Nazikumbuka siku zile. Nilikuwa shule ya msingi. Daftari limeisha u aenda nalo, store keeper anatoboa kwa kutumia punching machine, unapewa daftari jipya, kalamu unapewa, kitabu unapewa.Never mkuu
Labda tuache ushirikina na wizi
I wish ungeendeleza hii point yakoIla waafrika tunapokuwa tunajaribu kuelezea kwanini tupo nyuma kimaendeleo huwa kila mtu anaongea lake mbali kabisa na mwenzie tunachanganya mambo ambayo hayahusiani na kuwa kwetu nyuma kimaendeleo.
Nazikumbuka siku zile. Nilikuwa shule ya msingi. Daftari limeisha u aenda nalo, store keeper anatoboa kwa kutumia punching machine, unapewa daftari jipya, kalamu unapewa, kitabu unapewa.
Waliokuwa sekondari, wanakwenda na kurudi makwao kwa gharama ya Serikali.
Nimefika Sekondari, utaratibu ni ule ule, unapewa daftari, tena kubwa zaidi na zuri zaidi kuliko yale ya shule za msingi. Asubuhi chai kwa viazi mviringo, saa 4 asubuhi wakati wa break, mnapata maziwa. Wakati wa likuzo unapewa cash money kwenda na kurudi.
Kufika chuo kikuu unakuwa tajiri mdogo, nauli unapewa ya daraja la pili (zaidi ya nauli ya basi kwa sababu basi ni daraja la 3), mwisho wa mwezi una high learning allowance, una faculty requirements allowance, una book allowance, na una meal allowance. Wakati mwingine unaambiwa kuwa kuna arrears, eti wakati unalipwa travel allowance, nauli ziilikuja kupanda baadaye, wewe mwebyewe mhusika huna hata habaru. Sisi wengine, allowance za UDSM mpaka tuliwasomeshea wadogo zetu private secondary schools.
Awamu ya tano ilipoingia viwanda vingi vilikufaMtu mnafiki, mwongo, na ambaye hana uhuru wa mawazo huwa hagundui kitu chochote, akijitahidi ataishia kuiga na kukariri.
Moja ya sababu, wanasaikolojia wanasema kwa nchi ya China kutokufanya ugunduzi, na kuwa nchi ya copy and paste, ni wananchi wake kuelelewa katika mazingira yasiyoheshimu uhuru wa mtu.
Tanzania kuna wakati ilikuwa inaunganisha malori aina ya Scania, sasa hivi tumeishia kuunganisha pikipiki za China.
Kuna wakati tulikuwa tunaunganisha matrekta bora kabisa ya valmet, sahizi hatuunganishi hata power tiller.
Tulikuwa tunatengeneza baiskeli aina ya swala, baiskeli nzuri kabisa,sahizi hatutengenezi hata sindano ya cherehani.
Kuna wakati tulikuwa tunatengeneza matairi bora kabisa yakijulikana General Tyre, sahizi tumebakia kuwa watumiaji wa matairi ya hovyo kabisa kwa ubora kutoka China.
Kuna wakati tulikuwa tunatengeneza mashuka bora kabisa toka kiwanda cha Mutex, siku hizi tumebakia kuwa watumiaji wa mashuka ya hovyo kabisa, yapo kama vikaratasi, kutoka China.
Kuna wakati tulikuwa tunatengeneza viatu bora vya ngozi toka kiwanda cha Moro Shoes, siku hizi tumebakia kuwa wanunuzi wa viatu duni kabisa toka China, ukijikwaa tu kimechanika au kuraruka.
Tulikuwa tunatengeneza ndoo za ubora wa hali ya juu, Amboni Plastics, siku hizi tumebakia na ndoo takataka ukibebea tu maji, mshikio unachomoka au ndoo yenyewe kupasuka.
Wakati ule ilikuwa kipimo cha umaskini kwa mama ni kuvaa kanga iliyotengenezwa China au India, huku mwenye uwezo akivaa kanga ya Urafiki, leo hata ukiwa na hela, kanga nzuri huipati popote, kila mahali ni takataka za kutoka China.
Zamani, katika Afrika Mashariki, Tanzania ndiyo nchi angalao ilikuwa inaonekana kuwa na demokrasia, leo ndiyo nchi ya mfano kwa utawala usiozingatia sheria, usioheshimu mgawanyo wa mihimili. Tena imekuwa ni nchi ya kidikteta ambayo hata kura ya mwananchi haina maana yoyote katika kuwapata viongozi.
Kenya tuliokuwa tunawaona hawajastaarabika kwa kuendekeza siasa za ukabila, sasa ni nchi ya mfano Afrika Mashariki kwa kuheshimu utawala wa sheria, demokrasia, haki za watu, uhuru wa maoni, na katika kuheshimu mfumo wa siasa za vyama vingi.
Wakati wenzetu, kuendelea inamaanisha kuboresha, sisi kuendelea inamaanisha kuendeleza uharibifu. Tumekuwa Taifa bandia, taifa linaloongozwa kwa hadaa na ulaghai. Majukwaani wanatamka vingine, matendo yanakuwa kinyume. Wateule wamebakia kuumsifia anayewateua kwa unafiki. Kila mahali watasimama na kumsifia aliyewateua ili awaone na kuwasikia, wakiachia mic, wanamsema vibaya. Unafiki mtupu.
Watawala, hata pale ambapo mambo yanaenda vibaya, watakuambia kuwa sasa ndiyo tunapaa, wakati hata vyandarua vya mbu tunapewa msaada. Zamani, Serikali ilikuwa na watu wanapita mitaani kufanya fumigation kuua mbu na mende, leo tunashindwa hata kununua chanjo kwaajili ya watoto wetu wanaozaliwa.
Ni nani atalirudisha Taifa kutoka kwenye unafiki kulipeleka katika uhalisia? Nani ataweza kusimama na kusema kuwa Taifa letu ni duni katika nyanja nyingi, tusimame, turudi na kuanza upya?
Siku zote hatua ya kwanza kuleta mabadiliko chanya ni kuutambua na kuukubali udhaifu wako.
Nakumbuka Stephen Kibona rip miaka ile alinunua 504 mpya pale Peugeot House!Mtu mnafiki, mwongo, na ambaye hana uhuru wa mawazo huwa hagundui kitu chochote, akijitahidi ataishia kuiga na kukariri.
Moja ya sababu, wanasaikolojia wanasema kwa nchi ya China kutokufanya ugunduzi, na kuwa nchi ya copy and paste, ni wananchi wake kuelelewa katika mazingira yasiyoheshimu uhuru wa mtu.
Tanzania kuna wakati ilikuwa inaunganisha malori aina ya Scania, sasa hivi tumeishia kuunganisha pikipiki za China.
Kuna wakati tulikuwa tunaunganisha matrekta bora kabisa ya valmet, sahizi hatuunganishi hata power tiller.
Tulikuwa tunatengeneza baiskeli aina ya swala, baiskeli nzuri kabisa,sahizi hatutengenezi hata sindano ya cherehani.
Kuna wakati tulikuwa tunatengeneza matairi bora kabisa yakijulikana General Tyre, sahizi tumebakia kuwa watumiaji wa matairi ya hovyo kabisa kwa ubora kutoka China.
Kuna wakati tulikuwa tunatengeneza mashuka bora kabisa toka kiwanda cha Mutex, siku hizi tumebakia kuwa watumiaji wa mashuka ya hovyo kabisa, yapo kama vikaratasi, kutoka China.
Kuna wakati tulikuwa tunatengeneza viatu bora vya ngozi toka kiwanda cha Moro Shoes, siku hizi tumebakia kuwa wanunuzi wa viatu duni kabisa toka China, ukijikwaa tu kimechanika au kuraruka.
Tulikuwa tunatengeneza ndoo za ubora wa hali ya juu, Amboni Plastics, siku hizi tumebakia na ndoo takataka ukibebea tu maji, mshikio unachomoka au ndoo yenyewe kupasuka.
Wakati ule ilikuwa kipimo cha umaskini kwa mama ni kuvaa kanga iliyotengenezwa China au India, huku mwenye uwezo akivaa kanga ya Urafiki, leo hata ukiwa na hela, kanga nzuri huipati popote, kila mahali ni takataka za kutoka China.
Zamani, katika Afrika Mashariki, Tanzania ndiyo nchi angalao ilikuwa inaonekana kuwa na demokrasia, leo ndiyo nchi ya mfano kwa utawala usiozingatia sheria, usioheshimu mgawanyo wa mihimili. Tena imekuwa ni nchi ya kidikteta ambayo hata kura ya mwananchi haina maana yoyote katika kuwapata viongozi.
Kenya tuliokuwa tunawaona hawajastaarabika kwa kuendekeza siasa za ukabila, sasa ni nchi ya mfano Afrika Mashariki kwa kuheshimu utawala wa sheria, demokrasia, haki za watu, uhuru wa maoni, na katika kuheshimu mfumo wa siasa za vyama vingi.
Wakati wenzetu, kuendelea inamaanisha kuboresha, sisi kuendelea inamaanisha kuendeleza uharibifu. Tumekuwa Taifa bandia, taifa linaloongozwa kwa hadaa na ulaghai. Majukwaani wanatamka vingine, matendo yanakuwa kinyume. Wateule wamebakia kuumsifia anayewateua kwa unafiki. Kila mahali watasimama na kumsifia aliyewateua ili awaone na kuwasikia, wakiachia mic, wanamsema vibaya. Unafiki mtupu.
Watawala, hata pale ambapo mambo yanaenda vibaya, watakuambia kuwa sasa ndiyo tunapaa, wakati hata vyandarua vya mbu tunapewa msaada. Zamani, Serikali ilikuwa na watu wanapita mitaani kufanya fumigation kuua mbu na mende, leo tunashindwa hata kununua chanjo kwaajili ya watoto wetu wanaozaliwa.
Ni nani atalirudisha Taifa kutoka kwenye unafiki kulipeleka katika uhalisia? Nani ataweza kusimama na kusema kuwa Taifa letu ni duni katika nyanja nyingi, tusimame, turudi na kuanza upya?
Siku zote hatua ya kwanza kuleta mabadiliko chanya ni kuutambua na kuukubali udhaifu wako.
Wizi ni tabia ya mtu. Mbona wengine, kama kungekuwa na jukwaa ambalo nchi nzima wanaweza kukuona, tungepanda juu ya jukwaa hilo na kuuliza kama kuna mtu yeyote ana tuhuma dhidi yetu ya kuiba mali ya mtu binafsi, taasisi au Serikali, na kwa uhakika wa 100% asingepatikana.Asilimia kubwa ya hao waliosomeshwa ndo wamekuja kuwa wezi wakubwa....achilia mbali Ile "entitlement behaviour"waliyo kuwa nayo
Nyakati zile si wengi walikuwa na magari, lakini wachache waliokuwa na magari walikuwawananunua brand new cars, siyo hii mitumba tunayoinunua leo.Nakumbuka Stephen Kibona rip miaka ile alinunua 504 mpya pale Peugeot House!
Siku hizi mabehewa hadi Kigwangalla machale yanamcheza
Asante Bombabomba. Mungu atujalie maisha marefu yenye afya njema ili siku moja tushuhudie nchi yetu ikipiga hatua za maendeleo, maendeleo yanayoonekana.Mkuu Bams hongera sana. Huwa nasoma mada zako zote hapa jamii forum. Japo hatufahamiani lkn ni wazi kwamba wewe ni mmojawapo wa wenye uelewa mzuri na upo tayari kuisaidia jamii. Mungu akujalie afya njema ya mwili na roho tunaokusoma tuendelee kufurahia na kunufaika na uwepo wako.
Mkuu hili la watu kuwa na magari mapya ni kweli kabisaNyakati zile si wengi walikuwa na magari, lakini wachache waliokuwa na magari walikuwawananunua brand new cars, siyo hii mitumba tunayoinunua leo.
Hata kwenye mavazi, ukivaa mitumba ilikuwa inaonekana wewe ni mtu duni kabisa, ambaye hujiwezi. Na hizo second hand clothes zilikuwa zinapatikana zaidi kwa mapadre_misheni, na mara nyingi zilitolewa bure. Nguo zile tulikuwa tunaziita, "KAFAULAYA"
Namkumbuka Prof. Kweka (RIP) alipokuwa anafundisha Development Studies (DS) pale UDSM, akawa anasema:
"Symptoms of poverty - living on second items. Second hand clothes, second hand cars, some go further, to marry second hand wives because they are not able to pay required dowry for a virgin girl"