Pascal Mayalla
Platinum Member
- Sep 22, 2008
- 50,498
- 113,602
Preamble!.
"Ukiona mwenzako ananyolewa!"
na "Ukiona kwa mwenzako kuna ungua!, kwako kunateketea!"
Wale wote wenye matumaini na mategemeo kuwa kuna siku upinzani wa nchi hii, utakuja kushika dola!, hawa ni wishful thinkers na day dreamers, wanao ota ndoto za mchana, wasahau kabisa!.
Lengo la uzi huu ni kuwaanda kisaikolojia, wale wote wenye matumaini chanya, kuwa Tanzania ni nchi ya vyama vingi vya siasa, hivyo kuwa na mategemeo, kuna siku itafika, ambapo wapinzania pia watashika dola, na CCM itakuwa ni chama cha upinzani!, wasahau kabisa hili jambo, ili kuwazui kupata depression inayotokana na despair, kufuatia kuwa na too much great expectations kuwa kuna siku upinzani wa nchi hii, utakuja kushika dola!.
CCM inandaa kifo rasmi cha upinzani kwa dose za taratibu, na kuandaa kaburi la kuuzika jumla upinzani wa Tanzania!, na utauzika for good!.
Mkakati wenyewe uko hivi!
Miongoni mwa maazimio ya kikao cha NEC ya CCM kilichomalizika leo mjini Dodoma, kimeazimia CCM kuachana kabisa na kutegemea ruzuku, na badala yake CCM sasa kijigeuze kutoka chama cha kijamaa, kugeuka chama cha kibepari, kianze kufanya biashara kubwa kubwa kwa kuanzia na real estates, kizalishe fedha nyingi, kijitegemee, badala ya hali ilivyo sasa, kinajiendesha kwa kutegemea ruzuku!.
CCM Chama Kubwa! Chama Dola, Chama Tajiri!
Watu wote wanajua fika kuwa CCM ndio chama kikubwa kuliko vyote Tanzania!, licha ya kuwa ni chama dola, yaani ukizungumzia serikali ya Tanzania, unazungumzia CCM, yaani CCM ndio serikali ya Tanzania yenye jeshi, polisi, bunge na mahakama!, ndicho chama chenye wanachama wengi kuliko chama kingine chochote Tanzania!, ndicho chama tajiri, kuliko chama kingine chochote tanzania, na ndicho chama chenye rasilimali nyingi kuliko chama kingine chochote, hivyo kikiamua kujitegemea, ndicho chama pekee chenye uwezo huo wa kujitegemea, bila kutegemea ruzuku!.
Siri ya Utajiri wa CCM!
Utajiri na rasilimali za CCM ni michango ya lazima kwa Watanzania wote waliokichangia kwa michango ya lazima toka katika jasho lao katika kipindi chote cha miaka 30 ya utawala wa chama kimoja, na rasilimali zake karibu zote, zimetokana ama na michango ya lazima ya jasho la Watanzania wote, ama kupitia uporaji wa rasilimali za taifa ilizokuwa inajimegea kutoka serikalini ambazo ni mali halali za Watanzania.
Historia ya Ubinafsishaji!
Ubinafsishaji wa mabenki ulipoanzishwa nchini, wataalamu wa benki ya Dunia waliishauri serikali ya Tanzania, kwamba zoezi la ubinafsishaji kwa Tanzania, haliwezekani kwa sababu li benki la NBC ni kubwa mno na limetapakaa Tanzania nzima, hivyo ndilo lenye kuhodhi monopoly ya sekata ya mabenki nchini, hivyo hakuna benki nyingine yoyote inaweza kuja na kustawi Tanzania!. Hivyo wakashauri ili kuleta ushindani halali wa mabenki nchini, hili Li benki likubwa la NBC, kwanza lazima livunjwe, ligawanywe kwenye vibenki vidogo vidogo, na rasilimali zake ziuzwe ili benki za nje zije zilinunue ziweze kushindana, Mzee Ruksa alikuwa hana hiyana, akakubali, hivyo NBC ikavunjwa, na kuundwa NBC, NMB na CHC. Mwalimu Nyerere alishangaa na kukasirika sana na kiukweli hatua ilimtoa machozi, akaiandikia kitabu cha "Uongozi Wetu na Hatma ya Tanzania".
CCM ni Chama Dola, Utenganishaji wa Kofia Mbili ni Kiini Macho!
Tulivyoanzisha vyama vingi nchini, CCM kilikuwa chama Dola, ndicho kilichokuwa kimeshika hatamu za uongozi wa nchi, viongozi wote wa serikali walikuwa na kofia mbili za chama na serikali. Tulivyoanzisha vyama vingi, tukaondoa kofia mbili kule chini kote, kofia mbili zikabaki kwa Mwenyekiti tuu wa CCM, ndie rais wa nchi, lakini kwenye nafasi nyingine zote, watendaji wa CCM walivuliwa kofia moja, watu wakidhani huku ni kuwapunguzia mamlaka makada wa CCM serikalini, kumbe hawakujua, wateule wote walioteuliwa kwenye nyadhifa serikali ni makada wa CCM!. Hivyo CCM kuwa na nguvu zaidi, badala ya mtu mmoja kuwa na kofia mbili, sasa ni watu wawili!, ma RC, Ma DC, Spika, na watendaji wengine wote wakubwa wa serikalini ni makada!
Mali na Rasilimali za CCM ni Mali ya Umma, na Rasilimali za Umma
Wakati wote wa Chama kimoja, wafanyakazi wote wa nchi hii walikatwa michango ya lazima kukichangia Chama kana tunavyokatwa kodi kwa lazima. na kwa vile CCM ni chama dola, majengo, viwanja na maeneo inayomiliki na rasilimali mali ni mali za serikali ambazo ilijigawia kwa sababu CCM ilikuwa ndio serikali, huwezi kujiibia mwenwenyewe, mali ya serikali ni mali yako, hivyo CCM ilikuwa inajichukulia tuu mali zake.
Kama Ilivyo kwa NBC, Ilibidi Kwanza CCM Ivunjwe Ndipo Tuanze Mfumo wa Vyama Vingi
Ili kuleta ushindani halali wa vyama vyote, CCM ilibidi ivunjwe, rasilimali zake zichurudishwe serikalini, vyama vyote vianze moja from the scratch, lakini CCM kilianza hivyo hivyo na mali zake zote ilizo loot toka kwa Watanzania, hivyo kuwa ni chama kubwa tajiri, chenye nguvu ya pesa na rasilimali!, kuvishindanisha na vyama vidogo masikini, sio ushindani halali!. Niliwahi kushauri, siku ikitokea upinzani kuchukua nchi, kazi ya kwanza ni kuipurura CCM mali zote ilizo loot toka kwa Watanzania!.
Lengo la CCM Kujitegemea!
Uamuzi wa CCM kuamua kujitegemea, ukiuchukulia juu juu, ni jambo zuri!, lakini ukizama ndani deep inside, utagundua kuhusu the motive behind uamuzi huu!, utakubalia na mimi just to "fear the Greeks especially when they bring gifts!"
"ulterior motive behind" ya hatua hiyo, kwa CCM kuamua kujitegemea, could be, imegundua ruzuku ndio roho ya vyama vyote vya siasa vyenye nguvu!, kuna uwezekano mkubwa CCM ikapoteza wabunge wengi kwenye bunge lijalo, hivyo kupoteza kiwango kikubwa cha ruzuku!, hivyo sasa CCM inajiandaa kunyolewa!, wapinzani makini wote, watakapoliona hili dubwana kubwa lenye mali na lenye nguvi hivi kama CCM, tajiri kama CCM na rasilimali kama CCM, anajianda kunyolewa!, what about hivi vyama sisimizi?!.
Utegemezi wa Ruzuku!
Mpango wa kutoa ruzuku kwa vyama vya siasa, ulibuniwa ili kuinufaisha CCM!. CCM ndie mnufaika na mfaidika mkuu wa ruzuku, CCM ndie mtegemezi mkuu wa ruzuku, lakini vyama vingine vyote ni totally dependant on ruzuku!. Sasa inapotokea chama cha kijamaa kinachofaidi ruzuku, kujipanga kutotegemea tena ruzuku, hili likifanikiwa, kwa CCM kweli kujitegemea, na kuweza kujiendesha bila kutegemea ruzuku!, amini msiamini, huo ndio utakuwa mwisho wa ruzuku!. Nahisi kuna jambo la siri limejificha, usikute wamepanga CCM ikiisha jitegemea, then, zoezi ugawaji ruzuku kwa vyama vya siasa ndio litafikia mwisho, kwa vyama vyote sasa kutakiwa kujitegemea, na kwa vile vingi ya vyama vya upinzani ni vyama ruzuku, ruzuku ikikatwa, huenda huo ndio ukawa mwisho rasmi wa upinzani nchini!, hivyo hili nililowahi kulisema hapa chini kwenye rejea, huenda sasa ndilo linakwenda kutimizwa!.
Ushauri na Hitimisho
Kwa vile Tanzania ni nchi ya vyama vingi, na vyama hivyo vipo kwa mujibu wa katiba, then, uongozi wa chama chochote kilicho madarakani, una wajibu wa kuvilea vyama vingine na sio kuviangamiza.
Hivyo basi, Wale wote wenzangu na mimi, wenye matumaini na upinzani kuja kushika dola!, hii jamani kwa Tanzania ni ndoto ya mchana kweupe, ni bora muendelee kutumaini kwa kanuni ya "hope for the best!" but get prepared for the worst!".
Siku hizi, jambo likipangwa lisipotimia, linatimilizwa, na ili litimie kama kuna kitu kinapaswa kufanywa ili kitoshe, kisipotosha kinatosheshwa!. Kwa sasa tumshukuru sana Kikwete, ni mtu mwenye utu na aibu ya kuua upinzani wasiwazi, lakini siku za mbele, anaweza kutokea mtu katili asiye na huruma, akauua upinzani wazi wazi huku tukishuhudia.
CCM Hoyee!
NB. Hii ni opinion yangu!. Everybody has the right to his or her own opinion, wengine sisi tuoneni hivi hivi, tunaona mbali!, hivyo bandiko hili nitalitunza as a reference materials, siku ya siku likitimia, nitakumbusha.
Wasalaam
Paskali
PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!
CCM kutumia Hooks & Crooks Kushinda Chaguzi, Inajua Ikishindwa Ndio Itakufa Jumla, Itakubali?
Tuko Vitani Tuna Wapiganaji Shupavu, Wapiganaji Makini na Watazamaji, Je! Wewe Uko Kundi Gani ?
Watch TBC Live!. " William Malecela na Ndoto ya CCM Kutawala Miaka 50!.
"Ukiona mwenzako ananyolewa!"
na "Ukiona kwa mwenzako kuna ungua!, kwako kunateketea!"
Wale wote wenye matumaini na mategemeo kuwa kuna siku upinzani wa nchi hii, utakuja kushika dola!, hawa ni wishful thinkers na day dreamers, wanao ota ndoto za mchana, wasahau kabisa!.
Lengo la uzi huu ni kuwaanda kisaikolojia, wale wote wenye matumaini chanya, kuwa Tanzania ni nchi ya vyama vingi vya siasa, hivyo kuwa na mategemeo, kuna siku itafika, ambapo wapinzania pia watashika dola, na CCM itakuwa ni chama cha upinzani!, wasahau kabisa hili jambo, ili kuwazui kupata depression inayotokana na despair, kufuatia kuwa na too much great expectations kuwa kuna siku upinzani wa nchi hii, utakuja kushika dola!.
CCM inandaa kifo rasmi cha upinzani kwa dose za taratibu, na kuandaa kaburi la kuuzika jumla upinzani wa Tanzania!, na utauzika for good!.
Mkakati wenyewe uko hivi!
Miongoni mwa maazimio ya kikao cha NEC ya CCM kilichomalizika leo mjini Dodoma, kimeazimia CCM kuachana kabisa na kutegemea ruzuku, na badala yake CCM sasa kijigeuze kutoka chama cha kijamaa, kugeuka chama cha kibepari, kianze kufanya biashara kubwa kubwa kwa kuanzia na real estates, kizalishe fedha nyingi, kijitegemee, badala ya hali ilivyo sasa, kinajiendesha kwa kutegemea ruzuku!.
CCM Chama Kubwa! Chama Dola, Chama Tajiri!
Watu wote wanajua fika kuwa CCM ndio chama kikubwa kuliko vyote Tanzania!, licha ya kuwa ni chama dola, yaani ukizungumzia serikali ya Tanzania, unazungumzia CCM, yaani CCM ndio serikali ya Tanzania yenye jeshi, polisi, bunge na mahakama!, ndicho chama chenye wanachama wengi kuliko chama kingine chochote Tanzania!, ndicho chama tajiri, kuliko chama kingine chochote tanzania, na ndicho chama chenye rasilimali nyingi kuliko chama kingine chochote, hivyo kikiamua kujitegemea, ndicho chama pekee chenye uwezo huo wa kujitegemea, bila kutegemea ruzuku!.
Siri ya Utajiri wa CCM!
Utajiri na rasilimali za CCM ni michango ya lazima kwa Watanzania wote waliokichangia kwa michango ya lazima toka katika jasho lao katika kipindi chote cha miaka 30 ya utawala wa chama kimoja, na rasilimali zake karibu zote, zimetokana ama na michango ya lazima ya jasho la Watanzania wote, ama kupitia uporaji wa rasilimali za taifa ilizokuwa inajimegea kutoka serikalini ambazo ni mali halali za Watanzania.
Historia ya Ubinafsishaji!
Ubinafsishaji wa mabenki ulipoanzishwa nchini, wataalamu wa benki ya Dunia waliishauri serikali ya Tanzania, kwamba zoezi la ubinafsishaji kwa Tanzania, haliwezekani kwa sababu li benki la NBC ni kubwa mno na limetapakaa Tanzania nzima, hivyo ndilo lenye kuhodhi monopoly ya sekata ya mabenki nchini, hivyo hakuna benki nyingine yoyote inaweza kuja na kustawi Tanzania!. Hivyo wakashauri ili kuleta ushindani halali wa mabenki nchini, hili Li benki likubwa la NBC, kwanza lazima livunjwe, ligawanywe kwenye vibenki vidogo vidogo, na rasilimali zake ziuzwe ili benki za nje zije zilinunue ziweze kushindana, Mzee Ruksa alikuwa hana hiyana, akakubali, hivyo NBC ikavunjwa, na kuundwa NBC, NMB na CHC. Mwalimu Nyerere alishangaa na kukasirika sana na kiukweli hatua ilimtoa machozi, akaiandikia kitabu cha "Uongozi Wetu na Hatma ya Tanzania".
CCM ni Chama Dola, Utenganishaji wa Kofia Mbili ni Kiini Macho!
Tulivyoanzisha vyama vingi nchini, CCM kilikuwa chama Dola, ndicho kilichokuwa kimeshika hatamu za uongozi wa nchi, viongozi wote wa serikali walikuwa na kofia mbili za chama na serikali. Tulivyoanzisha vyama vingi, tukaondoa kofia mbili kule chini kote, kofia mbili zikabaki kwa Mwenyekiti tuu wa CCM, ndie rais wa nchi, lakini kwenye nafasi nyingine zote, watendaji wa CCM walivuliwa kofia moja, watu wakidhani huku ni kuwapunguzia mamlaka makada wa CCM serikalini, kumbe hawakujua, wateule wote walioteuliwa kwenye nyadhifa serikali ni makada wa CCM!. Hivyo CCM kuwa na nguvu zaidi, badala ya mtu mmoja kuwa na kofia mbili, sasa ni watu wawili!, ma RC, Ma DC, Spika, na watendaji wengine wote wakubwa wa serikalini ni makada!
Mali na Rasilimali za CCM ni Mali ya Umma, na Rasilimali za Umma
Wakati wote wa Chama kimoja, wafanyakazi wote wa nchi hii walikatwa michango ya lazima kukichangia Chama kana tunavyokatwa kodi kwa lazima. na kwa vile CCM ni chama dola, majengo, viwanja na maeneo inayomiliki na rasilimali mali ni mali za serikali ambazo ilijigawia kwa sababu CCM ilikuwa ndio serikali, huwezi kujiibia mwenwenyewe, mali ya serikali ni mali yako, hivyo CCM ilikuwa inajichukulia tuu mali zake.
Kama Ilivyo kwa NBC, Ilibidi Kwanza CCM Ivunjwe Ndipo Tuanze Mfumo wa Vyama Vingi
Ili kuleta ushindani halali wa vyama vyote, CCM ilibidi ivunjwe, rasilimali zake zichurudishwe serikalini, vyama vyote vianze moja from the scratch, lakini CCM kilianza hivyo hivyo na mali zake zote ilizo loot toka kwa Watanzania, hivyo kuwa ni chama kubwa tajiri, chenye nguvu ya pesa na rasilimali!, kuvishindanisha na vyama vidogo masikini, sio ushindani halali!. Niliwahi kushauri, siku ikitokea upinzani kuchukua nchi, kazi ya kwanza ni kuipurura CCM mali zote ilizo loot toka kwa Watanzania!.
Lengo la CCM Kujitegemea!
Uamuzi wa CCM kuamua kujitegemea, ukiuchukulia juu juu, ni jambo zuri!, lakini ukizama ndani deep inside, utagundua kuhusu the motive behind uamuzi huu!, utakubalia na mimi just to "fear the Greeks especially when they bring gifts!"
"ulterior motive behind" ya hatua hiyo, kwa CCM kuamua kujitegemea, could be, imegundua ruzuku ndio roho ya vyama vyote vya siasa vyenye nguvu!, kuna uwezekano mkubwa CCM ikapoteza wabunge wengi kwenye bunge lijalo, hivyo kupoteza kiwango kikubwa cha ruzuku!, hivyo sasa CCM inajiandaa kunyolewa!, wapinzani makini wote, watakapoliona hili dubwana kubwa lenye mali na lenye nguvi hivi kama CCM, tajiri kama CCM na rasilimali kama CCM, anajianda kunyolewa!, what about hivi vyama sisimizi?!.
Utegemezi wa Ruzuku!
Mpango wa kutoa ruzuku kwa vyama vya siasa, ulibuniwa ili kuinufaisha CCM!. CCM ndie mnufaika na mfaidika mkuu wa ruzuku, CCM ndie mtegemezi mkuu wa ruzuku, lakini vyama vingine vyote ni totally dependant on ruzuku!. Sasa inapotokea chama cha kijamaa kinachofaidi ruzuku, kujipanga kutotegemea tena ruzuku, hili likifanikiwa, kwa CCM kweli kujitegemea, na kuweza kujiendesha bila kutegemea ruzuku!, amini msiamini, huo ndio utakuwa mwisho wa ruzuku!. Nahisi kuna jambo la siri limejificha, usikute wamepanga CCM ikiisha jitegemea, then, zoezi ugawaji ruzuku kwa vyama vya siasa ndio litafikia mwisho, kwa vyama vyote sasa kutakiwa kujitegemea, na kwa vile vingi ya vyama vya upinzani ni vyama ruzuku, ruzuku ikikatwa, huenda huo ndio ukawa mwisho rasmi wa upinzani nchini!, hivyo hili nililowahi kulisema hapa chini kwenye rejea, huenda sasa ndilo linakwenda kutimizwa!.
Ushauri na Hitimisho
Kwa vile Tanzania ni nchi ya vyama vingi, na vyama hivyo vipo kwa mujibu wa katiba, then, uongozi wa chama chochote kilicho madarakani, una wajibu wa kuvilea vyama vingine na sio kuviangamiza.
Hivyo basi, Wale wote wenzangu na mimi, wenye matumaini na upinzani kuja kushika dola!, hii jamani kwa Tanzania ni ndoto ya mchana kweupe, ni bora muendelee kutumaini kwa kanuni ya "hope for the best!" but get prepared for the worst!".
Siku hizi, jambo likipangwa lisipotimia, linatimilizwa, na ili litimie kama kuna kitu kinapaswa kufanywa ili kitoshe, kisipotosha kinatosheshwa!. Kwa sasa tumshukuru sana Kikwete, ni mtu mwenye utu na aibu ya kuua upinzani wasiwazi, lakini siku za mbele, anaweza kutokea mtu katili asiye na huruma, akauua upinzani wazi wazi huku tukishuhudia.
CCM Hoyee!
NB. Hii ni opinion yangu!. Everybody has the right to his or her own opinion, wengine sisi tuoneni hivi hivi, tunaona mbali!, hivyo bandiko hili nitalitunza as a reference materials, siku ya siku likitimia, nitakumbusha.
Wasalaam
Paskali
PM, Hon. Mizengo Kayanza Peter Pinda; Sorry, You are very wrong!
CCM kutumia Hooks & Crooks Kushinda Chaguzi, Inajua Ikishindwa Ndio Itakufa Jumla, Itakubali?
Tuko Vitani Tuna Wapiganaji Shupavu, Wapiganaji Makini na Watazamaji, Je! Wewe Uko Kundi Gani ?
Watch TBC Live!. " William Malecela na Ndoto ya CCM Kutawala Miaka 50!.