding the so called wifi bali uliolewa naye.
Eti umesema unampenda, huyo hakupendi kabisa kwani angekuwa anakupenda angekuweka mbele katika maamuzi yote. Simama imara na hatoki mtu hapo, yaani mimi ningezipiga tu acha liwe mbaya kabisa. Huwezi kuingilia ndoa yangu nikae kimya. Wewe uache familia yako Tz uje ughaibuni kuharibu yangu, thubutu.
mkuuu naona umekuwa mkali sanaa..

vipi mbona umeichukulia personal sanaa..

actually sisi wahaya na dada zetu tuko very tight kutokana na malezi tulopewa.
tumezoea kuwa pamoja sanaa and infact dada yako ni kama mama yako tuu kwa hiyo mutueleweee..

mimi na dada yangu basilisa we are very close to the extent shemeji mwanzoni alipagawa ila later alielewaaa baaada ya kuona hata mama na mjomba walivyo close.
 
Uwe makini dada. Eti umesema watoto wa wifi wako Kagera. Je hao jamaa ni wahaya au ni wifi aliolewa na mhaya na watoto kaacha bukoba akakimbilia ulaya??? Kwanza kama mama hafai!! Pili kama ni kutoka Bukoba uwe makini sana. Wanaitaka kaka na dada lakini is the other side of the coin. Ni sawa na kuoa mwanamke wa Bukoba, utakutana ana mshikaji wake wa kihaya wa zamani au mpya halafu ukimkuta naye anaku introduce huyu ni kaka yangu, na huyu ni mume wangu ili uridhike!!!! Be very carefully, and put it clear to your hubby that hukuolewa na familia nzima, inlcuding the so called wifi bali uliolewa naye.
Eti umesema unampenda, huyo hakupendi kabisa kwani angekuwa anakupenda angekuweka mbele katika maamuzi yote. Simama imara na hatoki mtu hapo, yaani mimi ningezipiga tu acha liwe mbaya kabisa. Huwezi kuingilia ndoa yangu nikae kimya. Wewe uache familia yako Tz uje ughaibuni kuharibu yangu, thubutu.
mkuuu naona umekuwa mkali sanaa..

vipi mbona umeichukulia personal sanaa..

actually sisi wahaya na dada zetu tuko very tight kutokana na malezi tulopewa.
tumezoea kuwa pamoja sanaa and infact dada yako ni kama mama yako tuu kwa hiyo mutueleweee..

mimi na dada yangu basilisa we are very close to the extent shemeji mwanzoni alipagawa ila later alielewaaa baaada ya kuona hata mama na mjomba walivyo close.
 
Pole dada FIDEL kwa yote yaliyokukuta.
Mimi ktk ndoa yangu sina ubia na ndugu wa mke wala ndugu zangu. Tunayoamua na mke wangu huwa ndo final na kama kuwapa taarifa ni zile taarifa wanazowajibika kuzipata kwa ridhaa zetu na siyo kuwaomba watusaidie maamuzi. kama ni ushauri huwa hatulazimiki au kulazimishwi akuufuata.
 
Pole dada FIDEL

Du ee bwana eeeh!



Mimi ktk ndoa yangu sina ubia na ndugu wa mke wala ndugu zangu. Tunayoamua na mke wangu huwa ndo final na kama kuwapa taarifa ni zile taarifa wanazowajibika kuzipata kwa ridhaa zetu na siyo kuwaomba watusaidie maamuzi. kama ni ushauri huwa hatulazimiki au kulazimishwi akuufuata.

Nlidhani sijachelewa kutupa ndoano yangu kumbe si rizki (Joke)
Wifi ana bahati ya mtende wengi wanalilia maisha ya hivyo hawayapati.
 
Pole dada FIDEL kwa yote yaliyokukuta.
Mimi ktk ndoa yangu sina ubia na ndugu wa mke wala ndugu zangu. Tunayoamua na mke wangu huwa ndo final na kama kuwapa taarifa ni zile taarifa wanazowajibika kuzipata kwa ridhaa zetu na siyo kuwaomba watusaidie maamuzi. kama ni ushauri huwa hatulazimiki au kulazimishwi akuufuata.


Mkuu msanii nitake radhi.
 
wake up mami na cmama kwa miguu yako yote miwili, ulimzembea kuanzia mwanzo huyo,haipendezi/haitakiwi iwe hivyo kabisa, ni hivi alipofikia panatosha, kaa chini na mr uongee nae kiundani zaidi jinsi unavyokereka na hiyo tabia, kuwa mwazi mweleze kila linalo kutatiza juu ya wifi yako then mwambie ni wakati wa mie kuamka/kukemea! kuanzia hapo uckubali tena akuburuze huyo wifi mana ni anakuburuza, weka mpaka wako na akifikia kuuruka unamueleza ukweli wake, ikishindikana aondoke hapo home akatafute maisha yake mwenyewe, usiendekeze kabisa hii mambo, kuwa na msimamo ndoa ni ya wawili mami.
 
Nlidhani sijachelewa kutupa ndoano yangu kumbe si rizki (Joke)

Mwana huu utani mmmh!
teh teh teh teh Msanii alitaka kutupa ndoano kwi kwi kwi alitaka aliwazwe na TG.
 
Mimi ninachokiona hapa ni kwamba inaelekea huyo unayemuita wifi sio dada yake na mume wako kama alikutambulisha hivyo tangu mwanzo basi ujue alikudanganya. Pia hata kama ni dada yake iweje yeye ameolewa na ana watoto halafua awaache Bukoba yeye aishi UK? Uizi mtupu hapo. Ila kama amekuja kutembea wiki moja au mwezi mmoja na ataondoka basi umvumilie kidogo. Ila kama hatarajii kuondoka basi inabidi ufanye maamuzi ya kijeshi ya kumrudisha Bukoba akalee watoto, tena hili ufanye haraka kabla mambo hayajawa makubwa> We fikiria kama kijana wa Zimbabwe aliweza kumuoa na kumzalisha mama yake mzazi itakua dada? Changamka utaachwa mjini. Akigoma kwenda nyumbani basi maamuzi mengine sio lazima uwashirikishe kama ukisema kitu hakisikilizwi halafu financer ni wewe, fanya mwenyewe. Pia inabidi ujifunze lugha ya mmeo ili wanapozungumza uweze kunyaka. Pia ni uzembe uko kwenye ndoa miaka 5 halafu lugha ya mmeo huijui? Ndio maana wanakuteta.

Inabid mtu ushangae kidogo, dada gani ameolewa na ameacha watoto bukoba? Je mme wake humjui? Na je mmewe amfuatilii arudi? Kama hivi havifanyiki basi huyo sio dada.

Pia fikiria kumleta ndugu yako mmoja tena wa kiume ili ngoma iwe draws. Pia uwe unambania mmeo kama anapuuzia maamuzi yako, Usiwe unampa kila siku, mueleze ili upate usiwe unabisha bisha
 
Back
Top Bottom