Kozi ni ndefu sana. Kwa sasa Nimemaliza kujifunza kuhusu " UCHAWI NA WANYAMA ". Hapa nimjifunza uhusiano uliopo kati ya uchawi na wanyama mbalimbali. Nimejifunza kwa nini wachawi hutumia wanyama, ndege na wadudu mbalimbali katika mambo yao ya kichawi. Nimejifunza matumizi ya kichawi kuhusu wanyama kama bundi, paka, nyegere, fundichuma, mkatasanda(ndege wa kichawi ), kivunja chungu, mbwa, mbuzi, kuku, mjusi nakadhalika.
Kwa sasa naendelea na somo refu na gumu kuhusu TUNGULI NA MATUMIZI YAKE. Kuna zaidi ya aina ELFU NANE za Tunguli. Kwa sasa nimeshajifunza tunguli kama elfu tatu, nimejifunza zinavyotengenezwa, pamoja na kazi yake. Safari bado ni ndefu sana