What they call it a constant is not constant!

Hili ni suala la kiimani zaidi, kumbuka hata ulimwengu wote na vitu vilivyomo viliumbwa kwa Imani. Suala la Wanasayansi kufanya assumptions wakati wanapokuwa wana-create vitu wanakuwa ndani ya misingi ile ile ya imani. Kila kitu unachokifanya maishani mwako ili kiweze kutokea ni lazima ufanye assumptions ili kiweze kutokea kwa maana nyingine ni lazima ufanye kitendo cha Imani ili kitokee.

Mf. 1.Ukitaka kusafiri ili uweze kufika sehemu unayotaka kwenda lazima ufanye contant assumptions kwamba kama gari haitapata ajali, haitaharibika utafika salama, 2.Unafanya biashara lazima uweke assumptions kama utapata wateja, hutaibiwa, utatengeneza faida,3. Ukipanga mipango yako ya kesho, mwezi ujao au miaka ijayo lazima uweke assumption kama MUNGU akipenda ukawa na uhai utaifanikisha mipango yako, n.k, n.k.

Wanasayansi nao wanapofanya assumptions kitendo cha Imani ili kufanikisha yale wanayotarajia kuyaona. Hakuna utakachoweza kufanikisha katika maisha kama hujaweka assumptions( constant )
 
Sasa mbona tunakubaliana. Umeshasema kuwa equation ile ni "good approximation!!". Maana yake ni kuwa katika matumizi halisi (practical applications) madhara ya migongano kutokuwa "perfectly elastic", madhara ya "intramolecular forces", madhara ya hivyo vitu vingine vyote ni madogo tu. Hapo ndo maana ya approximations.

Tunatengeneza hypothetical ideal gas ili tuweze kutumia milinganyo kukokotoa matokeo fulani fulani. Ndiyo maana inabidi ukokotoaji huo ufuatwe na majaribio halisi. Majaribio hayo huthibitisha kuwa madhara ya vitu vile tulivyovipuuzia kwenye milinganyo ni madogo mno kwenye tokeo la mwisho. Tukishajiridhisha hivyo kwa kufanya majaribio ya kutosha na kulinganisha na matokeo ya kimahesabu ndio maana inawezekana watu kujua hata kiwango cha kosa (Margin of error). Kutokana na kujua kiwango cha kosa, kwenye matumizi halisi (practical application), Callibration hufanyika ili kuondoa kosa hilo.

Ndugu yangu, ndo maana watu walikwenda kwenye mwezi na wakarudi salama. Ingekuwa "approximations" maana yake ni uongo matokeo yake ungeyaona. Ndo uzuri wa sayansi. Tena akija mtu mwingine akatumia milinganyo ile ile na kufanya "assumptions" zile zile, matokeo yake huwa ni yale yale. Hapa ndo tunasema sayansi ni "superior" kuliko maalifa mengine ambayo binadam ameshayapata.

Tatizo la maarifa mengine kama yale ya dini na ushirikina, au mazingaombwe; mtu mwingine hawezi kuiga ulichofanya wewe na akapata matokeo sawa. Kwenye dini mtu unaweza ukafanya yale yale aliyofanya mwenzio, yeye akafanikiwa, wewe ukashindwa; halafu mtu akasema aaaa si mapaenzi ya mungu!!!! Mungu huamua pale anapotaka!!!!! n.k. Inaonekana maarifa kuhusu mungu anataka nini na wakati gani hayatoshi na kilichobaki tunakuwa tunadanganyana tu!

Sayansi ni mwisho wa uongo. Approximations na assumptions kama zimekosewa, ni wazi kiwango cha kosa (error margin) kitakosewa. Kiwango cha kosa kikikosewa "callibration" ya kuondoa kosa hilo haitafanikiwa. Kosa lisipoondolewa, balaa litaonekana kwenye matokeo ya mwisho; yaani kama ni jengo litadondoka, kama ni ndege italipuka hewani au kuanguka, n.k. Uhandisi wote uliopo, tiba, n.k. vyote hutegemea approximations na assumptions. Ukiona hizo fani zinafanikiwa na kutoa matokeo halisi, ujue assumpitions na approximations ni halisi!!!

Mkuu nakushauri hiyo Paragraph ya pili kutoka mwisho uiondoe, ina mapungufu makubwa sana ambayo yanaweza kusababisha hata hayo mazuri unayoelezea kuhusu sayansi yadharaulike, kwa sababu hiyo sayansi ni design of God, na hivyo viassumptions vyenu mnavyovifanya ni kwa sababu ya ama kukosa ufahamu wa kuvioncorporate kwenye formula zenu au huwa mnavifanyia reference kimakosa, lakini God know them ALL.

Kumbuka mnafanikiwa kuyafahamu na kuunga unga tu lakini hamna uwezo wa kutengeneza kitu chochote kile. sasa unapoanza kuchallenge credibility ya maandiko ya Mungu nashindwa kukuelewa.

Toa hiyo paragraph utupe fursa wengine ya kuendelea kufaudu uelewa wenu mzuri juu ya sayansi.
 
Dhana ya CONSTANT ni muhimu sana kwa watu wanaokariri,ukianza kutafakari tu,CONSTANT ni uzushi kweupe,wanasayansi wengi sana walitumia Constant ili kufikia hitimisho ya kile ambacho wameshindwa kukitambua kutokana na mapungufu ya kibinadam, Kama wahasibu vile,trial balance ikigoma unaweka balancing figure, kwa kuweka suspense akaunti,wakati wahasibu wanakuwa na kibarua cha kuondoa hiyo balancing figure,wanasayansi wanakomea hapoooooooooo hapo. Na wengine huendeleza utafiti kwaanzia na fix husika na kwenda mbele,huku wakitegemea peer review,kwa miaka mingi sana mwanafizikia Isaac Newton kwa kutumia sayansi hiyo hiyo aliupiga fix ulimwengu,na kwa kuwa wengi sayansi ni kukariri kwa kwenda mbele,baada ya kuoneshwa mapungufu ya kazi nyingi za Newton baadala ya kufunguka na kuona Fix zilivyonyingi kwenye sayansi ndio wanajikita kueneza imani kwa sayansi ndiyo mwake kila kitu kiko waaaah.

Wahasibu tupo hapa. Hiki kitu unaita balancing figure, nakushauri ukiondoe kwenye text yako, Nimesoma vitabu vingi sana vya accounting theories and princiles hakuna sehemu mhasibu anashauriwa kuweka balancing figure, naomba uiondoe sababu kwanza ni uongo na pili unashushia hadhi ya CONSTANT inayojadiriwa hapa.
 
naona unaiponda sayansi kwa halii na mali na ndo imekuwezesha kutu postia mawazo yako mgando hapa!
 
Nadahani sina cha kuongeza hapa, majibu waliyotoa wenzangu yanatosha. Huzuni yangu ni jinsi mtoa swali anavyoonesha kuwa na upeo mdogo kwenye maswala haya. Hata hivyo naamini nia yake ni kuelimishwa na kwamba ameelimika vizuri hapa.
 
Ebhana umenikumbusha pindi niko Iyunga Tech a-level, maneno assume, neglect, constant na negligible yalikua yametawala in physics. I would buy that idea that we use assumptions just to simplify life but in real life they ain't make no sense.
 
Tatizo lako ni kuwa unafikiria Constant Maana yake ni namba isiyobadirika. Kuna constants kama PI ambazo hazibadiriki. Lakini katika milinganyo kama hiyo, constant ni namba ambayo kuwepo kwake hakuathiriwi na "variables" za mlinganyo wenyewe. Kwenye mlinganyo huo ulioutoa maana yake ni kuwa nR haiathiriwi kwa vyovyote vile na P, V na T.
Sasa tuje kwenye "assumptions". Nadhani unajidanganya kwa kusema eti kwa sababu kuna "assumptions" ndo maana huamini sayansi!!! Mhhh, hapo naona ajenda yako ni nyingine. Ungesema kuwepo kwa "assumptions" kunafanya vitu vishindikane!! Hapo ungeleleweka! Sasa ukiangalia mfano wa ndege ulioutoa na eti zimefanyika "assumptions" nyingi!! Ni kweli zimefanyika, je ndege hairuki na ikatua?? Ni mamilioni mangapi ya watu wanasafiri kila mwaka kwa kutumia ndege?

"Assumptions" ni vitu ambavyo madhara yake kwenye matokeo ya mwisho ni madogo mno pamoja na kuwa vipo. Nadhani "assumptions" zinaonesha ushindi zaidi kwa sayansi kuliko kushindwa. "Assumptions" zinaonesha kuwa yule anayezifanya anazijua kuwa zipo; zinaweza kuleta madhara katika mazingira fulani; ila katika jambo hilo hazina madhara. Kwa mfano unapojumlisha namba moja kubwa sana na namba moja ndogo sana, katika matumizi ya kawaida tunasema ile namba ndogo sana ni sifuri na hivyo mchango wake kwenye jumla nzima hauna maana (tunaupuuzia - neglect).

Kuzungumzia 0-2 na kupata -2 mbona hili ni jambo linaloelezeka kirahisi sana. -2 ni deni. Hiyo mbili umeikopa kutoka sehemu fulani ndo ukaiweka pale (ndo maana inabidi uweke - kumaanisha kuwa hii mbili imekopwa kutoka mahali). Pengine wewe ulisoma hesabu tu kama kasuku hukufundishwa matumizi ya mahesabu ndo maana unachanganywa na mambo yanayoelezeka kirahisi mno. Ni kweli kuwa waalimu wengi huwa wanapofundisha hawayaweki mambo haya katika "context", kwa hiyo, "casual learner" unaona kama unafanyiwa mazingaombwe au viinimacho. Hapana, si viinimacho hivyo!!


Well said dude!!
Sina cha kuongeza kwani umejibu na kujaribu kumwelewesha vizuri sana ila pia inawezekana huyu jamaa hajui maana ya maneno "constant" na "assumption".

Lakini pia namshauri ajifunze kuhusu models and modelling itamsaidia kuilewa science and scientifi assuptions; kwani hizo formula anazoelezea ni models zinazotumika kusolve real life problems na watu maisha yanaenda-wanapata magali, ndege meli, maghorofa hata viti anavyokalia nk vyote vinaanzia kwenye ideal models to real things. kwa taarifa yake "SCIENCE IN THE ONLY REAL DISCIPLINE"
 
we mwongo wewe katika fluid mechanics hakuna PV=nRT....labda ungesema kinetic theory of matter au Thermodynamics usitudanganye toka hapa!
 
penda mijadala kama hii inatufungua macho ila tusitukanane ila tuelimishane ili kutoa ujinga hii italeta maana kwa great thinkers
 
Ther real question here is not that "ceteris paribus" is not practical.

The real question here is, is anything knowable beyond any degree of doubt?

The process of knowing itself interferes with the knowability of the item under observation, how can we know anything beyond any degree of doubt?
 
CONSTANT VARIABLE! in fizikia mfano gravitational constant varying inverse proportion to square of distance between point masses! My word.
 
we mwongo wewe katika fluid mechanics hakuna PV=nRT....labda ungesema kinetic theory of matter au Thermodynamics usitudanganye toka hapa!

Duh wewe mshikaji hapo sikuelewi, Fluid Mechanics itakosaje PV wakati P - pressure, V- Volume, T- tempereture, sasa unapoongelea Fluid utaachaje kuogelea Pressure au tempareture? utawezaje kuandika au kutafiti tabia za Fluid bila kuhusisha Temperature au Volume na Pressure?

Unasema labda kwenye kinetic theory, unaelewa kinetic theory inaelezea nini haswa? utatenganisha vipi Kinetic theory na Fluid?
 
Back
Top Bottom