Waziri wa mambo ya nje wa China aanza ziara ya kwanza ya mwaka mpya barani Afrika, desturi ikidumu miaka 33 mfululizo

ldleo

JF-Expert Member
Jan 9, 2010
1,010
1,034
VCG11433659357.JPG


Kuanzia tarehe 9 hadi 16 mwezi huu, waziri mpya wa mambo ya nje wa China Bw. Qin Gang atafanya ziara nchini Ethiopia, Gabon, Angola, Benin, Misri, na pia kutembelea makao makuu ya Umoja wa Afrika na ya Jumuiya ya Nchi za Kiarabu.

Hii sio tu ni ziara ya kwanza ya mambo ya nje ya Qin Gang akiwa waziri wa mambo ya nje wa China, bali pia ni desturi iliyodumu miaka 33 mfululizo, yaani ziara ya kwanza ya waziri wa mambo ya nje wa China mwanzoni mwa kila mwaka lazima iwe barani Afrika kama “kuwatembelea jamaa za Afrika”.

Mwaka 2013, Rais Xi Jinping wa China alifanya ziara nchini Tanzania, Afrika Kusini na Jamhuri ya Kongo, na kuandika historia kwa mkuu wa China kutembelea bara la Afrika katika ziara yake ya kwanza nje ya nchi.

Ni katika ziara hiyo, Xi Jinping alitaja kwa mara ya kwanza dhana ya sera ya China kuhusu Afrika yaani “Udhati, Nia njema, Upendo, Matokeo Halisi " na mtazamo sahihi kuhusu haki na faida, ukiwa ni kama mwongozo wa kimsingi wa ushirikiano kati ya China na Afrika katika zama mpya.

Safari hii ya waziri Qin Gang katika nchi tano za Afrika itakuwa ni ziara ya kurithi yaliyopita na kukaribisha yajayo, na italenga kuimarisha uhusiano wa wenzi wa ushirikiano wa kimkakati wa pande zote kati ya China na Afrika, kutekeleza makubaliano yaliyofikiwa na rais Xi Jinping na wenzake wa nchi za Afrika kwenye Mkutano wa nane wa mawaziri wa Baraza la Ushirikiano kati ya China na Afrika uliofanyika mwaka 2021, na kueleza kwa vitendo kuwa China inatimiza ahadi zake kwa ushirikiano wa kirafiki na Afrika na kamwe haiandiki ahadi tupu.

Mwaka uliopita ulikuwa mwaka wenye changamoto kubwa kwa China na Afrika kwa pamoja. Lakini haijalishi jinsi hali ya kimataifa inavyobadilika, urafiki kati ya China na Afrika haujawahi kufifia. Pande hizo mbili zimepiga hatua kubwa katika kuaminiana kisiasa, biashara na sekta nyingine.

Mwezi Februari, Chuo cha Uongozi cha Mwalimu Nyerere, kilichoanzishwa kwa pamoja na vyama sita vya Kusini mwa Afrika, kilizinduliwa Tanzania, na kuashiria kuanza kwa jaribio kati ya China na Afrika katika kubadilishana uzoefu kuhusu utawala wa nchi.

Baada ya kumalizika kwa Mkutano Mkuu wa 20 wa Chama cha Kikomunisti cha China CPC mwezi Oktoba, uhusiano kati ya China na Afrika ulipata fursa mpya.

Akiwa rais wa kwanza wa Afrika kupokelewa na China baada ya Mkutano huo, Rais Samia Hassan wa Tanzania alialikwa kufanya ziara ya kiserikali nchini China kuanzia tarehe 2 hadi 4 Novemba.

Rais Xi Jinping na Rais Samia kwa pamoja walitangaza kuinua ngazi ya uhusiano kati ya China na Tanzania kuwa wenzi wa ushirikiano wa kimkakati wa pande zote, na kufungua ukurasa mpya wa maendeleo ya uhusiano kati ya China na Tanzania na ujenzi wa jumuiya ya China na Afrika yenye mustakabali wa pamoja.

Kwa upande wa biashara, katika kipindi cha miezi 11 ya kwanza ya mwaka 2022, thamani ya biashara kati ya China na Afrika ilikuwa takriban dola za Marekani bilioni 258.9, na kuzidi ile ya mwaka mzima wa 2021.

Mapema mwezi Agosti, shehena ya kwanza ya maparachichi mabichi iliyosafirishwa kutoka Afrika ilifika katika bandari ya mjini Shanghai. Mbali na hayo, nchi 18 za Afrika zilipewa hadhi ya kutotozwa ushuru kwa asilimia 98 ya bidhaa zao na serikali ya China mwaka jana, ili nchi hizo zinufaike zaidi na soko kubwa la China.

Mwaka huu, tutaadhimisha miaka 10 ya kutolewa kwa dhana ya sera kwa Afrika “Udhati, Nia njema, Upendo, Matokeo Halisi” na mtazamo sahihi kuhusu haki na faida, na pia itakuwa kumbukumbu ya miaka 10 ya kutolewa kwa Pendekezo la "Ukanda Mmoja, Njia Moja".

Sababu ya uhusiano mzuri kati ya China na Afrika kuimarika kwa muda mrefu ni kwamba pande hizo mbili zinashikilia mtazamo sahihi katika kushughulikia uhusiano wao, na kutafuta maendeleo kwa pamoja.

Huku hali ya sasa ya kimataifa ikiendelea kukabiliwa na msukosuko na mabadiliko makubwa, China itaendelea kuunga mkono Afrika kufuata mikakati ya diplomasia huru na ya pande mbalimbali, kuunga mkono Umoja wa Afrika kujiunga na kundi la G20, na kuzisaidia nchi za Afrika kufufua na kuendeleza uchumi na kutoa mchango mpya kwa ujenzi wa Jumuiya ya China na Afrika yenye mustakabali wa pamoja.
 
Back
Top Bottom