tonicimmobility
JF-Expert Member
- Jun 17, 2025
- 493
- 1,038
Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega, amebaini maendeleo chanya katika ujenzi wa madaraja ya dharura mkoani Lindi, wakati wa ziara ya ukaguzi wa miradi hiyo ambayo imefikia karibu asilimia 90 ya utekelezaji wake.
Madaraja haya yamejengwa katika maeneo yaliyoathirika sana na mvua, ikiwemo Somanga, Njia Nne na Matandu, ambapo barabara zilizoharibika wakati wa majira ya mvua kwa miaka mingi zilikuwa zinakwamisha usafiri kuelekea mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma.
Akizungumza baada ya ukaguzi, Waziri Ulega alisema kuwa mara madaraja yote yatakapokamilika, changamoto za usafiri zinazojitokeza kila mwaka wakati wa mvua zitapungua na kutoweka kabisa.
“Nimefurahishwa na maendeleo haya. Kila kitu kipo kwenye mstari sahihi, na kazi inatia moyo sana. Natoa shukrani za dhati kwa Rais Dkt. Samia Suluhu kwa kuidhinisha matumizi ya zaidi ya Shilingi Bilioni 400 kwa miradi ya dharura inayolenga kupunguza athari za mvua na kimbunga,” alisema Waziri Ulega.
Aidha, Waziri Ulega aliwahakikishia Wananchi kuwa wakandarasi watashirikiana kufanya kazi kwa bidii usiku na mchana ili kufanikisha kukamilika kwa madaraja yote ifikapo Desemba 24, 2025. “Barabara za maungio na taa za barabarani pia zitatimia, kuhakikisha usafiri ni salama na wa uhakika,” aliongeza.
Ukaguzi wa madaraja umeonyesha maendeleo yafuatayo: Daraja la Somanga Mtama lenye urefu wa mita 60 limefikia asilimia 89, Daraja la Kipatwa (mita 40) asilimia 86.7, Daraja la Mikereng’ende (mita 40) asilimia 90.06, na Daraja la Njenga (Matandu, mita 60) asilimia 86.67.
Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Mohammed Nyundo, aliipongeza Wizara ya Ujenzi na TANROADS kwa juhudi za dhati, akithibitisha kuwa Wananchi wataanza kutumia madaraja haya mara mvua zitakapopungua.
Meneja wa TANROADS Mkoa wa Lindi, Emil Zengo, alifafanua kwamba katika Daraja la Somanga Mtama, mkandarasi amekamilisha ujenzi wa nguzo 43 zenye urefu wa mita 12, nguzo kuu tatu, boriti za chuma na kimsingi ameshamaliza kusuka nondo katika kitako cha daraja kwa ajili ya kumwaga zege.
Madaraja haya yamejengwa katika maeneo yaliyoathirika sana na mvua, ikiwemo Somanga, Njia Nne na Matandu, ambapo barabara zilizoharibika wakati wa majira ya mvua kwa miaka mingi zilikuwa zinakwamisha usafiri kuelekea mikoa ya Lindi, Mtwara na Ruvuma.
Akizungumza baada ya ukaguzi, Waziri Ulega alisema kuwa mara madaraja yote yatakapokamilika, changamoto za usafiri zinazojitokeza kila mwaka wakati wa mvua zitapungua na kutoweka kabisa.
“Nimefurahishwa na maendeleo haya. Kila kitu kipo kwenye mstari sahihi, na kazi inatia moyo sana. Natoa shukrani za dhati kwa Rais Dkt. Samia Suluhu kwa kuidhinisha matumizi ya zaidi ya Shilingi Bilioni 400 kwa miradi ya dharura inayolenga kupunguza athari za mvua na kimbunga,” alisema Waziri Ulega.
Aidha, Waziri Ulega aliwahakikishia Wananchi kuwa wakandarasi watashirikiana kufanya kazi kwa bidii usiku na mchana ili kufanikisha kukamilika kwa madaraja yote ifikapo Desemba 24, 2025. “Barabara za maungio na taa za barabarani pia zitatimia, kuhakikisha usafiri ni salama na wa uhakika,” aliongeza.
Ukaguzi wa madaraja umeonyesha maendeleo yafuatayo: Daraja la Somanga Mtama lenye urefu wa mita 60 limefikia asilimia 89, Daraja la Kipatwa (mita 40) asilimia 86.7, Daraja la Mikereng’ende (mita 40) asilimia 90.06, na Daraja la Njenga (Matandu, mita 60) asilimia 86.67.
Mkuu wa Wilaya ya Kilwa, Mohammed Nyundo, aliipongeza Wizara ya Ujenzi na TANROADS kwa juhudi za dhati, akithibitisha kuwa Wananchi wataanza kutumia madaraja haya mara mvua zitakapopungua.
Meneja wa TANROADS Mkoa wa Lindi, Emil Zengo, alifafanua kwamba katika Daraja la Somanga Mtama, mkandarasi amekamilisha ujenzi wa nguzo 43 zenye urefu wa mita 12, nguzo kuu tatu, boriti za chuma na kimsingi ameshamaliza kusuka nondo katika kitako cha daraja kwa ajili ya kumwaga zege.