Lyimo
JF-Expert Member
- Mar 7, 2006
- 3,826
- 2,017
Inasikitisha kusikia kauli ya Waziri mwenye dhamana katika mawasiliano, Sayansi na technologia, Prof. Makame Mnyaa Mbarawa kueleza kuwa Tanzania haina watafiti wenye sifa. Taarifa hii aliitoa kwenye maadhimisho ya miaka 50 ya chuo kikuu cha Dar es salaam (Source: Mwananchi ya leo). Kutokana na kauli yake anataka wafanyakazi wote kwenye taasisi zinazoendesha utafiti wawe wenye shahada ya juu ya uzamivu (PhD), kitu ambacho si kweli. Inaelekea hata yeye licha ya kuwa Professor hajui utaratibu wa jinsi tafiti zinavyoendeshwa. Hajathamini taaluma zingine kama Shahada za uzamili (Masters), Shahada ya kwanza (Bachelor), Stashahada (Diploma) naAstashahada (Certificate/Cheti), ambao wote wanashughuli muhimu katika kufanikisha shughuli nzima ya utafiti. Pia kuna wengine hujifunza kuendesha mitambo tu ama kazi za maabara (technicians) ambao hawahitaji kufikia ngazi ya shahada ya Uzamivu. Kwa ujumla mtu mmoja/wachache wenye PhD wanaweza saidiwa na kada zote hizi kulingana na aina ya tafiti iliyopangwa.
Ni ukweli ulio wazi serikali yetu haithamini mambo ya tafiti, kwanza inatoa pesa ndogo sana (Chini ya asilimia 1) katika taasisi zake ikiwemo vyuo vikuu. Huwezi amini watafiti wengi wanategemea waandike mapendekezo (proposals) kwa wafadhili wan je ambao mara nyingi inabidi kufuata matakwa yao, hivyo matatizo ya Tanzania yanakuwa hayawakilishwi kwa kiwango stahili. Vilevile tatizo linguine kubwa la serikali yetu, ni kutofanyia kazi matokeo/mapendekezo yanayotokana na tafiti zetu. Hivyo kuna taarifa nyingi za tafiti zimebaki kwenye makabati na hata kupoteza uhalisia wake kutokana na muda kupita. Kama serikali ingekuwa na nia ya dhati ya kuwatumia watafiti waliopo, ingepiga hatua kubwa katika kutatua matatizo mbalimbali. Tumeshuhudia watafiti wengi kwenye vituo vya tafiti (tena hao wenye PhD) kutokuwa na kazi kutokana na kutokuwepo kwa nyenzo/vitendea kazi na/ama kutotengwa fungu la kuendesha shughuli hizi muhimu.
Ni wakati muafaka sasa, serikali ijifunze kuwatumia wataalamu wetu kwa uchache wao ili kuleta tija kwa Taifa. Inasikitisha kutokana nakutokuwa na mazingira mazuri ya kuwatumia wataalamu wetu, hivyo inawafanya wengi kufanya tafiti zenye matakwa ya wafadhili, kukimbia nchi na kwenda kuutumia utaalamu wao nje ama kukimbilia kwenye siasa kama tunavyoshuhudia hivi sasa. Vilevile nchi yetu haina mahusiano ya moja kwa moja kati ya taasisi za utafiti, Viwanda, Vyuo vikuu, wadau (wakulima, wafanyabiashara nk) kwa kujumla wake katika kutekeleza shughuli nzima za tafiti kama wanavyo fanya nchi za wenzetu wanaoweza kutumia tafiti kama njenzo muhimu katika kutatua matatizo mbalimbali kwenye sekta mbalimbali. Hivyo serikali isikimbilie kusema tanzania haina watafiti wenye sifa wakati haina mikakati yoyote ya kuwatumia vizuri hawa walipo.
Ni ukweli ulio wazi serikali yetu haithamini mambo ya tafiti, kwanza inatoa pesa ndogo sana (Chini ya asilimia 1) katika taasisi zake ikiwemo vyuo vikuu. Huwezi amini watafiti wengi wanategemea waandike mapendekezo (proposals) kwa wafadhili wan je ambao mara nyingi inabidi kufuata matakwa yao, hivyo matatizo ya Tanzania yanakuwa hayawakilishwi kwa kiwango stahili. Vilevile tatizo linguine kubwa la serikali yetu, ni kutofanyia kazi matokeo/mapendekezo yanayotokana na tafiti zetu. Hivyo kuna taarifa nyingi za tafiti zimebaki kwenye makabati na hata kupoteza uhalisia wake kutokana na muda kupita. Kama serikali ingekuwa na nia ya dhati ya kuwatumia watafiti waliopo, ingepiga hatua kubwa katika kutatua matatizo mbalimbali. Tumeshuhudia watafiti wengi kwenye vituo vya tafiti (tena hao wenye PhD) kutokuwa na kazi kutokana na kutokuwepo kwa nyenzo/vitendea kazi na/ama kutotengwa fungu la kuendesha shughuli hizi muhimu.
Ni wakati muafaka sasa, serikali ijifunze kuwatumia wataalamu wetu kwa uchache wao ili kuleta tija kwa Taifa. Inasikitisha kutokana nakutokuwa na mazingira mazuri ya kuwatumia wataalamu wetu, hivyo inawafanya wengi kufanya tafiti zenye matakwa ya wafadhili, kukimbia nchi na kwenda kuutumia utaalamu wao nje ama kukimbilia kwenye siasa kama tunavyoshuhudia hivi sasa. Vilevile nchi yetu haina mahusiano ya moja kwa moja kati ya taasisi za utafiti, Viwanda, Vyuo vikuu, wadau (wakulima, wafanyabiashara nk) kwa kujumla wake katika kutekeleza shughuli nzima za tafiti kama wanavyo fanya nchi za wenzetu wanaoweza kutumia tafiti kama njenzo muhimu katika kutatua matatizo mbalimbali kwenye sekta mbalimbali. Hivyo serikali isikimbilie kusema tanzania haina watafiti wenye sifa wakati haina mikakati yoyote ya kuwatumia vizuri hawa walipo.