Habari wakuu,
Nimekuwa nikifuatilia mijadala mitandaoni, hasa kwenye Facebook, X na hapa JF, kuhusu sakata la Wachina kwenye biashara za rejareja.
Inaonekana wale ambao hawafanyi biashara au wanaoendesha biashara zisizotegemea uagizaji wa bidhaa kutoka nje ndio wanaoshabikia Wachina kuruhusiwa kuuza rejareja, eti kwa sababu bei zao ziko chini.
Hali hii inaua ajira nyingi kwa sababu maduka ya wenyeji yanashindwa kushindana. Mwisho wa siku, biashara za wazawa zinakufa, na uchumi unashikwa na wageni.
Hili si jambo la kawaida katika biashara. Hii ni mbinu ya predatory pricing, ambapo wanapunguza bei kupita kiasi ili kushinda ushindani, kisha baadaye, wakiwa wametawala soko, wanapandisha bei na kudhibiti uchumi.
Nimekuwa nikifuatilia mijadala mitandaoni, hasa kwenye Facebook, X na hapa JF, kuhusu sakata la Wachina kwenye biashara za rejareja.
Inaonekana wale ambao hawafanyi biashara au wanaoendesha biashara zisizotegemea uagizaji wa bidhaa kutoka nje ndio wanaoshabikia Wachina kuruhusiwa kuuza rejareja, eti kwa sababu bei zao ziko chini.
Sababu za Bei ya Mchina Kuwa Chini
- Wachina Wameshika Soko la Afrika
Wachina ndio wazalishaji wakuu wa bidhaa nyingi tunazoagiza barani Afrika. Wanamiliki viwanda na ndio wasambazaji wakuu wa bidhaa tunazouza. Lakini wanapokuja kuuza rejareja, wanavuruga mfumo wa biashara ambao umekuwepo kwa muda mrefu.- Mfumo wa biashara kawaida huwa na mlolongo huu:
Manufacturer → Supplier → Distributor → Wholesaler → Retailer - Mchina, akiwa Manufacturer au Supplier, anavunja mfumo huu kwa kuuza moja kwa moja kwa mlaji wa mwisho (Retail). Hii inaondoa nafasi ya distributor na wholesaler, hivyo faida ambayo ilipaswa kwenda kwao inabaki kwake, na hii inampa uwezo wa kuuza kwa bei ya chini zaidi.
- Mfumo wa biashara kawaida huwa na mlolongo huu:
Hali hii inaua ajira nyingi kwa sababu maduka ya wenyeji yanashindwa kushindana. Mwisho wa siku, biashara za wazawa zinakufa, na uchumi unashikwa na wageni.
- Wachina Wana Mkakati Maalum
Si Wachina wote wana viwanda au ni wasambazaji wakubwa. Wengi wao ni wafanyabiashara wa kawaida wenye mtaji, lakini wanafaidika na mitandao ya viwanda vyao vya nyumbani. Wanapata bidhaa kwa bei ya chini sana na wanauza kwa bei ya chini hapa kwetu ili kuteka soko.- Kwa nini wanauza bidhaa kwa faida ndogo sana hata kama wamesafirisha kwa muda mrefu?
- Kwa nini wanauza chini ya bei ya soko huku wakijua wameingia gharama za usafirishaji na ushuru?
Hili si jambo la kawaida katika biashara. Hii ni mbinu ya predatory pricing, ambapo wanapunguza bei kupita kiasi ili kushinda ushindani, kisha baadaye, wakiwa wametawala soko, wanapandisha bei na kudhibiti uchumi.
- Wahindi Vs Wachina
Wengine wanajitetea kuwa hata Wahindi wamekuwa kwenye biashara kwa muda mrefu. Lakini kuna tofauti kubwa:- Wahindi wanafuata mfumo wa biashara wa kawaida.
- Wahindi hawapunguzi bei kupindukia hadi washindani waanguke.
- Mfano: Tanga Anjari, Toptang Tomato, Seifi Plastics, Jambo Houseware—hawa wote hawavunji mfumo wa biashara, na mara nyingi hata wanauza kwa bei ya juu zaidi kwa sababu wanawaheshimu wasambazaji wao.
- Kodi na Gharama za Biashara
Mfanyabiashara wa kawaida anapoagiza bidhaa kutoka China, anapitia gharama nyingi—ushuru bandarini, VAT, na muda wa usafirishaji. Lakini mchina mwenyewe anapouza bidhaa hizo hapa, bado anaweza kuuza kwa bei ya chini zaidi ya mwenyeji. Inawezekanaje?
Suluhisho
Tunahitaji kulinda biashara za wazawa kwa kuhakikisha:- Wachina hawauzi bidhaa rejareja moja kwa moja kwa mlaji wa mwisho.
- Bei zao zinafuata viwango vya soko na haziwezi kupunguzwa kupita kiasi ili kuua ushindani.
- Mfumo wa biashara unaheshimiwa—wafanyabiashara wa ndani wanapaswa kuwa na nafasi ya kusambaza na kuuza bidhaa.