Wenje tangu ahamie CCM amecharuka zaidi


Vituko vinaendelea huko Wenje anasema amepata wokovu CCM leo hii anaiponda CHADEMA eti ni hawana mipango wanashinda Mtandaoni kazi yao nge nge nge nge nge
Uchawa ni mbaya yaani kama vile siyo Wenje wa enzi zile
-----------
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Nyamagana kupitia CHADEMA, Ezekiah Wenje amesema amepata “wokovu mpya” baada ya kuachana na kile alichokiita “chama cha matusi, malalamiko na makasiriko” na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Wenje alitoa kauli hiyo leo, Oktoba 18, 2025, katika mkutano wa kampeni wa mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan uliofanyika mkoani Katavi, ambapo amesema umati mkubwa wa wananchi ulioshiriki ni ushahidi wa nguvu ya chama hicho tawala
Wenje amesema vyama vinavyoshinda mitandaoni havina mipango wala mikakati ya maendeleo, na badala yake vimekuwa vikijikita katika matusi na malalamiko. Ameongeza kuwa taifa linapaswa kutofautiana katika sera za maendeleo, lakini linapokuja suala la ulinzi, usalama na amani, hakuna mjadala
Akiendelea, Wenje ametaja kuwa baadhi ya viongozi wa upinzani wamekuwa wakitumia kigezo cha tume ya uchaguzi kulalamikia matokeo wanaposhindwa, jambo aliloliita ujinga


Vituko vinaendelea huko Wenje anasema amepata wokovu CCM leo hii anaiponda CHADEMA eti ni hawana mipango wanashinda Mtandaoni kazi yao nge nge nge nge nge
Uchawa ni mbaya yaani kama vile siyo Wenje wa enzi zile
-----------
Aliyewahi kuwa Mbunge wa Nyamagana kupitia CHADEMA, Ezekiah Wenje amesema amepata “wokovu mpya” baada ya kuachana na kile alichokiita “chama cha matusi, malalamiko na makasiriko” na kujiunga na Chama Cha Mapinduzi (CCM)
Wenje alitoa kauli hiyo leo, Oktoba 18, 2025, katika mkutano wa kampeni wa mgombea Urais wa Tanzania kupitia CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan uliofanyika mkoani Katavi, ambapo amesema umati mkubwa wa wananchi ulioshiriki ni ushahidi wa nguvu ya chama hicho tawala
Wenje amesema vyama vinavyoshinda mitandaoni havina mipango wala mikakati ya maendeleo, na badala yake vimekuwa vikijikita katika matusi na malalamiko. Ameongeza kuwa taifa linapaswa kutofautiana katika sera za maendeleo, lakini linapokuja suala la ulinzi, usalama na amani, hakuna mjadala
Akiendelea, Wenje ametaja kuwa baadhi ya viongozi wa upinzani wamekuwa wakitumia kigezo cha tume ya uchaguzi kulalamikia matokeo wanaposhindwa, jambo aliloliita ujinga