Pole sana mkuu. Ushauri wangu ni huu: 1. Kuwa macho sana sana sana na hawa wanaokuambia wana ''tiba mbadala''. Wengi ni matapeli wanaopiga fedha na dawa zao huwa hazifanyi kazi. Na zaidi ogopa sana hawa wanaokupa dawa eg lita tano na kukuchaji fedha nyingi. Hawa ni matapeli. Narudia tena. Bnadamu wamekuwa ni zaidi ya wanyama na wengi ni matapeli. Siku yoyote kama unataka kujaribu tiba za kienyeji, epuka kabisa kulipa fedha nyingi unapopewa dawa. Kama kweli dawa zao zingekuwa zinafanya kazi, wangekuwa wanatoa kwa bei ndogo au kutaka ulipie baadae.
2. Huu ugonjwa UNAPONA hospitalini kama unatibiwa kwa usahihi na dakta sahihi pia kwa dawa sahihi. A. Una uhakika kweli anasumbuliwa na huo ugonjwa? Umejaribu kubadili hospital na vipimo? B. Dawa anazopewa anatumia kwa usahihi na dawa zenyewe siyo fake? C. Kwa sababu mara nyingi huu ugonjwa unasababishwa na vimelea vya magonjwa ya zinaa, je wewe uko clean (huna ugonjwa) na hutembei nje mara kwa mara bila kinga? D. Je, mke wako naye katulia au huwa anachepuka? C. Anajua namna sahihi ya kufanya usafi wa sehemu zake za siri? Nauliza kwa sababu wataalam wanasema mwanamke ''aki-flush ndani'' mara kwa mara anasababisha in-balance ya bakteria wazuri ndani ya uke na kuweza kupata huu ugonjwa.
Mwisho nakushauri kutumia ma-dr bingwa, kusoma sana njia sahihi za mwanamke kujisafi kwenye uke, kuhakikisha dawa unanunua sehemu sahihi na doze inatumika kama alivyoambiwa bila kuruka-ruka.