While Zitto is being attacked pls read here


M4C ni jambo la msingi na ni dira ya kukijenga chama nadhani unatakiwa umshauri ZITTO aungane na wenzie kujenga chama sababu kama kufikiri tofauti ni kuacha kukitumika chama na kwenda kuzunguka na SPIKA na kufanya mikutano ya mara kwa mara na KIKWETE basi ni bora afikiri kitofauti kwa niaba ya familia yake si CHADEMA.
 
Mkuu nadhani utakubaliana na mimi kua hiyo sera ya ukweli na uwazi ilikua katika maneno tu
na si katika matendo. Sisi tunataka sera ya ukweli na uwazi katika matendo na si katika maneno.

Sasa swali la kujiuliza ni je Sera hii hii ya Uwazi na Ukweli ambayo iliimbwa sana na Serikali ya awamu ya tatu chini ya CCM na haikuwekwa kwenye vitendo itatekelezwaje chini ya Serikali ya watu walewale na wa chama kilekile? Ndiyo maana watu wanahoji Zitto anautafutaji Uwazi kwenye mikataba ya madini/nishati kwenye Serikali ya watu walewale na chama kilekile kilichoshindwa kuiweka kwenye vitendo Sera ya Ukweli na Uwazi? Tafakari.
 

bora umesema..unajua watanzania tuna ushabiki tu..mtu akiwa na 5mins of fame basi kila mtu anamshabikia hatujui really nini kinachoendelea behind the scenes...kila mtu alikua anasema JK ni mtu wa watu kijana mwenzetu atamtoa kila mtanzania kwenye umaskini..akapewa kura zote zile 2005...i think we all know what happened next!!
 
Watu wanamchukia Zitto bila sababu yoyote ile

Sidhani kama kuna mtu anayemchukia Zitto Kama Zitto. Kinachochukiwa kutoka kwa Zitto ni tabia yake ya kukubali kununuliwa kirahisi. Zitto anadhani peke yake anaweza kuleta mabadiliko katika Nchi yetu. Kupata mabadiliko ya kweli; Lazima aunganishe nguvu zake na zawenzake ili ushindi wa kweli upatikane. Dhambi ya kupanga mipango ya kuihujumu CDM lazima imwandame hadi mwisho wa maisha yake. Anatamani sana kuanza kutembea kabla ya kuanza kutambaa. Zitto lazima atambue kuwa maisha ni hatua na haihitaji haraka kwani mambo mazuri lazima yaje kwa wakati.
 

Tatizo la Zitto anauota Urais hata akiwa barabarani anatembea. Tamaa ya fisi.
 
Zitto aachane na Mkono!

Kuna interests nyingi nyuma ya jitihada hizi japo ni kwa maslahi ya Taifa lakini ni vigumu sana kwa ZZK kuaminika for the time being!
 
KWA HIYO TUNAJADILI JINA la ZITTO ZUBERI KABWE(MBUNGE) AMA ISSUE?KWA TAARIFA YENU UKITAMKA REVIEW KWA WACHIMBA MADINI WAKIJUA UNA NGUVU FULANI WANAKUTUMIA UJUMBE WA KHERI HAPO HAPO NA UKIZIDI KUKUNJA SHINGO WATALETA AJALI,MAJAMBAZI AMA SUMU YA RUSSIA,HILO NENO REVIEW LIMEWATAJIRISHA WENGI!
 
... ??????????????????????????

 
The problem with our hero is his inconsistency over the same issue. He was vociferous in the forefront to demand review of the same contracts he pointed out to Tanzanians as unfair, corrupt and that benefited investors more than us. And he did this with the full backing of his party to which he was and is still the Deputy Sec Gen.

Today he comes with a different stance that appears to be pro investors, this time without the official backing of his party. A common thinker has to ask him/herself what made this same man contradict his stance within a short spell of time.
This is what makes Tanzanians to act cautiously with our once super hero.
 
Tatizo la Zitto anauota Urais hata akiwa barabarani anatembea. Tamaa ya fisi.

Katongozwa katongozeka sana kwa kubinyiwa jicho tuu na MSACKY..sasa anaota ndoa na tamaa zake zinazidi kua hakuan cha kukata kiu,anaamini ndoa tuu ndio itakaa hiyo kiu.Huku ajajua tofauti ya "infatuation" na "Love" kwa i dunia yake inakimbia haraka sana,tena sana kiasi cha kumfanya ashindwe tofautisha sana mambo.
 

Mkuu Kitila naomba nitofautianae na mtazamo wako kwasababu kuu moja kumekuwa na kundi ambalo linatumia hizo movement za zitto kuudharirisha uongozi wa juu wa CDM kama Mbowe, Dr Slaa, BAVICHA, mambo ya udini na ukanda ktk chama na hiyo ndio imesababisha zitto aonekane mnafki na majina mengi. Nyie kama viongozi mnatakiwa muangalie hizo weakness kwa ustawi wa CDM.
 
Hivi niulize swali moja ambalo sijawahi kusikia mtu akilizungumzia. Kuna wakati wowote Zitto amewahi kuzungumzia siasa za Ukanda na Udini ndani ya Chadema?
 
Kosa la zito ni moja na dogo 2 na anaweza kujirekebisha,ni kupenda kusimama pembeni ya chama,haya mambo yote anatakiwa kuyafanya kwa kushirikiana na chama na kupata ushauri na baraka za chama.kutofanya hivi kunaleta wasiwasi juu ya maslahi aliyonayo huko mpaka afanye peke yake au kwa kushirikiana na watu wanaojulikana kwa uchafu wao (mafisadi).
 
Naona Zitto anatafuta mbinu ya Julias Marema maana amepoteza supporters wengi kwenye chama chake

Je hii mbinu yake ya kutaka kureview hii mikataba itamsadia?

Just doing for the sake of a poor country and your grandsons. Polepole mtamuelewa tu.
 
i don't know who to believe anymore..and kitila's statement ,somehow,i mean wassira is almost right,let's pray the party is not broken into pieces before 2015..
 
Great thinker naona wengi wameanza poteza muelekeo na wamekuwa waongeaji sana bila vitendo na wengine wamekuwa hata wasemaji wa vyama au kundi la watu, mimi ningependa kuona mwaleta ushahidi za tuhuma za zzk hapa si porojo na kama mnasema yupo karibu na serekali na chama kimekuwa kimya then kunajambo kina pata kwa ukaribu huo wa zzk na serekali, pia watu wengi mnapiga porojo za m4c kwa zzk but mimi najua wabunge wengi sana wa chadema ambao hawafanyi shughuli hii ukianza na shibuda then why zzk? Pia kwenye chaguzi zote ndogo za wabunge na madiwani zzk huwa hakosi je hapa anatumikia chama gani? Mwisho Kama zzk ni mzigo hope chama kingekuwa kimesha mwita na kumuonya juu ya uwajibikaji wake but sijawahi sikia mwenyekiti wala katibu mkuu wakimnyoeshea kidole zzk then nyie Mliyo nje ya chumba mtikisiko wa kitanda unawatisha nini ? chadema nw is strong than ever let us know new face and talent, so zzk atulie na afanye anayo fanya kwani na imani chama kinanufaika kwa anayoona huko serekalini
 
Kwanza nimpongeze kakangu Dr. Mkumbo kwa jinsi alivojaribu kufafanua juu ya alivyo zito. Mi nafikiri tusiwe na conclusive statements juu ya Zitto kisa tu eti anafikiri tofauti na sisi, hatutaenda haki kwa Ndg yetu Zitto hata kidogo. Zitto ni mwanasiasa mchanga wengi wanaomfahamu toka yuko sekondari na Chuo pale mlimani ni mtu makini anayependa kusimamia anachokiamini, na mda mwingine huwa yuko tayari hata kusimama peke yake kutetea anachokiamini na hii ndio sifa kubwa ya viongozi wengi duniani ilimradi tu anachokisimamia na kukiamini kiwe na maslahi kwa waliowengi. Tumeona hivyo kwa Mwal. kipindi cha uongozi wake kuna kipindi aliotofautiana na wenzake ndani ya chama akawambia CCM sio mama yake kwa kuwa alijua anachosimamia, vivyo hivyo mapema miaka ya mwanzoni kuna hata waliotaka kumpindua kwa kufikiri tofauti na yeye. Na kwa CDM mimi nafikiri ili chama hiki imara kiwe imara we need a diverse of views and sometimes our ideas may differ as far as we think differently. Zitto asihukumiwe kwa lolote kwa sasa, personaly bado namuona Zitto kama kiongozi shujaa, makini, visionary, mzalendo, na wa mfano kwa vijana wengi na ambae atakisaidia sana chama huko mbele. Mfano mzuri ni katika kutetea rasilimali za nchi kutonufaisha wachache. Tutafute taarifa sahihi kumhukumu kiongozi huyu sio uvumi unaletwa na wasioitakia mema CDM tutakuja kujuta baadae.

Na kwako zitto huu ni wakati wa changamoto ndio wakati wa kusimama imara katika kuwatumikia watanzania, tunakuamini chapa kazi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…