Website opening, operating and costs

Website opening, operating and costs

Kuna aina mbili za Website (1). static website -hii ni website ambayo haina support ya user interraction yaani huwezi kufanya activity yoyote zaidi ya kuperuzi website pages zake. (2). Dynamic website ni website ambayo inaweza kuwa na form unajaza na kuiSubmitt hapo na ikaenda kwenye database ya website hiyo.

Blog ni aina ya website ambayo mwanzoni zilikuwa zinaandaliwa kwa Page moja tu ambayo ni refu, ila kwa sasa blog zimeboreshwa na zinaweza kuwa na page nyingi nyingi mfano wa blog ni blog ya IssaMichuzi.blogspot.com . blog ni maalum kwaajili ya kuweka matukio kwa mfumo wa POSTS.

Gharama za kutengeneza na kuMaintain website zinatofautiana kulingana na aina ya website, ukubwa na lugha iliyotumika pamoja na mahitaji ya mwenye website.

Sheria zinazoregulate operation za website ni sheria za MTANDAO- kulingana na dhumuni la website na shughuli zake, kama ni website ya biashara basi biashara yako iwe imesajiliwa, halali na ulipe kodi.

website kama JF ni Dynamic website ambayo ni Forum.

Mkuu kama nna static website ni lazima nitumie back end languages kama php??au css na html na js zinatosha??

Ni site nliyotaka kuweka contents ambazo users wata download...picha ...documents!!
 
Mkuu kama nna static website ni lazima nitumie back end languages kama php??au css na html na js zinatosha??

Ni site nliyotaka kuweka contents ambazo users wata download...picha ...documents!!
Kila language hapo ina umuhimu wake hata kama website sio dynamic.

CSS inatumika kwenye Layout/muonekano wa web page. Yaani hiyo ndio itakayoisimamisha website yako na kuifanya ionekane kama unavyotaka. Css itafanya yafuatayo: Size ya page, rangi ya section za page au page nzima au background color, font color/ size/style, effects ndogo ndogo za picha kama vile opacity, hover, transition delays na filter.

JAVASCRIPT : pia inatumika zaidi katika effects Za text picha na slideshows pamoja na onPage validations.

PHP sasa hapo ndipo unaporahisisha website yako ya static/ dynamic.
Kwa mfano umeDesign website yenye page 40 na kila page ina sections 5
1. Header/menu
2. Left-bar
3. Right-bar
4. Contents-container
5. Footer

Sasa kwa kutumia PHP utatengeneza function ya kila section. Na hizo function utazisave kwenye file totauti kwa hiyo kwenye kila page utaziita (include) hizo function pale panapohusika.

Faida zake PHP
Mfano ,Mwenye website akitaka umbadilishie ile copyright kutoka mwaka2016 kuwa 2017 , basi wewe utaenda tu kwenye function ya FOOTER.PHP utaiEdit na itaReflect page zote. Pia kuEdit menu ni hivyo hivyo.

Bila PHP utasota sana.
 
Kwa kifupi kusajili na kurusha website hewani inagharimu takriban elfu 70 kwa mwaka kwa makampuni ya hapa tanzania.

Utahitaji kulipa hiyo gharama kila mwaka.

Ili website iwe hewani unahitaji kuitengeneza (designing) ambapo unaweza kuifanya mwenyewe kama una uwezo au unaweza kufanyiwa na mtu mwingine kwa malipo ya makubaliano.

............

Kifupi ili web iwe hewani:
1. Design your site
2. Register (sajili jina/ domain) utalipia kama elfu 20 .
3. Hosting (utalipia storage ya kuiweka web yako kwa gharama kama tsh elfu 50)

4. Upload ( kuirusha web yako) hii hailipiwi
Thankyuuu
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom