Waziri mkuu wa mpito Nepal Aahidi kutokomeza ufisadi

Waziri mkuu wa mpito Nepal Aahidi kutokomeza ufisadi

DuaZaMama

JF-Expert Member
Joined
Jun 2, 2025
Posts
1,882
Reaction score
4,129
Waziri Mkuu wa mpito nchini Nepal Sushila Karki ameapa kufuata matakwa ya waandamanaji ya kukomesha ufisadi nchini humo wakati alipokuwa anaanza kazi yake rasmi baada ya kushika wadhifa huo..

Sushila, Waziri mkuu wa kwanza mwanamke Nepal aliye na umri wa miaka 73, alichukua nafasi hiyo baada ya maandamano ya vijana wa Gen Z kumuondoa madarakani mtangulizi wake Khadga Prasad Oli na amepewa jukumu la kuirejesha nchi katika hali ya utulivu kuelekea uchaguzi mkuu ndani ya miezi sita ijayo.

Maandamano hayo yalianza Septemba 8 baada ya serikali kufungia mitandao kadhaa ya kijamii ambapo baadae maelfu ya vijana hao waliojaa hasira waliingia barabarani kupinga pia kile walichokiita ni ufisadi na umasikini.

Soma Pia: Waziri Mkuu wa Nepal ajiuzulu kufuatia maandamano makubwa dhidi ya ufisadi yaliyopelekea vifo vya watu 19
1757915523680.png
 
Huko Nepal waziri mkuu ana nguvu kuliko rais? Maana rais ye yupo salama salimini hajala kichapo kama waziri mkuu na maafisa wengine wa serikali.
 
Inakuwaje gen z waweke ajuza madarakani, si wangeweka gen z mwenzao!?
 
Huko Nepal waziri mkuu ana nguvu kuliko rais? Maana rais ye yupo salama salimini hajala kichapo kama waziri mkuu na maafisa wengine wa serikali.
Nchi nyingi tu marais siyo watendaji wa serikali. Nepal iko hivyo. Hata Tanzania tukitaka kubadilisha utamaduni wa kuabudu rais, ingekuwa vizuri tuwe na serikali inayoundwa na vyama/chama chenye idadi kubwa ya wabunge na waziri mkuu ndiye wawe mtendaji.
 
Back
Top Bottom