Weekend story: Bad wives

Weekend story: Bad wives

Amar! My Story.

I always wanted to something with my life, bigger than life itself. Since i was aboy i always saw the bigger picture. I started stealing by the age of five. It just felt right. Kwenu naweza kuonekana gaidi, bandidu mtu mubayaaa, ila mimi ni mtu kama nyie na nina sababu zangu za msingi kabisaa. Nilipokuwa naiba mama alikuwa ananimbia Mungu hapendi, ni dhambi and so on.

Wanasema Baba ni Mungu wako wa 2 duniani, ndio Mungu unaemuona, na baba yangu alinikataaa kata kata. At first i just couldnt accept the fact that my dada doesnt want me. WHY was baically the main question. Nikasema labda mama limuuzi na alimkosea sanaaa. Kwa jitihada zangu nikiwa primary nilimchimba bibi, pasipo kutaka sababu kila siku ieandayo wa Mungu nilikuwa namuuliza baba yngu ni nani, bibi jibu lake likawa moja, baba ako firauniii mjkuu wangu, hastahili hata tone la akili yako, yule alikojoa mbegu tu, bibi yangu ni mzaramo mumsamehe bureee.

Siku bibi akachoka akasema twende ukamuone firauni ambae ni baba yako, labda ukiona firauni kiasi gani utapata akili ya kuangalia maisha yako, usikae kabisaa hata sekunde ukawza una baba,sijui aakusaidia ule mfano wa baba tu, wala baba huna paleeeee. Bibi akanikokota mpaka kwenye ofisi moja ya bank, akasema ngoja hapa. Baadae akatoka mbaba, nilivomuona tu nilimjua maana tumefanana sana akamuila Julius. Julius kutuona akawa kama kaona kitu cha kumchefuaaa na kumuondoa mood.

Bibi akamfata akamsalimia shikamoo. Bibi akajikausha, akamwambia mwanao alikuwa anakuulizia baba yake, sasa sijataka kukufanyia uchuro umekufa, japo matendo yako na mfu hayana tofauti kabisaaa, nimeleta maana sie tukikuteta ananuna anatuona wangu tu, hatukupendi, nimemlet akuone mwenyewe ulivo firauni, ila akae akijua hana baba wal mfano wa baba. Julius akakasirikaa, sikia wewe bibi nikwambie kwa mara ingine, mimi sio baba wa mtoto huyo, kaka na mama yake akuoneshe baba yake, ila mimi sio, mbona unataka kuniharibia ndoa yangu? Muulize mwanao vizuri, dogo mimi sio baba yako, wanakupotezaaa. Akaondoka.

Tangu siku hio sikuwahi kumuulizia baba yangu tenaaa. Sasa Mungu wangu naemuona ndo alinitenda hivo, put your self in my shoes, my second god wants nothing to do me, absolutely nothing, ist because i have done something to him, no, he just dont like me, it made me loose faith on my bigger father Sr. God. I just concluded i dont have any fatherim just on my own.

Growing up withou a father nad mather wasnt easy, mama aliolewa tena, and she too didnt want me, anasingizia mume wangu hatakiii kabisaa huyu mtoto tukae nae. Pale kwa bibi palikuwa pagumu manake bibi ana watoto wngine mama zangu adogo wana watoto ao, wamezaa pale pale kwa bibi na wapo, so kila mtu anaangalia wanae mimi sina wa kuniangalia, bibi mzee mpaka aje anikumbuke jioni sanaa. Wale mama wadogo wananunua chips wanakula na wanao, au sikukuu wananunua nguo za watoto wao mi nabakia hivo hivo, labda bibi akiona vipi ndo afanye manuvaa. Kula chakula bila nyama ilikuwa kawaida manake mpaka kila mtu ampakulie mwanae nyama zimeishaaa. I jus grew up knowing i am on my own. Nikizubaaa napotea.

Mjomba wangu Mungu amuweke pema peponi, alinipeleka English Medium, akanimbia uncle mimi nikiwepo utasomaa mpaka ufike mwishoo, maka unambie uncle mi basi shule, nita fight usiku na mchana. Uncle alikuwa konda wa magari ya mikoani. Hakuwa na uwezo ilaalion umuhimu wa elimu. Ananimbia uncle wangu wewe kama mimi, ni kama tu yatima, wazazi wote hawakutaki, usiposoma huko mbele kugumu, utapoteaaa. Mi nitakusomesha uncle, kwanza baba yako mwenyewe japo hakutaki msomiyulee, darasa kaenda za kutosha, babu yako kwanza professor, shule itakukubali mi nakwambia.

Mamdogo kama wanga wacha watake ile chance apewe watoto wao, uncle akakomaa nyie akili hamna, mmezaa na wabeba mizigo, sijui ma dj hao watoto akili watatoa wapi. Si baba zao wapo wawalipie. Shule kiukweli nilikuwa nakuwa wa 1 kila siku, not that i ws bright, ilikuwa ukiwa wa 1 ada ulipi, sasa ikawa inanilazimu niwe wa 1 ili uncle kumpunguzia mzigo, mara chache nilikuwa nikiwa wa 2 uncle ananipa moyo,ila mwenywe najistukia asije kunichokaaa. Wakati uncle yupo kidogo hela ya shule , uniform, sikosi kabisaa, hata wenzangu haakujua home pagumu wala nini, mpaka school bus ananilipia fresh.

Darasa la 4, uncle alipata ajali, gari yao ikapindukaaa akakatika mguu, akaugua sanaa, akawa tu yupo home hana issue, amelost, ananimbia uncle Mungu hakupendaaa, uncle wako nimelost. Miasha yakawa magumu sanaaa. Nauli ikawa ishu. Na uncle alikuwa kama ndo anasimamia show pale kwa bibi, sasa alivokuwa alosto, mguu ana, anashinda kijiweni anavuta tu bangi, kulaviroba na kuangalia porno, maisha yaliyumba sanaaa, sanaaa. Kuna wiki sikwenda shule wiki nzima nauli hamna.Bibi akakereka akaniambia beba begi lako, we si una mama, twende huko huko.

Tumefika kwa maza, ushuani, maza anaishi nyumba nzima,kuna geti, tiles, kama hotel, akaniambia mi naenda, akija mama yako, mwambie bibi kasema kachokaaa na yeye anapumzikaaa ukae huku huku. Nikawa nimekaa nje barazani. Badae akaja mtoto na school bus kama darsa la 1 ananiuliza who are you? nakajibu. Kananiambia njoo ndani. Nikasita. Baadae namwambia dada, you are very bad kwanini humpi kaka chakulaaa. Dada wa kazi akaniletea nje.

Mama kuja dada kamuwahi nje, bibi kamleta mtoto anasema mwanao, kachoka yeye, mama kuja mbio kuniuliza imekuwaje? Basi ndo kuchukua hela ndani kunipa usiku huo huo kaniitia taxi nirudi kwa bibi, akanipa namba hela ikiisha tuma sms humu nitamtumia bibi akupe. Hapa hutakiwi kukutwa na mume wangu, itakuwa sooo. Ndo ikawa nafuuu, natuma tu sms huku hela imeisha. Hela ya ada, wakati ada silipi nampa uncle naona namsaidia kumbe ndo anazidi kunywea viroba tu.

Nikiwa darasa la 6, akiwa kalewa akagongwa na gari na kufariki dunia hapo hapo. I never felt alone in this worldkama siku hio. Japo uncle maisha yalikuwa yashamla Tigo kimtindo ila uwepo wake ulikuwa wa maana sana, he was the father that i didnt have. Sema sasa ndo bad father. Kuna siku nilipigwa shule, akanipa kisu, wakikupiga tena choma wote visuuu, choma usiwaze, dunia hii ukilegea unapotea. Uncle anakaa vijiweni na mimi naka nae, sasa story za kutukuza umalaya, wanawake, pombe na wizi zilinikolea sanasanaaa. Nikawa na uncle kitu kimoja. Bibi anapiga yowe unamuharibu huyo mtoto, uncle anamjubu mnataka ashinde na nyie wanwake awe shoga? Huyu anatakiwa akae na sisi wanaume awe dume la mbegu. Hahahaaaa.

Kijiweni wenywe walianza kunikubali kuwa dogooo, hatariiii. Sasa na mimi kutaka sifa nazidisha sasa, kuwa mkoraa mkora kweliii. Wakifanya matukio mi ndo mchora ramaniiii,na hivi nacheki muvi,nasoma vitabu watanipatia wapi. By the time niko darasa la 5 nikaanza kusimamia show kwa bibi, bibi anajua hela napewa na mama, kumbe nipo kwenye michongo ya wizi huko, ukabaji, uporaji.

Uzuri ncle aliniruhusu kutumia pombe tu, vilevi vingine alinikataza kabisaaa. Baada ya uncle kufariki kijiweni wakanichenjia wewe dogo bwana Uncle wako alikuwa anakutakia mambo makubwaa, alikuwa na mipango mikubwa na wewe sanaa. Alitaka usome darasa uwe boss kitambi meneja. Sasa sababu alikuwa mtu wetu sanaaa, tumona tumsaidie kutimiza matkwa yake ya mwisho. Ambayo ni kukusaidia wewe usome ufike mbali. Uhuni, wizi, ulevi marufukuuu. Tukikukamamta ni kichapo tuuu. Vijiwe marufukuuu. Hata uende kijiw cha mbagala ujue hatutajua tutajua na tutakuchenjia. Hapa hutakiwi kabisaaaa. Unachoruhusiwa ni kuwa malya tani yako, tembea na mtaa mzima, temba na mama zako, bibi zako huo ndo uanaume. Ila wizi, uhuni utaishia jela afuuncle wako alivokuwa mkorofi yule atajia ndotoni na mibakoraaa, atatucharazajeee sasa na hivi mzimu, anaweza hata akawaanatucharaza mchana kweupee. Hahaaaaaaaa! Bora mizimu mingine inangoja giza ndo ifanye yao, yule hata asubuhi akikumbuka ufirauni tulioufanya anatembeza bakora tu. Haahaaaaa!

Sikukaa tena kijiweni ila sio kwamba wizi nilicha, wizi kama kawaida. Niliacha kuwa front maana wale washkaji za uncle waliniwekea rada, wakanichimba mkwara ukiiba tunakupeleka wenyewe polisi, ikabidi nikae kwenye sekta ya udalali wa mali zilizoibiwa. Na hivi shule niko na wakishua, hela ilikuwa wazi. Mali ikiibiwa napewa kwa siri ili wale wanga wasijue, nami nawaonesha wanafunzi wenzangu wanawaambia uncle zao, na wengine mambo yanakuwa level.

Kuna siku ililetwa simu, nikataka kuipasisha kwa uncle wa rafiki yangu, kumbe huyo uncle anamjua alie ibiwa ile simu bwanaa. Wkaja huyu uncle wake na dogo. Nikawaambia kama vipi nyie nedeni polisi. Uncle akasema siis hatuendi polisi ila tunataka mgao ikiuzwa. Mi kuinunua siwezi maana mwenyewe ataniona nayo, ila ikiuzwa nipozwee. Nikamwambia hayo ndo maneno ya nyie watoto wa kiume kuongeaaaa, sio kushobokaa. Ikiuzwa utapata mgao. Ikauzwa nikawapooza soo likapitwa.

Siku nikaletewa simu imepigwa psota huko, kuikagua simu ya baba yangu wa kambo. Na kilichonijulisha yule dogo mtoto wa mama alikuwa screen saver. Nikaipitisha ukaguzi, kumbe baba firauni tu na yeye ana wanawake kibao, nikatami zile meseji nizitue kwa mama, anu nimpelekeesimu nzima, nikawaza tu dogo yule damu yangu ujue, afu kalelewa kimayai mayai, afu mtoto wa kike, kitaa hatodumu siku 2. Nikamee tu maana nikajua nikikiwasha tu kule dogo atajikuta kwa bibi na bi mkubwa mtu wa kuolewa tena tu. Na simu nikaiuza hela nzuri tu.

Japo simu ndo ilikuwa biashara yangu kubwa ila dhahabu nazo zilikuwa dili zangu, saa, na mambo kama hayo ya wakabaji. Bibi niliwahi kumpa jikufu la gram 250, alnalipenda mpaka kesho, kufu lisipoonekana hakulaliki mule ndani kabisaaaaa. Mama zangu wadogo nilikuwa siwapendi natoa mswaki tu, hata waniagize nini sitoiii. Bibi akaniona mimi tegemezi eti mda mwingine watu wanataka hela anasema mngojeni Amar arudi, Amar mwenyewedarasa la 7 jamaniiii. Kuna muuza Unga lishoboka kutaka kuniingiza kwenye u pusha, habari zikafika kijiweni, Pusha alijuuta, alichomewa moto kijiwe chake, gheto na nyumba yao ya urithi. Akaambiwa hio rasha rasha tu ajaribu tena ndo atawajua wao kina nani. Pusha alihama mtaa kabisaa na hajawahi kuonekana tenaaa. Tangu hapo watu wakaanza kuniogopa kabisaaa.


Wanawake nilianza nao tangu na balehe, huenda kabl hata sijabalehe kwenye baba na mama nimefunua sanaa wadada. Kwanza nilikuwa na hela, afu kikristo kinapanda, na mtu wa swagga sanaa sasa nakosaje wanawake kwa mfano, uswaiz hali ilivo ngumu. Soda tu unamla mke wa mtu. Nasikitika sikupata mfano wa kuheshimu wanawake, au sijui nimerithi mzee wangu maana vya kurithi vinazidi, mama wadogo nao walikuwa chupi mkononi sanaa, ukipa chocho hili lazima umkute huyu na bwana huyu leo, yule kesho hawasomeki kabisaa.

Nimemaliza msingi nikaingia secondary Azania, Aza boy, sikutaka boarding kusudi biashara yangu si mnajua tena. Nimefanya umalaya sanaa form 1 mpaka basiii. Manake hela ninayo, miziki naijuaaa pombe nakunywa, pamba napiga, simu nabadili kama nguo, yani nilionekana wa kishua hatariiii.

Sijui ilikuwaje ila nilikuwa na mkono wa kupiga wanawake. Demu akinizingua nampa kichapo cha uhakika.Sasa nilikua moraaa. Before i know it mademu wote hawanitakiii, washanijua sio, kwanza kitombiii, afu natembeza u Francis Cheka wa hatariii kwa Mademu. I jsut didnt know how to treat women. Dont blame me, given nimekulia kijiweni what could you expect.

Ilifika mahala nikienda na emu kwa bibi, bibi anamwambia utapigwaaaa, utakungutwaaa, huyu mara huyu japo mjukuu wangu ila sio mtuuuu, mi nakwambia binti, bora uondoke usije tenaa, huyooo mbwa tuu. Deu anatoka relay hana hamu. Baadae namchenjia bibi ile ile namwambia kwanza wewe bibi utakuwa mwangaa wewe si bure, mtu gani umezeeka hufi, mchawi wewe nakwambia, nae ananipa vyangu ningekuwa mwanga si ningekula nyama tangu mdogo, wazazi wako wamekutupa hapa na kwashiakor, umekondeanaa, nakupangua mavi, na kupambana uwe mtu leo hii umeota vuzi unaniita mimi mwanga? Ndo malaya kama baba yako, Mi nakwambia hio damu yenu ya vampayaa sio baba wala mtoto. Tunapeana kavu na bibi naingi gheto. Dakika 10 nyingi,Amara baba yangu umelala, si unajua nakupenda sana mjukuuwangu, fanya mpango wa mboga basi. Ndo kesi imeishaaa. Nikileta demu mwingine kama kawaida yake lazima aniwangie tenaaa. Nammind namwambia bibi wakati unakitembeza umezaa watoto baba mbalimbali mbona nilikuwa sikuingiliii lakini kwenye mishe zako, mbona hivo bibi unakuwa hunipendi. Anajitetea mimi nimeolewa ndoa 5 nazote nimezaa, sina mwanaharamu hata mmoja. Wew unavofanya dini haitakiii. Japo msikiti umeuasi ila haitakiw tukuendekezeee, we umlaya fanyia mbali ukijaribu humu lazima nikuingilie kwenye anga zakooo na kukuharibiaaa. Mwisho nikaacha kupeleka mademu home nikaona isiwe tabu lodge si zipo.


ITAENDELEA SAA 6 USIKU HUU.
 
The source! (Sidney)

Nikaja kuzinduka namkuta Amar yuko na HG, na Dr, na Nesi. Nikasema kwanza nisifumbue macho nisikie wanachoongea. Dr. anasema there si nothing we can do, absolutely nothing, huyu ana matatizo kuyabaini yanahitaji equipments ambazo za gharama mnoo zinapatikana hospitali tuuuu. Mimi bila vifaa siwezi kumsaidia. Amar anamwambia money is not an issue kabisaaa, do anything i can pay. Myahudi anakomaa there is nothing i can do.

Baadae akaja mume wa HG, mzungu kabisaa kabisaa blonde hair, analalamika please can you gt these illegal immigrants out of our home. Anaongea shit kinomaa. HG anamwambia she is my siste, mumewe anasema you jsut have brothers you dont have a sister, comming from the same palce doesnt make you sisters. Too many negros in my home, and the worst part they dont have papers, before i know it coke will be sold from my home. If they dont leave by evening i swear i am calling the Pollice on them myself.

Akatoka na HG wanabishana kwa sauti kubwa sio kidogooo. Nikafungua macho, Amar akaniuliza unajisikiaje, nikamwambia nakufaaa. Tuondokee hapa, Tusimletee HG matatizo. Take me home, i dont wanna die alone in this country, take me home please. Akaniambia ngoja tuondoke hapa nitajua cha kufanya. By then niko kilo 5, nimekakukaaa,mdhaifuuu Bongo lazima wangesema nina UKIMWI.

Akanibeba, tukapita sebuleni na kuwakuta HG na Mzungu wake. Yule Mzungu analeta kwere, where do you think you are taking her, you are trying to kill her or something? Mzungu nae haeleweki si alisema anatuitia polisi jamaniii. Mmmmmmh! Amara akamwmbia we si umesema unatuitia polisi, haya tunaondokaa. Muzngu mzungu tu siku zote wana roho nzuri sanaa wale watu mda mwingine. Anauliza sasa, where are you gonna go, with such a sick person without papers, i dont want you out but i am just confused, i might have said some rude things but i dont mean them, you have to stay here till she gets better then you can leave. Yuko serious kabisaaa.

Sasa sijui alitaka kutufanyia roho mbaya ila roho mbaya haiweziii, sijuiiii, ila akakomaa hamna kuondoka mtu pale, kamaAmar anaenda, aende ila mgonjwa anabaki. Mmmmh! Amar akamchana huyu mgonjwa tangu aje hapa unamuita nigger na illegal immirant, japo nchi yenu sawa au ya kaka zenu ila na sisi watu pia kama nyie. Sasa nasema pisha niondoke nae mbakie na nyumba yenu. HG yuko upande wa mumewe nibakie. Ikawa zogo mzungu hataki nitoke kabisaaa. Anamwambia Amar ukitoka tu nje nakuitia polisi huyu mgonjwa haendi kokote, where where you mpaka anaachwa park ajifie. Amar akatoa bastola. Wakatulia kwanza wote. Trust Amar being involved in crime, kama nilivojua huku USA lazima atakuwa kwenye magendo kama kawaida yake. Mzungu akatulia, Amara akmwambia polisi wakitufata nitakurudia na utanijua, asante sana Anna kwa msaada wako, wabongo huku nje tupendane.

He jsut drove for hours, njiani anasimama tu kunipa chakula na maji. He drove for hours and hours. Kuja kustuka nipo kwenye nyumba nzuri tu nikawa nasikia anaongea na wa Columbia kuwa lazima aondoke, demu wake anaumwa sanaa, anamrudisha kwao kwanza afu yeye atarudi waendelee na business. Wa Columbia hawataki aondokee wanamwambia ukitoka US kurudi tena ni impossible hasa kwa yeye alie overstay. Basi wanasema kama issue ni hospital basi nipelekwe Columbia au popote watalipa Ila Amar abakie aendelee na kazi. Ikawa ubishani mkubwaa. Mmmoja akasema anamjua Mjamaica ana vuduuu spell zinatibu mpaka cancer, hawezi kushindwa na kiugonjwa hiko. Amar akakubali mzee wa Vudu aletwe. Nikawa napoteza sasa network nikazimiaaa.

Kuja kustukaa kuna bibi mzee wa kijamaicaa ananihudumia, ananinywesha portion sijui nini ila mavitu mesuiiii mabayaaaa. Sikutaka kunywa ila nguvu ya kupambana sikuwa nayo. Baadae aaniwekea beseni, nikatapikaaaa, nikatapikaa nywele kabisaaa unazionaaa. Zinatoka vifundooo fundooo. Amar akastukaaa. What is this? Bibi ana mwambia in hospital they call this Tuberculosis (TB), alifnya kazi za nywele sanaa bila mask. Hata hivo huyu ana matizo mengi, hata alivokuwa mdogo aliumwaa sanaa, na aliponea herbs.Her body is just weak, she was born weak. Mwingine nywele angezio toa kwa excreation ila yeye zilijaa kwenye mapafu, pia kuna semehmu amevilia damu, na figo zake haziko vizuri. Ila her will to leave is so strong angekuwa mwingine angekufa.

Nilitapika nywele siku 3, baadae akasema nywele zimeishaa, ila nina mawe kwenye figo akawa ananipa dawa za kusaga yale mawe ili niyakojoe. Basi naumia nikikojoaa, anahesabu jiwe 1, la pili mpaka siku akasema hilo la mwisho na sikuumia tena nilipokojoa. Basi hio lishe yake utajuta ana blend mboga mbichi nakunywaa, nyma anachemsha kidogo nutrients, yaani alinilisha mpaka mijusi madai dawa. anaichemsha maji nakunywa. Konokono anawatoa ule utelezi nao dawa. Nikaanza kurudi afya yangu sasa. Haaaaa! Utanijuaaa. Mpaka nikapona kabisaa siumwi kituuu. Akamwamba asifanye kazi huyu hata miaka mi 2 mwili umeji strain sanaa huu. Alilipwa hela ndefu.

Nilivopona nikawa nakaa tu nyumbani na Amar tena, maisha mazuri, mpaka nina maid wa kufanya usafi, nikitaka kutengeneza nywele namuita professional ananitengeneza nyumbani, kucha, yani American dream ndo hio nilikuwa naionja. Kama unajiuliza Amar alikuwa anafanya kazi gani kama kawaida kusikia wa Colombia huo Unga tu.

Ila yeye alikuwa kitengo cha INTENATIONAL MARKETS. Kazi yake kubwa kutafuta masoko ya Coccaine na Heroine Dubai, Muscut, New Dehli, Bangkok. Aliakabidhiwa masoko ya Assia. Sababu asia kulikuwa kumeshdnikanaa kabisaa maana wenyewe wanalima huo ungaa tena umejaaa, na wa colombia wanataka wapeleke na soko la huko maana soko la ulaya na marekani wanalo ila halitoshi.

Amar kwa manuva yake, akaanza kutafuta masoko Africa, si anajua unga deal, anatafuta wateja online. AKawa anapata ila casualities zikawa nyingi unga haufiki, route ndefu sanaaa. Unga unaokamatwa mwingi. Afu mapunda wakitoka Colombia wanakaguliwa sana afu ndege za ku connect ni nyingi sana.

Amar akashauri wakalime Pakistan, watengeneze brand yao n kupack huko huko Pakistan itakuwa rahisi ku penetrate Asia na Africa. Akasema unga wa Asia hauna ubora, so wakiuza kwa kukomaa na bei watapotea wapeleke kitu chenyewe kile pure colombian, wakilime kule kule. Boss wao akamkubli dogo ana vision kubwa. Na kweli mmbo yalivoenda yakawa bam bam. Amar tenaaa, kma yuko nyumbani. Designer bag gani sikubeba? Mpaka karatasi nilipewa, chezea cartel.

Nikawa nakumbuka siku ya kwanza kukutana na Amar, wala sikudhania tungefika huku kote. Siku nakutana na Amar ilikuwa kama Mungu tu, manake sijui alitoke wapi ila alinifaa kinomaa.

Kulikuwa na mpira wa kirafiki, shule yetu na shule ingine wala sio ya kina Amar. Kipindi hiko Phesto ndo ananifatilia kinomaaa. Yani hataki hata kuelewa. Phesto aliwahi kuwa bwana wa shoga ake Rahma yule aliekuwa analiwa Tigo. Sasa kama Phesto au mwingine ndo alimfanyia vile sikuwahi kujua kwa uhaki, ila i was not going to take chances, Nikagomaaa kutoka nae. Sasa yeye mbabe hatari. Nilivomkataa akaniweka WANTED.

Nikawa naishi kama digi digi, siku hio ya mechi alishatangaza ananikungutaa. Na alivokuwa baunsa anabeba vyuma kila mtu anamuogopa. Mpira umeisha imekaa uwanjani mpaka mwisho kabisaa naogopa kutoka nitapigwa. Mwisho giza likaanza nikajua keshaondoka bwana, ile natoka tu akanikwidaaa. Mtama chini. Yaani sikuwahi kupigwaaa, kchapo kilinikolea. Niko chii ananifumua mateke sio ya kitoto. Watu wanamwambia muachee utamuua, utamuua, ndo kwanza ananipigaa mateke imagine. Walimu washaondoka. Kila mtu anamuogopaaa.

Nikijua sasa nakufa akatoke mkaka akamwambia mwache huyu dada, we choko nini unapigaje mademu? Demu hapigwi mateke anapigwa vibao tu, tena vya kishkaji. Phesto alivo baunsa akaanza kumpiga yule kaka, kaa akanza kupigwa, mara akatoa kisu. Phesto akakimbia akmwambia huyu niko nae shule moja ugomvi huu haujaisha.

Mi ndo kujizoa, ananiuliza umemfnya nini yule, na nyie dada zangu mjihurumie we kimwili huko ukatembee na yule baunsa kweli, haya nenda kwenu. Nishamtimua hatokuchokoza tena. Namwambia we humjui yul, namjua mimi, yani hapo ndo umemtia ndimu. Akasema mtajuana wenyewe. Akaondoka. i nikawa namfata nyuma nyuma. Anarudi ananifokea nenda kwenu bwanaaa, sasa utanifata mpaka wapi? Mi nina mishe za hela utaniharibiaaa, usnifanye kujutia kukusaidia. We nenda kwenu yule harud tenaa. Mi namfata tu nyuma nyuma nahisi Phesto yuko kona inayofata. Akchukia mpaka kunifokea are you dumb or something? Nimekwamba usinafate, sasa nitakukunguta mwenyee, nitakutia mambata sasa hivi. Mmmh! Nikawa na mashaka nikakaa chini tu pale pale. Akaondoka katokomea mi bado nimekaa. Sijui hata nilikuwa nawaza nini. Akarudi hivi wewe una akili nzuri kweli? Utakaa hapo mpaka saa ngapi? Ndo tatizo la kutoa msaada, utakuwinda lazimaaa. Twende nikupeleke kwenu. Nikamuelekeza kwetu tukawa tunaend akimya kimya, tumepanda haice kimy kimya, mi niko mbele yeye yuko nyuma. Nikafika home, nikaingia ndani, nikajua ladba ataondoka, kumbe kaenda mbele kawakuta wamama wamekaa kawauliza yule msichana mama ake nani, niitieni. Kamwambia kila kitu, Kuna mtu anaitwa Phesto, kampiga sanaa, tena mpeleke hospital na kakinukishe shule. Yani CD yote kaimimina afu kaondoka.

Maza kunibana ikabidi niseme, asubuhi kaja kunya shuleee, kaharishaa kweli kweli mpaka wazazi wa Phesto wameitwaaa, ilikuwa kesi kubwa sanaa. Phesto kapewa suspension. Sijui kiranga gani kikanifanya nimfate Azaniatena madai naenda kumshukuru. Jina simjui, ila walimjua nilivosema anatembea na kisu, wakasema huyo laima ni Man Amar, Nikatafutiwa akashangaa alijua labda mteja. Aaniuliza unataka nini, nikamwambia nimekuja kukushukuru, akasonyaa, umekuja kunishukuru unajua Phesto atakurudia na jeshi ndo unaomba ulinzi, wanawake na nyie. Utanipa nini mpaka nikupe escort? Kwanza mtu mwenyewe mbaya sanaa sio type yangu kabisaa, mi nakula mademu visuuuuuu. We nenda shukrani zako nimezipata. Ukiwapata mademu wakali huko shuleni kwenu nilegeshee utakuwa umenishukuru sio kitoto, sema nini nyie shule yenu ya kishua mademu drama nyingi. Au chukua hiki hapa kisu akij Phesto mchome cha korodani atakujua we nani. Na nilivokuwa zombi nikapokea kile kisu.

Sikwenda tena kumtafuta Amar wala Phesto alivorudi akunifata hata kidogo, jpo kisu kilikuwa standby kina mngoja. Siku moja kama mweiz tangia Phesto arudi, natoka shule Amar huyu hapa yuko na jeshi la watoto wa Azania, wamebeba mawe a visu sio vya kitoto. Hali ikawa tete. Akanimbia nooo njoo we binti umenigharimu sanaaa, yule boya wako jana na wenziewamenizunguka wakanipiga walikuwa wa 5, na kisu changu siku nacho nilikuhonga kimakosa, sasa leonataka nimundishe adabuuuu. Mimi ndio Amar, kubwa la Maadui. Kukusaidia tu ndo kanipiga sasa nakumbatooo live tuone atanifanya nini.

Mi nikawa nimesimama tu pale kam jinga. Amara akaniambia kesho unatakiw ujeAzania pale mchana, sawa mama, usinifanyenikufate hukuuu, utajutaaa,Phesto kwangu anakaaa. Najua nikiw na wewe Phesto lazima anifate mwenyewe na akinifata mwenyewe ndo nitamfurahisha na kumfunza adabu. Phesto hakutoka, mpaka polisi wakaja, kina Amar wakakimbia, na Phsto shule alihama hakuja tenaaa.

Mchana nikaenda ku report for duty, what choice did i have? Kuniona ndo umekuja, hivi wewe kweli una akili vizuri? Ndo ukaja kweli? Anyway nahitaji secetary itabidi uwesecretary wangu,ila ukilogwa mambo yangu ukayatangaza utajutaa kunifahamu sawaaa. Kazi yako unafanya nachokutuma sawa. Mi najibu sawa. Pamoja na kutokuwa na choice il pi nilikuwa sijui nimempenda, sijui woga tuu sijui, ila moyoni nilikuwa tayari kufanya anachonituma.

Kazi yangu siku hio nilitumwa kupeleka hela na barua na kumtongozea dada mmoja wa mzizima. Ananiambia watu wanga sanaa wananiharibia kishenzi, kama watu washaniwangia wamemwambia mambo ya uongo uongo sijui mi malaya sijui napiga wanawakewewe ndo kazi yako kumshawishi anikubali sawa. Umuelezee nilikuokoa mimi mtu mzuri sanaaa, si etiii. We wanamke mwenzie atakuelewa. Nikakubali ile kazi.

Kazi ikanishinda kabisaa, dada hatakii hatakiii. Akanimind kinoma Amar. Akanituma kwa wadada kama wa 2 nikashindwa kote. Akaniambia we kazi ya kutongoza huiwezi ishakushinda. Akanipa kazi ya kudeliver simu za wizi. Akitokea mteja mi ndo nampelekeaa. Siku nikadakwa nikapelekwa polisi, chupi ilinibanaaa. Simu Motorola walimuibia mtu huyohuyo na kumuuzia mu huyo huyo bila kujijua. Akanidakaaa. Amar kusikia nimedakwa akaja kunitoa ndani.

Nilivokaa nae nikawa nimemzoea tunaongea kabisaa, akaniuliza wembona huna bwana? Ina maana ulikuwa na bwana mmoja yule Phesto hahaaaaa! Nikamambia mi bwana naempenda hanipendi. I dont know why ila alihisi mi nampenda yeye. And he just wanted me to say it out loud. Akanichimba daah sijui nikusaidiaje. Nikamwambia unaweza kunitongozea lakini, you know pict it to him iwe kama idea yake. Akastukaa hivi kweli kuna bwana unampenda seriously? Nani kwanza?

Nikamjibu Joey. Tuko nae shule yuko Form 4. Akabadilika hivi umeniona mimi bwabwa kabisaa nimtongozee mwanaume mwenzangu demu, atanionae, watu wakisikia watanionaje? Ikawa sooo.Nikampooza basi Amar nimekosea. Tena sitaki kusikia mambo ya kipuuzi kama hayo. Ikawa basi tena.Kuna mhikaji wake mmoja akamwambia Amar yule demu si humtaki, mi nampendaa, nakuomba ruhusa uniachie mimi, wewe si ushasema mbaya, mi nimemuelewa. Alipigwaaa sio kitoto. Kisa mi nimehangaika kutafuta secretary mda mreu kmpata mnashoboka mnataka kumjaza mimba ili niadhirike. Hakuna kuchanganya kazi na mapenzi.

Joey akawa kaanza kurudi rudi baada ya Phesto kuondoka, kumbe Phesto alimchimba mkwara akae mbali kabisa lasivo atamjua yeye nani. Basi Joey hana iyana, si anajua mi kwa Amar nafanya kazi tu, basi kiroho safi akataka kuwa washkaji na boss wangu. Maana mda wa kuhang out na mimi hakuna, mda wote nipo kazini kwa Amar au shule. Basi Amar akawa cool kabisa, zikaiva na Joy, Joey akanza kuleta wateja, hapo Amar yuko byeeee. Ila Joey asipokuwepo Amara anmponda Joey kishenziii. Akiwepo washkaji hatariiii.

Siku hio tukapanga na Joey kesho tukafanye yetu, si mnajua hatukumaliza. Alishaniomba msamaha na sahivi akawa anataka hatari, mi ndo namcheleweshaaa. Anabembelezaaaa, nikawa sasa nisharidhia kbisaaa kumpaaa. Sasa kwa Amar ndo kazi ipo, nitapataje ruhusa. Ikabidi tu nimwambie sikia Amar, nikampa A to Z. Jinsi ambavo hatukufanikisha na sasa kesho naomba off nikafanikishe mambo yangu. Akasema Off hakuna. Namuuliza kwanini nimesema off hakuna. Nikawa nimenuna. Nikapelekasimu, na kuleta hela nimenuna, sicheki kabisaaa. Akajua nimechukia. Akaniambia we usiende shule kesho njoo home, kuna delivery moja tu afu unaweza kwenda kuliwa zako maana ulivoshupalia huko kuliwa mmmh. Nikafurahiii. Akanisistiza usije na Joey hii simu tumemuibia baba yake Joey nimeikagua kuna picha za familia yao.

Asubuhi nikavaa uniform, kufika bar nikavua na kuvaa mini yangu y hatari, nikaenda kwa kina Amar, sikuwa nimewahi kufika wala nini. Maisha magumu, ila nikajionea sawa tu akili yote kwenye kwenda kuliwa. Nataka nichukue simu nichimbe. Bibi akaniambia huyo mwenzio mbwaa, wala sio mtu. Yaani unajiaribia maishaaa, tunamjua sis. Nikasema mimi secretary wake, bibi akasonya. Amar alikuwa bafuni akatoka na mapovu hajajissuza vizuri, analalamika bibi bwana mbona unaniwangiaaaa lakiniii. Sydney twende bwana. Bibi yuko Secretary, mxiuuuuuuuuuuu. Mtumie condom. Hahahaaaaaa! Mi nikacheka tuuuuu.

Tumefika, akafunga mlango na funguo. Akili yote labda sababu bibi kachonga chonga htaki ajue anafanya dili za simu. Weeeeeeeeeeeeeeee! Mmmmmmmmmhhhhhhhh

ITAENDELEA KESHO SAA 7 MCHANA.
 
Back
Top Bottom