WAZIRI NCHIMBI:Damu ya mchungaji ilete Amani

WAZIRI NCHIMBI:Damu ya mchungaji ilete Amani

WABHEJASANA

JF-Expert Member
Joined
Jun 22, 2011
Posts
4,225
Reaction score
869
Habari wakuu?!

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya nchi Emmanuel Nchimbi amesema Damu ya Mchungaji Mathayo Kachira aliyeuawa katika mapigano kati ya Wakristo na Waislamu yaliyotokea Jumatatu wiki hii katika Mji Mdogo wa Katoro wilayani Chato Mkoani Geita,itumike kuleta Amani juu ya mgogoro wa Uchinjaji.



Nchimbi ametoa kauli hiyo muda mfupi uliopita wakati wa mazishi ya mchungaji huyo ambayo yamefanyika nyumbani kwake Buselesele,na kuhudhuriwa na mamia ya watu ambao ni waumini wa madhehebu ya kikristo.



Amewataka wachungaji na maaskofu kuhubiri Amani,na kuwakemea wachungaji wote ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kuchochea mgogoro wa nani mwenye mamlaka ya kuchinja kati ya Waislamu na wakristo ambao uliibuka hivi karibuni,huku akisema kwamba serikali itaendelea kusimamia amani ili kuepusha nchi kuingia kwenye vurugu.



Hata hivyo mmoja wa wachungaji waliokuwa wakishikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya Mchungaji Mathayo,akihubiri wakati wa kuuaga mwili wa marehemu(Mchungaji),alisisitiza kwamba wakristo wataendelea kuchinja nyama kwa ajili ya mahitaji yao,na kwa kuanza wanaanza leo kwenye msiba huo.



Kuachiwa kwa mchungaji huyo Isaya Ikiri wa kanisa la TAG na mwenzake Daud Merdad wa kanisa la PAG kulikuja kufuatia barua iliyoandikwa na umoja wa makanisa ya Kikristo tarehe 11 mwezi huu kwenda kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Paul Leonard wakimtaka kuwaachia wachungaji hao mara moja kwa vile hawahusiki katika tukio hilo.waliachiwa jana jioni.



Katika Tamko la umoja wa madhehebu ya Kikristo iliyosomwa mbele ya Waziri Nchini na umati wa watu waliokuwa wamehudhuria mazishi ya Mchungaji huyo,wamewataja kwa majina watu wawili waliohusika na kumchinja mchungaji Kachira na kuimba serikali kuwakamata mara moja.



Katika hali ya kungaza hakukuweo na kiongozi yeyote wa Kiislamu aliyekuwepo kwenye mazishi hayo,na habari za kina zinaeleza kwamba hata waumini wa kiislamu hawakuweza kuhudhuria mazishi hayo hata wale majirani zake na marehemu.
 
Mmoja wa waliotajwa kwenye tamko kwamba alihusika na tukio la mauaji anatibiwa hospitali ya wilaya chini ya ulinzi mkali wa polisi.
 
Habari wakuu?!

WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya nchi Emmanuel Nchimbi amesema Damu ya Mchungaji Mathayo Kachira aliyeuawa katika mapigano kati ya Wakristo na Waislamu yaliyotokea Jumatatu wiki hii katika Mji Mdogo wa Katoro wilayani Chato Mkoani Geita,itumike kuleta Amani juu ya mgogoro wa Uchinjaji.



Nchimbi ametoa kauli hiyo muda mfupi uliopita wakati wa mazishi ya mchungaji huyo ambayo yamefanyika nyumbani kwake Buselesele,na kuhudhuriwa na mamia ya watu ambao ni waumini wa madhehebu ya kikristo.



Amewataka wachungaji na maaskofu kuhubiri Amani,na kuwakemea wachungaji wote ambao wamekuwa mstari wa mbele katika kuchochea mgogoro wa nani mwenye mamlaka ya kuchinja kati ya Waislamu na wakristo ambao uliibuka hivi karibuni,huku akisema kwamba serikali itaendelea kusimamia amani ili kuepusha nchi kuingia kwenye vurugu.



Hata hivyo mmoja wa wachungaji waliokuwa wakishikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya Mchungaji Mathayo,akihubiri wakati wa kuuaga mwili wa marehemu(Mchungaji),alisisitiza kwamba wakristo wataendelea kuchinja nyama kwa ajili ya mahitaji yao,na kwa kuanza wanaanza leo kwenye msiba huo.



Kuachiwa kwa mchungaji huyo Isaya Ikiri wa kanisa la TAG na mwenzake Daud Merdad wa kanisa la PAG kulikuja kufuatia barua iliyoandikwa na umoja wa makanisa ya Kikristo tarehe 11 mwezi huu kwenda kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Paul Leonard wakimtaka kuwaachia wachungaji hao mara moja kwa vile hawahusiki katika tukio hilo.waliachiwa jana jioni.



Katika Tamko la umoja wa madhehebu ya Kikristo iliyosomwa mbele ya Waziri Nchini na umati wa watu waliokuwa wamehudhuria mazishi ya Mchungaji huyo,wamewataja kwa majina watu wawili waliohusika na kumchinja mchungaji Kachira na kuimba serikali kuwakamata mara moja.



Katika hali ya kungaza hakukuweo na kiongozi yeyote wa Kiislamu aliyekuwepo kwenye mazishi hayo,na habari za kina zinaeleza kwamba hata waumini wa kiislamu hawakuweza kuhudhuria mazishi hayo hata wale majirani zake na marehemu.


Hili suala ni rahisi sana,ila hawa wanasiasa ndio wanalikoroga,ukiangalia hapo kuwaagiza maaskofu kukemea wachungaji wanaolivalia njuga hilo,Ina maana maaskofu wakiishawakemea halafu nani aendelee kuchinja?Hapo alipaswa kuwaambia serikali italipatia ufumbuzi suala hili,then arudi zake Dar, akae na magamba wenzie waone jinsi ya kulitatua hili tatizo.Kufa kwa huyo mchungaji ni doa ambalo litaendelea kuweka uadui wa kichinichini ,siku litakuja ibuka tatizo jingine.Haya mambo ya "Funika kombe........." sio ya dunia ya sasa.
 
Hili suala ni rahisi sana,ila hawa wanasiasa ndio wanalikoroga,ukiangalia hapo kuwaagiza maaskofu kukemea wachungaji wanaolivalia njuga hilo,Ina maana maaskofu wakiishawakemea halafu nani aendelee kuchinja?Hapo alipaswa kuwaambia serikali italipatia ufumbuzi suala hili,then arudi zake Dar, akae na magamba wenzie waone jinsi ya kulitatua hili tatizo.Kufa kwa huyo mchungaji ni doa ambalo litaendelea kuweka uadui wa kichinichini ,siku litakuja ibuka tatizo jingine.Haya mambo ya "Funika kombe........." sio ya dunia ya sasa.

'Hata hivyo mmoja wa wachungaji waliokuwa wakishikiliwa na polisi kwa tuhuma za kuhusika na mauaji ya Mchungaji Mathayo,akihubiri wakati wa kuuaga mwili wa marehemu(Mchungaji),alisisitiz a kwamba wakristo wataendelea kuchinja nyama kwa ajili ya mahitaji yao,na kwa kuanza wanaanza leo kwenye msiba huo.


Kuachiwa kwa mchungaji huyo Isaya Ikiri wa kanisa la TAG na mwenzake Daud Merdad wa kanisa la PAG kulikuja kufuatia barua iliyoandikwa na umoja wa makanisa ya Kikristo tarehe 11 mwezi huu kwenda kwa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita Paul Leonard wakimtaka kuwaachia wachungaji hao mara moja kwa vile hawahusiki katika tukio hilo.waliachiwa jana jioni.

'''

KESI IMESHISHA, HAPO HAKUNA SULUHU TENA
 
Hakuna kiongozi wa serikali ngazi ya wilaya wala Mkoa aliyekuwepo wakati wa Mazishi hayo.
 
Nimesikitishwa na upotoshaji mkubwa kuhusu suala la Buseresere, pamoja na kwamba thread ya kusema Waziri Nchimbi alifukuzwa mazikoni imefungwa lakini ni vema nieleze kidogo kwa kuwa itafika mahali tutakuwa hatuamini tena kila kinachoandikwa humu. Waziri Nchimbi hakufukuzwa mazikoni alihutubia vema na akaaga akaondoka nyumbaninkwa marehemu bila bugudha yoyote. Baada ya kuondoka hapo alikwenda kupanda gari na kuondoka kurejea Geita kwa ajili ya kupanda Helikopta kuwahi Mkutano Mkuu wa Polisi unaoendelea Dodoma. Kwenye mazishi makaburini hakuwapo na huo waraka unaosemwa kuwa ulisomwa akiwepo si kweli. Waziri Nchimbi kaondoka Geita saa tano asubuhi. Ni vema waleta thread wawe wakweli kwa kuwa uongo haudumu hata kama mtu humpendi au hupendi chama chake si vema kuongea uongo wa namna hii. La mwisho, mgogoro huu katika jamii yetu tunapaswa kuwa makini sana, madhara yake yatatupata sote hakuna atakayepona hivyo tuache ushabiki wa kijinga, kawaulizeni Rwanda. Taifa likigawanyika kurudi kuwa moja itachukua muda lakini baada ya damu kumwagika sana, tizama Lebanon. Tumshukuru Mungu kwa amani hii na tuitunze.
 
Hakuna sheria katika nchi yetu inayohalalisha uchinjaji wanyama uwe wa waislamu tu. tupeane uhuru, kamwe wakristo hawawezi fanya ibada ya waislamu na waislamu vivyo hivyo.
 
Back
Top Bottom