WhatsApp kutumia Username badala namba ya simu

WhatsApp kutumia Username badala namba ya simu

Whatsapp inacopy mambo mengi mpaka inaanza kupoteza ule upekee wake, upekee ndio unafanya utumie mtandao fulani kwa sababu unachokipata humo hakipatikani kwenye mitandao mingine. Inapoteza mvuto, walivyoweka tu channels nimeanza kuiona ya ajabu.
Shida ni namna walivyo ziweka yani ni kama private groups hazina mvuto.
 
Huwa nashangaa marafiki wanajiunga telegram kwa fujo halafu baadae ukifuatilia unaona seen long time ago nashangaa na kujiambia hawa wamezoea wasap na faceook tu. Uhondo wa huku hawaujui, hawajui kutafuta wanacho kitaka na hawataki kuuliza. Naamua kukausha tu.
Shida wanaitumia Telegram kama WhatsApp au Facebook ndiyo makosa yanapoanzia hapo.
Ila wangeijua Telegram kwa undani zaidi wangekuwa muda wote wanaingia Telegram. Tangu nilipoifahamu Telegram sijawahi kujuta
 
Whatsapp inacopy mambo mengi mpaka inaanza kupoteza ule upekee wake, upekee ndio unafanya utumie mtandao fulani kwa sababu unachokipata humo hakipatikani kwenye mitandao mingine. Inapoteza mvuto, walivyoweka tu channels nimeanza kuiona ya ajabu.
Whatsapp inatakiwa ibaki na ule upekee wake kuwa ni simple na inaheshimika. Ila wakianza kuleta mambo ya telegram watapotea na kuoneka hawana mana
 
Hivi telegram huwa kazi yake nini zaidi ya watu kutafuta zile mambo, binafsi nimejiunga lakini hata sijui kwanini nilijiunga
Ushamba wako unatokana na yale MACHANJO yale!!!

Unayakumbuka???

MACHANJO DOT COM 🙈
 
Whatsapp inatakiwa ibaki na ule upekee wake kuwa ni simple na inaheshimika. Ila wakianza kuleta mambo ya telegram watapotea na kuoneka hawana mana
Tengeneza na wewe mtandao wako uuite MACHANJO DOT YAHOO
 
Mimi nilishaacha kutumia WhatsApp kutokana na hizi features mpya wanazoongeza. WhatsApp ilikuwa ni mtandao mzuri kuwasiliana na ndugu, jamaa na marafiki: walipoleta "Status" mtandao ukabadilika kwenye Status za watu unakuta videos, picha ambazo huhitaji kuziona maana lengo kuu la mtandao ilikuwa ni kutumiana jumbe, picha na video baina ya mtu na mtu.

Wakaja kuharibu zaidi kwa kuweka "Channels" ambazo ukiingia tu unakuta suggestions kibao ambazo huzihitaji maana tayari kila kitu kwenye Channels kipo kwenye Social Work zao: Instagram, Facebook.

Meta pia wameharibu mitandao ya Facebook na Instagram kwa kuweka "Reels" na "Suggestion Posts" unaingia mtandaoni badala uone posts za watu uliowa-follow unakutana na mavitu ya ajabuajabu tu.

Facebook ilikuwa mtandao wa kuungasha ndugu na marafiki. Instagram ilikuwa mtandao wa kuweka picha na matukio ila sasa hivi imekuwa kama uwanja wa picha za utupu na video TikTok.

Meta wajitafakari, hizi updates zinaharibu maana ya mitandao ilivyoanzishwa.
 
Ushamba wako unatokana na yale MACHANJO yale!!!

Unayakumbuka???

MACHANJO DOT COM 🙈
Sometimes huwa napata mashaka na jinsia yako, mwanzo nilidhani wewe ni me. Pia umewahi kujiuliza kwanini kila mtu humu anakudharau?
 
Back
Top Bottom