Waziri wa viwanda akijibu swali kuhusu uagizwaji wa toothpick kutoka nje ya nchi

real G

JF-Expert Member
Feb 7, 2013
5,227
5,296


Anasema ''Mashine ya kutengeneza toothpick ni doa 28,000, dola 28,000 ni jukumu lako mtanzania kuwekeza, kuna watanzania wanaogiza mashine za toothpick, mfano mheshimiwa Lema ameagiza mashine ya toothpick anapeleka Kilimanjaro, watu wanahangaika, msikosoe tu,

Toothpick inatumia mabaki ya miti yasiyokuwa na kazi nyingine, na wala sio mbao, viwanda ni vita bwana Msigwa, toothpick mkitaka zisiagizwe nitazizuia zisiagizwe, TBS ni yangu, lakini na nyie muwekeze, watu wanapenda toothpick''

Mimi naona watanzania tusikae chini na kuiacha serikali pekee ndio ianzishe viwanda, bali wenyewe tujiongeze tupige hata kolabo kuanzisha viwanda vidogo vya usindikaji na hatimae tujenge uwezo hadi kuwekeza kwenye viwanda vikubwa, badala ya kuwekeza kwenye matanuzi na luxury na kukaa kuiombea serikali ifeli na kukesha kwenye social media kuchonga.
 
Mimi naona watanzania tusikae chini na kuiacha serikali pekee ndio ianzishe viwanda, bali wenyewe tujiongeze tupige hata kolabo kuanzisha viwanda vidogo vya usindikaji na hatimae tujenge uwezo hadi kuwekeza kwenye viwanda vikubwa, badala ya kuwekeza kwenye matanuzi na luxury na kukaa kuiombea serikali ifeli na kukesha kwenye social media kuchonga
Wanaiachia serikali kwa sababu kuu 2 Moja ni urasmu katika sekta ya uwekezaji ukiomba mkopo benk utaishia kujaza karatasi tu wakati mafisadi wanakopa hadi BOT! pili ni mitaji ni shida sana na amana hatuna pia hatuna chombo cha kusimamia sekta binafsi ili zipate mikopo hata BOT inaweka amana kwa wala rushwa tu!
 
Wanaiachia serikali kwa sababu kuu 2 Moja ni urasmu katika sekta ya uwekezaji ukiomba mkopo benk utaishia kujaza karatasi tu wakati mafisadi wanakopa hadi BOT! pili ni mitaji ni shida sana na amana hatuna pia hatuna chombo cha kusimamia sekta binafsi ili zipate mikopo hata BOT inaweka amana kwa wala rushwa tu!
pamoja na hayo bado kuna watu wenye uwezo wa kuanzisha viwanda
 
Mimi naona watanzania tusikae chini na kuiacha serikali pekee ndio ianzishe viwanda, bali wenyewe tujiongeze tupige hata kolabo kuanzisha viwanda vidogo vya usindikaji na hatimae tujenge uwezo hadi kuwekeza kwenye viwanda vikubwa, badala ya kuwekeza kwenye matanuzi na luxury na kukaa kuiombea serikali ifeli na kukesha kwenye social media kuchonga

Mkuu, wazo alilisema JPM wakati akiongea na wafanyabiashara. Alitoa mfano viwanda vya ku process samaki wa bahari pamoja na kuvua. Akasema, akijitokeza mtu, serikali itamuwezesha afanikiwe.

Sasa kuna miongoni mwetu tunadhani ni kazi ya serikali kufungua viwanda. Si kweli. Mzee Bakhresa ameonyesha mfano viwanda vingi tu. Akina Mengi nao waige si lazima iwe vitalu vya gesi.
 
Na kwa mwendo huu hakuna mtu atathubutu kuanzisha kiwanda, kama mahakama inaamuru kiwanda kilichoufungwa kwa makosa kilipwe fidia halafu rais anasema silipi, nani atathubutu kuweka hela yake rehani? Acha tuachie serikali ianzishe viwanda sie tuwe waajiriwa.
 
pamoja na hayo bado kuna watu wenye uwezo wa kuanzisha viwanda
Hakuna mfanya biashara wakuwekeza pesa yake kwenye eneo ambalo halina tija!..Mfano nataka kuwekeza sehemu ninayoona kuna mzunguko wa pesa naenda sekta ya uwekezaji inasema kwa hii miradi yako utabidi uweke njombe unadhani nitarudi??Urasi urasimu urasmu..umeingiliwa kisiasa wanasiasa wanapenda mikoa yao iwena viwanda hivyo unashinikizwa uweke mradi sehemu hata isiyofaa kuweka mradi.
 
Mkuu, wazo alilisema JPM wakati akiongea na wafanyabiashara. Alitoa mfano viwanda vya ku process samaki wa bahari pamoja na kuvua. Akasema, akijitokeza mtu, serikali itamuwezesha afanikiwe.

Sasa kuna miongoni mwetu tunadhani ni kazi ya serikali kufungua viwanda. Si kweli. Mzee Bakhresa ameonyesha mfano viwanda vingi tu. Akina Mengi nao waige si lazima iwe vitalu vya gesi.

Mengi amuige Bakhresa hahah, upstairs ni shida
 
Waziri anapojibu swali kwa hoja za msingi inafurahisha sana. Wabunge walw mabingwa wa mipasho na maneno ya ovyo ovyo nina imani wamejifunza kitu kwa waziri huyu.
 
Si waliahidi, sasa sisi watanzania masikini tutatoa wapi hela ya kuwekeza wakati hela ya chakula tu inatusumbua

Kutengeneza toothpick ni kitu kidogo sana.Kanunue wembe tafuta ile mifagio inaitwa chelewa ifumue chonga na wembe kila kipande cha mfagio funga vipande 30 kila kifungo hata na raba bendi anza kuuza.Mtaji hauzidi hata shilingi elfu 20.

Hivi vitivo vya engineering vya vyuo vyetu vikuu hawajaweza toa hata engineer wa kutengeneza toothpick kwa kutumia vile vimiti vya mifagio ya chelewa?

Hizo mashine hawawezii unda? Ni aibu kukuta msomi tena engineer anafanya biashara ya baa au duka la kupima unga.

Mainjinia oneni aibu popote mlipo
 
Hakuna mfanya biashara wakuwekeza pesa yake kwenye eneo ambalo halina tija!..Mfano nataka kuwekeza sehemu ninayoona kuna mzunguko wa pesa naenda sekta ya uwekezaji inasema kwa hii miradi yako utabidi uweke njombe unadhani nitarudi??Urasi urasimu urasmu..umeingiliwa kisiasa wanasiasa wanapenda mikoa yao iwena viwanda hivyo unashinikizwa uweke mradi sehemu hata isiyofaa kuweka mradi.
mkuu mbona kuna wadau wamewekeza kwenye viwanda vya maziwa, tomato, juice, chilli, chakula cha mifugo, unga, mafuta n.k na vinawalipa au hawaishi Tanzania?
 
Kutengeneza toothpick ni kitu kidogo sana.Kanunue wembe tafuta ile mifagio inaitwa chelewa ifumue chonga na wembe kila kipande cha mfagio funga vipande 30 kila kifungo hata na raba bendi anza kuuza.Mtaji hauzidi hata shilingi elfu 20.

Hivi vitivo vya engineering vya vyuo vyetu vikuu hawajaweza toa hata engineer wa kutengeneza toothpick kwa kutumia vile vimiti vya mifagio ya chelewa?

Hizo mashine hawawezii unda? Ni aibu kukuta msomi tena engineer anafanya biashara ya baa au duka la kupima unga.

Mainjinia oneni aibu popote mlipo
soko la ushindani hili, mtu unatakiwa utoe vitu vyenye ubora na vinavyovutia, mifagio ya chelewa???
 
soko la ushindani hili, mtu unatakiwa utoe vitu vyenye ubora na vinavyovutia, mifagio ya chelewa???

Wanunuzi wa aina zote wapo.Wako wapenda vya hiGH quality na wako wapenda vya low quality.Tanzania inao wote
 
Nimependa wazo lako. Nami naongezea kwanini serikali isipeleke wasomi wachukue utaalamu

Wasomi wetu si kuwa hawajui wameshapelekwa sana huko nje kujifunza wakiwemo wabunge.Tatizo linalokuja wakirudi badala ya kuja na mshine za kutengeneza toothpick wanarudi wakituonyesha picha walizopiga huko nje we angalia mbunge Mchungaji Msigwa aliyeenda marekani karudi na hii picha

_DSC8604.JPG
 
Back
Top Bottom