Uchaguzi 2020 Wazo Langu: Lowasa kuwania urais 2020 kwa mara nyingine

Watoto ni wengi humu jf hadi kero!.

Hawajui kuwa CCM tayari inao utaratibu wake wa ndani, hakuna fomu yoyote ya urais itatolewa kwa mwana CCM yeyote zaidi ya the seating one.

P.
Mkuu huo utaratibu umewekwa na watu kwa utaratibu wa kumpata mgombea Urais wa ccm 2015 ndio ule? Watanzania sio Wajinga mkuu , Kwani uliamini Lowassa huyu angeweza kubembelezwa na ccm arudi ccm? Unaukumbuka ule wimbo aliyoimbiwa Lowassa dodoma? Unakumbuka hotuba ya Mwenyekiti baada ya kukabidhiwa uongozi Dodoma?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Huyo Kanjanja Pascal Mayalla anadhani ana hati miliki ya ujuvi wa siasa za Tanzania. Haha.

Hafahamu kwamba Katiba za vyama vya siasa zinabadilishwa wakati wowote tu.
 
Ile sheria ya Msajili wa vyama vya siasa ikifanya kazi Lowassa atapita..wacheze tu vyema na msajili hapo ndio watajua sheria ni msumeno

Msajili anamfuta Magufuli then Lowassa anashika usukani, Picha linaisha
 
Watoto ni wengi humu jf hadi kero!.

Hawajui kuwa CCM tayari inao utaratibu wake wa ndani, hakuna fomu yoyote ya urais itatolewa kwa mwana CCM yeyote zaidi ya the seating one.

P.
Binafsi nilishaongea jukwaa la siasa sasa limekuwa jukwaa la propaganda! watu wakunywa Double Kick wanakuja kupost habari za kipuuzi na kama wakina Prof; kitila, Makamba, Kingwangala na Mwigulu tumewapoteza basi sitoshangaa kama Mayala naye atatukimbia! Imekuwa zaidi ya Ffacebook jamani mpaka inaboa..! na watu wanaolipwa ndiyo wanatuharibia jukwaa.
 
Si mbunge msukuma kasema huyo mdingi anajinyea nyea sasa nani atampitisha kugombea labda aende kwa Dovutwa.
Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kama katiba za vyama hubadilishwa, basi kwa lowassa anything can happen. Halafu, kinachofikirisha hoja za upinzani zitakuwaje, endapo anasimamishwa na lissu. Tusubiri. 2020 sio mbali, sijui kina juma nkamia lile wazo la miaka 7 watalitoa tena wakiwa na nani. Siasa bwana. Nasisitiza tena kwa jinsi siasa zinavyobadilika tusimpinge mtoa mada!!
 
Watoto ni wengi humu jf hadi kero!.

Hawajui kuwa CCM tayari inao utaratibu wake wa ndani, hakuna fomu yoyote ya urais itatolewa kwa mwana CCM yeyote zaidi ya aliyepo.
Kuhusu "utoto" hapo unawaonea na kutaka kuwafunika gubigubi kwa shuka la mchunga ng'ombe.Hivi ni utaratibu usio kwenye maandishi waliojiwekea CCM au ni sheria?Kama ni sheria,ina maana inapingana na sheria mama ya nchi?
 
Ile sheria ya Msajili wa vyama vya siasa ikifanya kazi Lowassa atapita..wacheze tu vyema na msajili hapo ndio watajua sheria ni msumeno

Msajili anamfuta Magufuli then Lowassa anashika usukani, Picha linaisha
Ha ha ha hiyo sio picha ni jinamizi la kutisha sana.
 

Mkuu ni ' Vijiwe ' gani hapo ulipo vinauza Bange / Bangi zenye ' Viwango ' vizuri vya ' Kumlandua ' Mtu?
 
Wazee wasiokuwa na shukrani ndiyo hawa, umekaribishwa umekula ugali umeshiba hata kusema asanteni ndugu naondoka zii - ukiwa na wazee 10 wa sampuli hii taifa haliwezi kusonga.
 
Akitaka kugombea anarudi CHADEMA anawateka anagombea. Maana anawajua sana dawa yenu, ni kupenyeza rupia nyote chaliiiiiiii! manaanza kudeki lami basi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…