ntemintale
JF-Expert Member
- Sep 6, 2016
- 952
- 1,872
Tumeshuhudia Waziri Mkuu Majaliwa, akikemea hadharani, watuhumiwa (Innocent Till Proved Guilty Under the court of law) Kwa Mujibu wa Vyanzo vyake. Watuhumiwa Hao Wa makosa mbalimbali, Ni watendaji Wa Kada za Chini Na za kawaida, Hasa Tamisemi, Elimu. n.k.
Japo kukemea kunarekebisha Tabia, lakini Kuna tatizo lililojificha ndani ya tatizo.
Mosi, Waziri Mkuu Ni Mtendaji Mkuu Wa shughuli zote za kila siku za Serikali. Je, Yeye Kama Mkuu, anakuwa wapi kusimamia na kuhakikisha Kuna Udhibiti (checks & controls) ndani ya Serikali, mpaka tunayoaminishwa kuwa Ni madudu yanatokea?
Pili, Kama taarifa anazopata Ni sahihi, Je Hao wanaopaswa kukamata, kushitaki Na kutoa haki wanakuwa wapi, mpaka wasubirie aje yeye amtaje mtuhumiwa, ambaye bado hajafikishwa mahakamani, kuwa Ni mkosaji?
Je, hizi Sio staged events (matukio ya kupangwa) ili kutuhadaa Sisi wananchi?
Je, mahakama ikimkuta mtuhumiwa Hana hatia, Waziri Mkuu atarudi Tena kutupa taarifa kuwa yule mtuhumiwa niliyemhukumu hadharani Hana hatia. Je pernality damage anayoifanya Kwa mtuhumiwa itafidiwa namna gani?
Je, Mamlaka ya Waziri Mkuu, ya kuwajibishana ndani Kwa ndani yamekuwa hafifu namna hiyo mpaka yapewe nguvu Na vyombo vya habari?
Je, Kuna muunganiko Mzuri kweli Kati ya Mamlaka ya Waziri Mkuu Na Mawaziri, Manaibu Waziri, Makatibu Wakuu Na Manaibu Makatibu Wakuu Wa Wizara husika? Wao wanakuwa wapi kukemea hayo, au wanamuacha aje atengeneze Jina Kwa wananchi?
Je, hizi ni kampeni za kuniaminisha kwa wananchi kuwa ni mchapakazi?
Nawasilisha.
Japo kukemea kunarekebisha Tabia, lakini Kuna tatizo lililojificha ndani ya tatizo.
Mosi, Waziri Mkuu Ni Mtendaji Mkuu Wa shughuli zote za kila siku za Serikali. Je, Yeye Kama Mkuu, anakuwa wapi kusimamia na kuhakikisha Kuna Udhibiti (checks & controls) ndani ya Serikali, mpaka tunayoaminishwa kuwa Ni madudu yanatokea?
Pili, Kama taarifa anazopata Ni sahihi, Je Hao wanaopaswa kukamata, kushitaki Na kutoa haki wanakuwa wapi, mpaka wasubirie aje yeye amtaje mtuhumiwa, ambaye bado hajafikishwa mahakamani, kuwa Ni mkosaji?
Je, hizi Sio staged events (matukio ya kupangwa) ili kutuhadaa Sisi wananchi?
Je, mahakama ikimkuta mtuhumiwa Hana hatia, Waziri Mkuu atarudi Tena kutupa taarifa kuwa yule mtuhumiwa niliyemhukumu hadharani Hana hatia. Je pernality damage anayoifanya Kwa mtuhumiwa itafidiwa namna gani?
Je, Mamlaka ya Waziri Mkuu, ya kuwajibishana ndani Kwa ndani yamekuwa hafifu namna hiyo mpaka yapewe nguvu Na vyombo vya habari?
Je, Kuna muunganiko Mzuri kweli Kati ya Mamlaka ya Waziri Mkuu Na Mawaziri, Manaibu Waziri, Makatibu Wakuu Na Manaibu Makatibu Wakuu Wa Wizara husika? Wao wanakuwa wapi kukemea hayo, au wanamuacha aje atengeneze Jina Kwa wananchi?
Je, hizi ni kampeni za kuniaminisha kwa wananchi kuwa ni mchapakazi?
Nawasilisha.