Waziri Mkuu Majaliwa afikishiwe ujumbe, wananchi siyo tu wanastahili kusikilizwa lakini ndio wenye maamuzi ya Mwisho

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,547
41,060
Nchi yetu ina bahati mbaya sana kwa kuwakosa viongozi ambao wana uelewa mpana, wanaoyajua mamlaka yao, wanaoelewa vizuri wajibu wao, wanaoelewa vizuri mamlaka yao yanapoishia, na hasa kwa ujumla, viongozi wanaozielewa vizuri sheria zetu na katiba yetu.

Mkataba wa hovyo wa bandari umetufanya tuwafahamu vizuri viongozi wetu ni watu wa namna gani, na zaidi kufahamu dhamira zao, na uduni wa uelewa wao katika masuala mazito ya kitaifa.

Rais hajatamka lolote mpaka sasa, tunamlaumu kwa kusaini mkataba wa hovyo kabisa usiolinda mamlaka ya nchi, uhuru wetu na wa Taifa letu, na kushindwa kufuata taratibu za mikataba. Mikataba ya uwekezaji huwa haisainiwi na Rais wa nchi, lakini kwenye hili la DP, ambayo ni kampuni, amesaini Rais wetu. Kwenye mkataba wa biashara, pande mbili zinazosaini mkataba huwa zenye nafasi sawa. Kwa hiyo Rais wa nchi yetu amejishusha na kuwa sawa na wawakilishi wa kampuni ya DP. Mkataba kwa upande wetu una sahihi ya Rais Samia, kwa upande wa pili hakuna sahihi ya Rais/kiongozi mkuu wa UAE. Rais amidhalilisha nchi.

Makamu wa Rais Dr. Mpango, kwenye hili kaamua kukaa kimya, na kwenye process nzima amejikalia kimya. Lakini kukaa kimya ni automatic submission. Kwa hiyo hapa, inamaanisha Makamu wa Rais amebariki.

Waziri Mkuu, Majaliwa Majaliwa, ambaye ana historia ya kutokuwa mkweli (wakati watu walipokuwa wanahoji kuwa Hayati Magufuli kwa nini hajaonekana kwa muda mrefu, huku kukiwa na tetesi kuwa anaumwa sana, na wengine wakisema amekwishafariki, Majaliwa alijibu kwa kufoka kuwa Rais Magufuli haonekani, wanaouliza walitaka wamwone wapi? Wamwone Kariaokoo sokoni? Akaeleza kuwa Rais Magufuli ni mzima kabisa, yupo ikulu anachapa kazi, wakati tayari Hayati Magufuli alikuwa amekwishafariki), yeye amejitokeza hadharani kuutetea mkataba huo wa hovyo. Ukiutazama mkataba wenyewe, na maneno anayoyatamka Majaliwa, ambayo hayamo kwenye mkataba, unaona wazi kuwa anaendelea na ile historia yake, kama alivyofanya kwenye taarifa kuhusiana na kifo cha Rais Magufuli. Majaliwa, mwishoni anasema kuwa eti wao viongozi wamesikia hofu za wananchi, lakini wananchi wawaamini vjongozi wao. Yaani wananchi wawaamini viongozi ambao wana historia ya kusema uwongo. Yaani wanaanchi waamini porojo za viongozi wakati wakati mkataba wenyewe upo wazi, na wananchi wana uwezo wa kuusoma, na kuuchambua, na tena baadhi ya wananchi hawa wana uelewa mkubwa maradufu ya viongozi wanaotaka waaminiwe wakati hawaaminiki.

Maswali muhimu kuhusiana na mambo ya hovyo yaliyopo kwenye mkataba ule wa hovyo, Majaliwa hajajibu hata moja, halafu anataka watu wamwini! Sisi wananchi hatujawa wajinga wa kiwango hicho.

Majaliwa anatakiwa ajibu kwa hoja, huku akifanya rejea kwenye mkataba wenyewe:

1) Kwa nini mkataba huu wa hovyo kwa upande wetu umesainiwa na Rais na kwa kwa upande wa pili haujasainiwa na mkuu wa nchi, bali kampuni?

2) IGA huwa kati ya nchi na nchi, je DP ni nchi?

3) Kama DP siyo nchi, na kama ni kampuni, zabuni ya kumtafuta mwendeshaji ilifuata taratibu na sheria za nchi, au haikufuatwa? Kwa nini?

4) IGA iliyosainiwa ndiyo Master agreement, yaani mkataba mama na mkataba kiongozi, na una nguvu ya kisheria, na hairuhusiwi kuuvunja mpaka DP waridhie, analifahamu hilo?

5) Aeleze, kwa kadiri ya IGA, kuna HGA itakayokuwa na uwezo wa kuikiuka IGA? Na hilo limeandikwa wapi kwenye mkataba uliosainiwa na Rais?

6) Nchi kutoruhusiwa kuingia makubaliano na mwekezaji mwingine yeyote ama kujenga, kuendeleza au kuendesha bandari zingine, haoni kuwa ni kuua sovereignty ya nchi?

7) Sheria zetu za fidia ya ardhi zinatamka wazi kuwa anayehitaji kuitumia ardhi, na ardhi hiyo ikawa inamilikiwa na watu au taasisi nyingine, anayeihitaji ndiye anatakiwa kulipa fidia, lakini IGA inatamka kuwa ardhi yoyote ambayo DP ataihitaji, Serikali ya Tanzania ndiyo itakayowajibika kuwaondoa wamiliki wa ardhi na kuwalipa fidia. Kwa nini sheria zetu zikanyagwe kwa sababu ya DP? Kama sheria ni mbaya, kwa nini haijabadilishwa ili kila mwekezaji akitaka kuwekeza, kazi ya kutafuta ardhi kwaajili ya mwekezaji liwe ni jukumu la Serikali?

8) Nchi yetu imewekeza matrilioni ya pesa katika kuijenga, kuiboresha na kuiendeleza bandari ya Dar es Salaam, Majaliwa aoneshe kwenye mkataba, uwekezaji wetu utatupatia hisa ngapi katika uendeshaji baada ya DP kuwekeza kiasi gani? Lakini akumbuke kuwa mktaba na DP unasema DP atakuwa na umiliki wa 100% katika uendeshaji! Yaani sisi uwekezaji wetu umefanywa kuwa ni 0%. Kama tulichowekeza sisi ni 0%, kwa nini DP asipewe eneo akajenge bandari from scratch?

9) Tatizo kubwa la kukosekana ufanisi katika miradi na mashirika yote yanayosimamiwa na Serikali, iwe ni bandari, TANESCO, mamlaka za maji, ATCL, mahospitali, TBS, n.k. ni uwezo mdogo wa viongozi wa Serikali ambao wameyageuza mashirika haya kuwa sehemu za kuwapachika watu kwa misingi ya itikadi za kisiasa, kufahamiana na undugu, na kisha kiyaingilia katika uendeshaji waje. Je, ina maana kila mahali tutawaweka wawekezaji wa nje? Kwaajili ya ufanisi, kwa nini tusiangalie kwanza msingi na chanzo cha matatizo yote ambayo ni uduni, upeo mdogo, ukosefu wa uadilifu na udhaifu wa uongozi wa nchi yetu kwa muda mrefu? Haoni tunapoteza muda kushughulika na matawi wakati shina na miziz ya mti wenye sumu umebakia kama ulivyo?

10) Ni lini JMT ilitangaza kuwa suala la bandari siyo miongoni mwa mambo ya Muungano? Maana bandari za Zanzibar hazijaingizwa kwenye mkataba huu wa hovyo.

11) Kwa nini Mbarawa, ambaye ni Mzanzibari, amekuwa waziri kwenye wizara isiyo ya Muungano? Kwa nini Aisha ambaye ni Mzanzibari, amekuwa katibu mkuu wa Wizara isiyo ya Muungano?

12) Kwa nini uporaji huu wa rasilimali za Tanganyika umefanyika kipindi ambacho wafanya maamuzi wote ni Wazanzibari, tena wengine, kwa kadiri ya artickes of union, hawakustahili kuwa kwenye nafasi ambazo zimewezesha kuporwa kwa bandari ziluzopo Tanganyika?

NB: MAJALIWA AFAHAMU KUWA WANANCHI SIYO TU WANASTAHILI KUSIKILIZWA LAKINI NDIO WENYE MAAMUZI YA MWISHO KUHUSU RASILIMALI ZAO.

WANANCHI HAWATAKIWI KUFUATA MAAMUZI YA VIONGOZI BALI VIONGOZI WANATAKIWA KUTII MAAMUZI YA WANANCHI.
 
Nchi yetu ina bahati mbaya sana kwa kuwakosa viongozi ambao wana uelewa mpana, wanaoyajua mamlaka yao, wanaoelewa vizuri wajibu wao, wanaoelewa vizuri mamlaka yao yanapoishia, na hasa kwa ujumla, viongozi wanaozielewa vizuri sheria zetu na katiba yetu.

Mkataba wa hovyo wa bandari umetufanya tuwafahamu vizuri viongozi wetu ni watu wa namna gani, na zaidi kufahamu dhamira zao, na uduni wa uelewa wao katika masuala mazito ya kitaifa.

Rais hajatamka lolote mpaka sasa, tunamlaumu kwa kusaini mkataba wa hovyo kabisa usiolinda mamlaka ya nchi, uhuru wetu na wa Taifa letu, na kushindwa kufuata taratibu za mikataba. Mikataba ya uwekezaji huwa haisainiwi na Rais wa nchi, lakini kwenye hili la DP, ambayo ni kampuni, amesaini Rais wetu. Kwenye mkataba wa biashara, pande mbili zinazosaini mkataba huwa zenye nafasi sawa. Kwa hiyo Rais wa nchi yetu amejishusha na kuwa sawa na wawakilishi wa kampuni ya DP. Mkataba kwa upande wetu una sahihi ya Rais Samia, kwa upande wa pili hakuna sahihi ya Rais/kiongozi mkuu wa UAE. Rais amidhalilisha nchi.

Makamu wa Rais Dr. Mpango, kwenye hili kaamua kukaa kimya, na kwenye process nzima amejikalia kimya. Lakini kukaa kimya ni automatic submission. Kwa hiyo hapa, inamaanisha Makamu wa Rais amebariki.

Waziri Mkuu, Majaliwa Majaliwa, ambaye ana historia ya kutokuwa mkweli (wakati watu walipokuwa wanahoji kuwa Hayati Magufuli kwa nini hajaonekana kwa muda mrefu, huku kukiwa na tetesi kuwa anaumwa sana, na wengine wakisema amekwishafariki, Majaliwa alijibu kwa kufoka kuwa Rais Magufuli haonekani, wanaouliza walitaka wamwone wapi? Wamwone Kariaokoo sokoni? Akaeleza kuwa Rais Magufuli ni mzima kabisa, yupo ikulu anachapa kazi, wakati tayari Hayati Magufuli alikuwa amekwishafariki), yeye amejitokeza hadharani kuutetea mkataba huo wa hovyo. Ukiutazama mkataba wenyewe, na maneno anayoyatamka Majaliwa, ambayo hayamo kwenye mkataba, unaona wazi kuwa anaendelea na ile historia yake, kama alivyofanya kwenye taarifa kuhusiana na kifo cha Rais Magufuli. Majaliwa, mwishoni anasema kuwa eti wao viongozi wamesikia hofu za wananchi, lakini wananchi wawaamini vjongozi wao. Yaani wananchi wawaamini viongozi ambao wana historia ya kusema uwongo. Yaani wanaanchi waamini porojo za viongozi wakati wakati mkataba wenyewe upo wazi, na wananchi wana uwezo wa kuusoma, na kuuchambua, na tena baadhi ya wananchi hawa wana uelewa mkubwa maradufu ya viongozi wanaotaka waaminiwe wakati hawaaminiki.

Maswali muhimu kuhusiana na mambo ya hovyo yaliyopo kwenye mkataba ule wa hovyo, Majaliwa hajajibu hata moja, halafu anataka watu wamwini! Sisi wananchi hatujawa wajinga wa kiwango hicho.

Majaliwa anatakiwa ajibu kwa hoja, huku akifanya rejea kwenye mkataba wenyewe:

1) Kwa nini mkataba huu wa hovyo kwa upande wetu umesainiwa na Rais na kwa kwa upande wa pili haujasainiwa na mkuu wa nchi, bali kampuni?

2) IGA huwa kati ya nchi na nchi, je DP ni nchi?

3) Kama DP siyo nchi, na kama ni kampuni, zabuni ya kumtafuta mwendeshaji ilifuata taratibu na sheria za nchi, au haikufuatwa? Kwa nini?

4) IGA iliyosainiwa ndiyo Master agreement, yaani mkataba mama na mkataba kiongozi, na una nguvu ya kisheria, na hairuhusiwi kuuvunja mpaka DP waridhie, analifahamu hilo?

5) Aeleze, kwa kadiri ya IGA, kuna HGA itakayokuwa na uwezo wa kuikiuka IGA? Na hilo limeandikwa wapi kwenye mkataba uliosainiwa na Rais?

6) Nchi kutoruhusiwa kuingia makubaliano na mwekezaji mwingine yeyote ama kujenga, kuendeleza au kuendesha bandari zingine, haoni kuwa ni kuua sovereignty ya nchi?

7) Sheria zetu za fidia ya ardhi zinatamka wazi kuwa anayehitaji kuitumia ardhi, na ardhi hiyo ikawa inamilikiwa na watu au taasisi nyingine, anayeihitaji ndiye anatakiwa kulipa fidia, lakini IGA inatamka kuwa ardhi yoyote ambayo DP ataihitaji, Serikali ya Tanzania ndiyo itakayowajibika kuwaondoa wamiliki wa ardhi na kuwalipa fidia. Kwa nini sheria zetu zikanyagwe kwa sababu ya DP? Kama sheria ni mbaya, kwa nini haijabadilishwa ili kila mwekezaji akitaka kuwekeza, kazi ya kutafuta ardhi kwaajili ya mwekezaji liwe ni jukumu la Serikali?

8) Nchi yetu imewekeza matrilioni ya pesa katika kuijenga, kuiboresha na kuiendeleza bandari ya Dar es Salaam, Majaliwa aoneshe kwenye mkataba, uwekezaji wetu utatupatia hisa ngapi katika uendeshaji baada ya DP kuwekeza kiasi gani? Lakini akumbuke kuwa mktaba na DP unasema DP atakuwa na umiliki wa 100% katika uendeshaji! Yaani sisi uwekezaji wetu umefanywa kuwa ni 0%. Kama tulichowekeza sisi ni 0%, kwa nini DP asipewe eneo akajenge bandari from scratch?

9) Tatizo kubwa la kukosekana ufanisi katika miradi na mashirika yote yanayosimamiwa na Serikali, iwe ni bandari, TANESCO, mamlaka za maji, ATCL, mahospitali, TBS, n.k. ni uwezo mdogo wa viongozi wa Serikali ambao wameyageuza mashirika haya kuwa sehemu za kuwapachika watu kwa misingi ya itikadi za kisiasa, kufahamiana na undugu, na kisha kiyaingilia katika uendeshaji waje. Je, ina maana kila mahali tutawaweka wawekezaji wa nje? Kwaajili ya ufanisi, kwa nini tusiangalie kwanza msingi na chanzo cha matatizo yote ambayo ni uduni, upeo mdogo, ukosefu wa uadilifu na udhaifu wa uongozi wa nchi yetu kwa muda mrefu? Haoni tunapoteza muda kushughulika na matawi wakati shina na miziz ya mti wenye sumu umebakia kama ulivyo?

10) Ni lini JMT ilitangaza kuwa suala la bandari siyo miongoni mwa mambo ya Muungano? Maana bandari za Zanzibar hazijaingizwa kwenye mkataba huu wa hovyo.

11) Kwa nini Mbarawa, ambaye ni Mzanzibari, amekuwa waziri kwenye wizara isiyo ya Muungano? Kwa nini Aisha ambaye ni Mzanzibari, amekuwa katibu mkuu wa Wizara isiyo ya Muungano?

12) Kwa nini uporaji huu wa rasilimali za Tanganyika umefanyika kipindi ambacho wafanya maamuzi wote ni Wazanzibari, tena wengine, kwa kadiri ya artickes of union, hawakustahili kuwa kwenye nafasi ambazo zimewezesha kuporwa kwa bandari ziluzopo Tanganyika?

NB: MAJALIWA MAJALIWA AFAHAMU KUWA WANANCHI SIYO TU WANASTAHILI KUSIKILIZWA LAKINI NDIO WENYE MAAMUZI YA MWISHO KUHUSU RASILIMALI ZAO.

WANANCHI HAWATAKIWI KUFUATA MAAMUZI YA VIONGOZI BALI VIONGOZI WANATAKIWA KUTII MAAMUZI YA WANANCHI.
Huwa wanakuja na hoja zao dhaifu eti kwamba wananchi tumeshirikishwa na tumekubali kupitia wawakilishi wetu bungeni.
 
Nchi yetu ina bahati mbaya sana kwa kuwakosa viongozi ambao wana uelewa mpana, wanaoyajua mamlaka yao, wanaoelewa vizuri wajibu wao, wanaoelewa vizuri mamlaka yao yanapoishia, na hasa kwa ujumla, viongozi wanaozielewa vizuri sheria zetu na katiba yetu.

Mkataba wa hovyo wa bandari umetufanya tuwafahamu vizuri viongozi wetu ni watu wa namna gani, na zaidi kufahamu dhamira zao, na uduni wa uelewa wao katika masuala mazito ya kitaifa.

Rais hajatamka lolote mpaka sasa, tunamlaumu kwa kusaini mkataba wa hovyo kabisa usiolinda mamlaka ya nchi, uhuru wetu na wa Taifa letu, na kushindwa kufuata taratibu za mikataba. Mikataba ya uwekezaji huwa haisainiwi na Rais wa nchi, lakini kwenye hili la DP, ambayo ni kampuni, amesaini Rais wetu. Kwenye mkataba wa biashara, pande mbili zinazosaini mkataba huwa zenye nafasi sawa. Kwa hiyo Rais wa nchi yetu amejishusha na kuwa sawa na wawakilishi wa kampuni ya DP. Mkataba kwa upande wetu una sahihi ya Rais Samia, kwa upande wa pili hakuna sahihi ya Rais/kiongozi mkuu wa UAE. Rais amidhalilisha nchi.

Makamu wa Rais Dr. Mpango, kwenye hili kaamua kukaa kimya, na kwenye process nzima amejikalia kimya. Lakini kukaa kimya ni automatic submission. Kwa hiyo hapa, inamaanisha Makamu wa Rais amebariki.

Waziri Mkuu, Majaliwa Majaliwa, ambaye ana historia ya kutokuwa mkweli (wakati watu walipokuwa wanahoji kuwa Hayati Magufuli kwa nini hajaonekana kwa muda mrefu, huku kukiwa na tetesi kuwa anaumwa sana, na wengine wakisema amekwishafariki, Majaliwa alijibu kwa kufoka kuwa Rais Magufuli haonekani, wanaouliza walitaka wamwone wapi? Wamwone Kariaokoo sokoni? Akaeleza kuwa Rais Magufuli ni mzima kabisa, yupo ikulu anachapa kazi, wakati tayari Hayati Magufuli alikuwa amekwishafariki), yeye amejitokeza hadharani kuutetea mkataba huo wa hovyo. Ukiutazama mkataba wenyewe, na maneno anayoyatamka Majaliwa, ambayo hayamo kwenye mkataba, unaona wazi kuwa anaendelea na ile historia yake, kama alivyofanya kwenye taarifa kuhusiana na kifo cha Rais Magufuli. Majaliwa, mwishoni anasema kuwa eti wao viongozi wamesikia hofu za wananchi, lakini wananchi wawaamini vjongozi wao. Yaani wananchi wawaamini viongozi ambao wana historia ya kusema uwongo. Yaani wanaanchi waamini porojo za viongozi wakati wakati mkataba wenyewe upo wazi, na wananchi wana uwezo wa kuusoma, na kuuchambua, na tena baadhi ya wananchi hawa wana uelewa mkubwa maradufu ya viongozi wanaotaka waaminiwe wakati hawaaminiki.

Maswali muhimu kuhusiana na mambo ya hovyo yaliyopo kwenye mkataba ule wa hovyo, Majaliwa hajajibu hata moja, halafu anataka watu wamwini! Sisi wananchi hatujawa wajinga wa kiwango hicho.

Majaliwa anatakiwa ajibu kwa hoja, huku akifanya rejea kwenye mkataba wenyewe:

1) Kwa nini mkataba huu wa hovyo kwa upande wetu umesainiwa na Rais na kwa kwa upande wa pili haujasainiwa na mkuu wa nchi, bali kampuni?

2) IGA huwa kati ya nchi na nchi, je DP ni nchi?

3) Kama DP siyo nchi, na kama ni kampuni, zabuni ya kumtafuta mwendeshaji ilifuata taratibu na sheria za nchi, au haikufuatwa? Kwa nini?

4) IGA iliyosainiwa ndiyo Master agreement, yaani mkataba mama na mkataba kiongozi, na una nguvu ya kisheria, na hairuhusiwi kuuvunja mpaka DP waridhie, analifahamu hilo?

5) Aeleze, kwa kadiri ya IGA, kuna HGA itakayokuwa na uwezo wa kuikiuka IGA? Na hilo limeandikwa wapi kwenye mkataba uliosainiwa na Rais?

6) Nchi kutoruhusiwa kuingia makubaliano na mwekezaji mwingine yeyote ama kujenga, kuendeleza au kuendesha bandari zingine, haoni kuwa ni kuua sovereignty ya nchi?

7) Sheria zetu za fidia ya ardhi zinatamka wazi kuwa anayehitaji kuitumia ardhi, na ardhi hiyo ikawa inamilikiwa na watu au taasisi nyingine, anayeihitaji ndiye anatakiwa kulipa fidia, lakini IGA inatamka kuwa ardhi yoyote ambayo DP ataihitaji, Serikali ya Tanzania ndiyo itakayowajibika kuwaondoa wamiliki wa ardhi na kuwalipa fidia. Kwa nini sheria zetu zikanyagwe kwa sababu ya DP? Kama sheria ni mbaya, kwa nini haijabadilishwa ili kila mwekezaji akitaka kuwekeza, kazi ya kutafuta ardhi kwaajili ya mwekezaji liwe ni jukumu la Serikali?

8) Nchi yetu imewekeza matrilioni ya pesa katika kuijenga, kuiboresha na kuiendeleza bandari ya Dar es Salaam, Majaliwa aoneshe kwenye mkataba, uwekezaji wetu utatupatia hisa ngapi katika uendeshaji baada ya DP kuwekeza kiasi gani? Lakini akumbuke kuwa mktaba na DP unasema DP atakuwa na umiliki wa 100% katika uendeshaji! Yaani sisi uwekezaji wetu umefanywa kuwa ni 0%. Kama tulichowekeza sisi ni 0%, kwa nini DP asipewe eneo akajenge bandari from scratch?

9) Tatizo kubwa la kukosekana ufanisi katika miradi na mashirika yote yanayosimamiwa na Serikali, iwe ni bandari, TANESCO, mamlaka za maji, ATCL, mahospitali, TBS, n.k. ni uwezo mdogo wa viongozi wa Serikali ambao wameyageuza mashirika haya kuwa sehemu za kuwapachika watu kwa misingi ya itikadi za kisiasa, kufahamiana na undugu, na kisha kiyaingilia katika uendeshaji waje. Je, ina maana kila mahali tutawaweka wawekezaji wa nje? Kwaajili ya ufanisi, kwa nini tusiangalie kwanza msingi na chanzo cha matatizo yote ambayo ni uduni, upeo mdogo, ukosefu wa uadilifu na udhaifu wa uongozi wa nchi yetu kwa muda mrefu? Haoni tunapoteza muda kushughulika na matawi wakati shina na miziz ya mti wenye sumu umebakia kama ulivyo?

10) Ni lini JMT ilitangaza kuwa suala la bandari siyo miongoni mwa mambo ya Muungano? Maana bandari za Zanzibar hazijaingizwa kwenye mkataba huu wa hovyo.

11) Kwa nini Mbarawa, ambaye ni Mzanzibari, amekuwa waziri kwenye wizara isiyo ya Muungano? Kwa nini Aisha ambaye ni Mzanzibari, amekuwa katibu mkuu wa Wizara isiyo ya Muungano?

12) Kwa nini uporaji huu wa rasilimali za Tanganyika umefanyika kipindi ambacho wafanya maamuzi wote ni Wazanzibari, tena wengine, kwa kadiri ya artickes of union, hawakustahili kuwa kwenye nafasi ambazo zimewezesha kuporwa kwa bandari ziluzopo Tanganyika?

NB: MAJALIWA MAJALIWA AFAHAMU KUWA WANANCHI SIYO TU WANASTAHILI KUSIKILIZWA LAKINI NDIO WENYE MAAMUZI YA MWISHO KUHUSU RASILIMALI ZAO.

WANANCHI HAWATAKIWI KUFUATA MAAMUZI YA VIONGOZI BALI VIONGOZI WANATAKIWA KUTII MAAMUZI YA WANANCHI.
Msipoelewa maana ya responsible opposition mtapata tabu sana.
 
Nchi yetu ina bahati mbaya sana kwa kuwakosa viongozi ambao wana uelewa mpana, wanaoyajua mamlaka yao, wanaoelewa vizuri wajibu wao, wanaoelewa vizuri mamlaka yao yanapoishia, na hasa kwa ujumla, viongozi wanaozielewa vizuri sheria zetu na katiba yetu.

Mkataba wa hovyo wa bandari umetufanya tuwafahamu vizuri viongozi wetu ni watu wa namna gani, na zaidi kufahamu dhamira zao, na uduni wa uelewa wao katika masuala mazito ya kitaifa.

Rais hajatamka lolote mpaka sasa, tunamlaumu kwa kusaini mkataba wa hovyo kabisa usiolinda mamlaka ya nchi, uhuru wetu na wa Taifa letu, na kushindwa kufuata taratibu za mikataba. Mikataba ya uwekezaji huwa haisainiwi na Rais wa nchi, lakini kwenye hili la DP, ambayo ni kampuni, amesaini Rais wetu. Kwenye mkataba wa biashara, pande mbili zinazosaini mkataba huwa zenye nafasi sawa. Kwa hiyo Rais wa nchi yetu amejishusha na kuwa sawa na wawakilishi wa kampuni ya DP. Mkataba kwa upande wetu una sahihi ya Rais Samia, kwa upande wa pili hakuna sahihi ya Rais/kiongozi mkuu wa UAE. Rais amidhalilisha nchi.

Makamu wa Rais Dr. Mpango, kwenye hili kaamua kukaa kimya, na kwenye process nzima amejikalia kimya. Lakini kukaa kimya ni automatic submission. Kwa hiyo hapa, inamaanisha Makamu wa Rais amebariki.

Waziri Mkuu, Majaliwa Majaliwa, ambaye ana historia ya kutokuwa mkweli (wakati watu walipokuwa wanahoji kuwa Hayati Magufuli kwa nini hajaonekana kwa muda mrefu, huku kukiwa na tetesi kuwa anaumwa sana, na wengine wakisema amekwishafariki, Majaliwa alijibu kwa kufoka kuwa Rais Magufuli haonekani, wanaouliza walitaka wamwone wapi? Wamwone Kariaokoo sokoni? Akaeleza kuwa Rais Magufuli ni mzima kabisa, yupo ikulu anachapa kazi, wakati tayari Hayati Magufuli alikuwa amekwishafariki), yeye amejitokeza hadharani kuutetea mkataba huo wa hovyo. Ukiutazama mkataba wenyewe, na maneno anayoyatamka Majaliwa, ambayo hayamo kwenye mkataba, unaona wazi kuwa anaendelea na ile historia yake, kama alivyofanya kwenye taarifa kuhusiana na kifo cha Rais Magufuli. Majaliwa, mwishoni anasema kuwa eti wao viongozi wamesikia hofu za wananchi, lakini wananchi wawaamini vjongozi wao. Yaani wananchi wawaamini viongozi ambao wana historia ya kusema uwongo. Yaani wanaanchi waamini porojo za viongozi wakati wakati mkataba wenyewe upo wazi, na wananchi wana uwezo wa kuusoma, na kuuchambua, na tena baadhi ya wananchi hawa wana uelewa mkubwa maradufu ya viongozi wanaotaka waaminiwe wakati hawaaminiki.

Maswali muhimu kuhusiana na mambo ya hovyo yaliyopo kwenye mkataba ule wa hovyo, Majaliwa hajajibu hata moja, halafu anataka watu wamwini! Sisi wananchi hatujawa wajinga wa kiwango hicho.

Majaliwa anatakiwa ajibu kwa hoja, huku akifanya rejea kwenye mkataba wenyewe:

1) Kwa nini mkataba huu wa hovyo kwa upande wetu umesainiwa na Rais na kwa kwa upande wa pili haujasainiwa na mkuu wa nchi, bali kampuni?

2) IGA huwa kati ya nchi na nchi, je DP ni nchi?

3) Kama DP siyo nchi, na kama ni kampuni, zabuni ya kumtafuta mwendeshaji ilifuata taratibu na sheria za nchi, au haikufuatwa? Kwa nini?

4) IGA iliyosainiwa ndiyo Master agreement, yaani mkataba mama na mkataba kiongozi, na una nguvu ya kisheria, na hairuhusiwi kuuvunja mpaka DP waridhie, analifahamu hilo?

5) Aeleze, kwa kadiri ya IGA, kuna HGA itakayokuwa na uwezo wa kuikiuka IGA? Na hilo limeandikwa wapi kwenye mkataba uliosainiwa na Rais?

6) Nchi kutoruhusiwa kuingia makubaliano na mwekezaji mwingine yeyote ama kujenga, kuendeleza au kuendesha bandari zingine, haoni kuwa ni kuua sovereignty ya nchi?

7) Sheria zetu za fidia ya ardhi zinatamka wazi kuwa anayehitaji kuitumia ardhi, na ardhi hiyo ikawa inamilikiwa na watu au taasisi nyingine, anayeihitaji ndiye anatakiwa kulipa fidia, lakini IGA inatamka kuwa ardhi yoyote ambayo DP ataihitaji, Serikali ya Tanzania ndiyo itakayowajibika kuwaondoa wamiliki wa ardhi na kuwalipa fidia. Kwa nini sheria zetu zikanyagwe kwa sababu ya DP? Kama sheria ni mbaya, kwa nini haijabadilishwa ili kila mwekezaji akitaka kuwekeza, kazi ya kutafuta ardhi kwaajili ya mwekezaji liwe ni jukumu la Serikali?

8) Nchi yetu imewekeza matrilioni ya pesa katika kuijenga, kuiboresha na kuiendeleza bandari ya Dar es Salaam, Majaliwa aoneshe kwenye mkataba, uwekezaji wetu utatupatia hisa ngapi katika uendeshaji baada ya DP kuwekeza kiasi gani? Lakini akumbuke kuwa mktaba na DP unasema DP atakuwa na umiliki wa 100% katika uendeshaji! Yaani sisi uwekezaji wetu umefanywa kuwa ni 0%. Kama tulichowekeza sisi ni 0%, kwa nini DP asipewe eneo akajenge bandari from scratch?

9) Tatizo kubwa la kukosekana ufanisi katika miradi na mashirika yote yanayosimamiwa na Serikali, iwe ni bandari, TANESCO, mamlaka za maji, ATCL, mahospitali, TBS, n.k. ni uwezo mdogo wa viongozi wa Serikali ambao wameyageuza mashirika haya kuwa sehemu za kuwapachika watu kwa misingi ya itikadi za kisiasa, kufahamiana na undugu, na kisha kiyaingilia katika uendeshaji waje. Je, ina maana kila mahali tutawaweka wawekezaji wa nje? Kwaajili ya ufanisi, kwa nini tusiangalie kwanza msingi na chanzo cha matatizo yote ambayo ni uduni, upeo mdogo, ukosefu wa uadilifu na udhaifu wa uongozi wa nchi yetu kwa muda mrefu? Haoni tunapoteza muda kushughulika na matawi wakati shina na miziz ya mti wenye sumu umebakia kama ulivyo?

10) Ni lini JMT ilitangaza kuwa suala la bandari siyo miongoni mwa mambo ya Muungano? Maana bandari za Zanzibar hazijaingizwa kwenye mkataba huu wa hovyo.

11) Kwa nini Mbarawa, ambaye ni Mzanzibari, amekuwa waziri kwenye wizara isiyo ya Muungano? Kwa nini Aisha ambaye ni Mzanzibari, amekuwa katibu mkuu wa Wizara isiyo ya Muungano?

12) Kwa nini uporaji huu wa rasilimali za Tanganyika umefanyika kipindi ambacho wafanya maamuzi wote ni Wazanzibari, tena wengine, kwa kadiri ya artickes of union, hawakustahili kuwa kwenye nafasi ambazo zimewezesha kuporwa kwa bandari ziluzopo Tanganyika?

NB: MAJALIWA AFAHAMU KUWA WANANCHI SIYO TU WANASTAHILI KUSIKILIZWA LAKINI NDIO WENYE MAAMUZI YA MWISHO KUHUSU RASILIMALI ZAO.

WANANCHI HAWATAKIWI KUFUATA MAAMUZI YA VIONGOZI BALI VIONGOZI WANATAKIWA KUTII MAAMUZI YA WANANCHI.
Huu mkataba wanaujua waislam peke yao.
 
WANANCHI HAWATAKIWI KUFUATA MAAMUZI YA VIONGOZI BALI VIONGOZI WANATAKIWA KUTII MAAMUZI YA WANANCHI.

Wananchi tunampa mwongozo PM Kassim Majaliwa kiongozi wa shughuli za serikali bungeni, spika wa bunge la muungano, mawaziri, wabunge pamoja na kiongozi mkuu ambaye huwa hashiriki mijadala bungeni kuwa wasome hansard hii :

03 Julai 2017​

Dodoma, Tanzania

Bunge lapitisha Miswada ya sheria za ulinzi wa Maliasili za Taifa​

HOTUBA YA WAZIRI WA SHERIA NA KATIBA MH. PROF. PALAMAGAMBA KABUDI



Hansard :
NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
1
BUNGE LA TANZANIA
____________
MAJADILIANO YA BUNGE
___________
MKUTANO WA SABA
Kikao cha Hamsini na Nane – Tarehe 3 Julai, 2017
(Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi)
D U A
Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua
MWENYEKITI: Tukae, Katibu!
NDG. RAMADHANI ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI:
HATI ZA KUWASILISHA MEZANI:
Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:-
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA:
Maelezo ya Waziri wa Katiba na Sheria kuhusu
Muswada wa Sheria ya Mamlaka na Nchi kuhusiana na Umiliki
wa Maliasili wa Mwaka 2017 [The Natural Wealth and
Resources (Permanent Sovereignty) Bill, 2017]
Maelezo ya Waziri wa Katiba na Sheria kuhusu
Muswada wa Sheria ya Mapitio na Majadiliano kuhusu
masharti Hasi katika Mikataba ya Maliasili za Nchi wa mwaka
2017 (The Natural Wealth and Resources Contracts (Review
and Re-negotiation of Unconscionable Terms) Bill, 2017] ...


NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI:
MISWADA YA SHERIA YA SERIKALI
Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana na
Umiliki wa Maliasili, 2017 (The Natural Wealth and
Resources (Permanent Sovereignty) Bill, 2017)
na
Muswada wa Sheria ya Mapitio na Majadiliano kuhusu
Masharti Hasi katika Mikataba ya Maliasili za Nchi, 2017
(The Natural Wealth and Resources Contracts (Review and
Re-negotiation of Unconscionable Terms) Bill, 2017)
(Kusomwa Mara ya Pili)
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu
Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya 86 ya Kanuni za Kudumu za
Bunge, Toleo la Mwaka 2016, naomba kutoa hoja kwamba
Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana na Umiliki
wa Maliasili wa 2017 (The Natural Wealth and Resources
(Permanent Sovereignty) Bill, 2017) na Muswada wa Sheria ya
Mapitio na Majadiliano kuhusu Masharti Hasi katika Mikataba
inayohusu Maliasili za Nchi, 2017 (The Natural Wealth and
Resources Contracts (Review and Re-negotiation of
Unconscionable Terms) Bill, 2017) sasa usomwe kwa mara ya
pili na Bunge lako Tukufu lijadili na hatimaye lipitishe Miswada
hii na kuwa sehemu ya sheria za nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kabla ya kuwasilisha
maudhui ya Miswada hii, naomba nianze kwa kumshukuru
Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kuturuzuku uhai,
kutujalia afya na kutuwezesha kutekeleza majukumu yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua fursa hii pia
kumshukuru Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa imani kubwa
aliyoonesha kwangu kwa kuniteua kuwa Mbunge na Waziri
wa Katiba na Sheria. (Makofi)...

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya maelezo hayo
ya utangulizi, naomba sasa kutoa maelezo kuhusu Muswada
wa Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana na Umiliki wa
Maliasili wa Mwaka 2017 (The Natural Wealth and Resources
(Permanent Sovereignty) Bill, 2017) na Muswada wa Sheria ya
Mapitio na Majadiliano kuhusu Masharti Hasi katika Mikataba
inayohusu Maliasili za Nchi, 2017 (The Natural Wealth and
Resources Contracts (Review and Re-negotiation of
Unconscionable Terms) Bill, 2017).
Mheshimiwa Naibu Spika, misingi ya Katiba ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania; Muswada wa Sheria ya Mamlaka
ya Nchi kuhusiana na Umiliki wa Maliasili wa 2017
unapendekeza kuweka masharti yanayohusianisha misingi
iliyomo katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
1977, mikataba na misingi ya sheria mbalimbali za Kimataifa
ambazo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inazitambua
na ama imesaini au kuridhia.
Mheshimiwa Naibu Spika, sheria inayopendekezwa
kupitia Muswada huu ina msingi wake katika Ibara ya 8(1) ya
Katiba ambayo inaweka masharti kuwa Tanzania ni nchi
inayozingatia msingi wa demokrasia na haki ya kijamii na
kwa msingi huo, wananchi wake ndio msingi wa mamlaka
yote ya nchi na Serikali inawajibika kwa wananchi wake.
Ibara hiyo inaeleza kama ifuatavyo:-
“Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi
inayofuata misingi ya demokrasia na haki ya kijamii na kwa
hiyo: –
(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka yote na
Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa
wananchi kwa mujibu wa Katiba hii;
(b) lengo kuu la Serikali litakuwa ni ustawi wa
wananchi;
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi;
(d) Wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali
yao kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.” Mwisho wa
kunukuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ujumla, Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania ikiwa ni nchi yenye uhuru kamili ina
haki na mamlaka ya kusimamia maliasili na utajiri wake. Kwa
msingi huo, Serikali inayo wajibu wa kulinda maslahi ya
wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika
mikataba inayoingia kuhusiana na maliasili na utajiri huo
kama inavyoelekezwa katika Ibara ya 27 ya Katiba ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania. Ibara hiyo inaeleza kama
ifuatavyo:-
“(1) Kila mtu ana wajibu wa kulinda mali asilia ya
Jamhuri ya Muungano, mali ya Mamlaka ya Nchi na mali
yote inayomilikiwa kwa pamoja na wananchi, na pia
kuiheshimu mali ya mtu mwingine.
(2) Watu wote watatakiwa na sheria kutunza vizuri mali
ya Mamlaka ya Nchi na ya pamoja, kupiga vita aina zote za
uharibifu na ubadhirifu, na kuendesha uchumi wa Taifa kwa
makini kama watu ambao ndio waamuzi wa hali ya baadaye
ya Taifa lao.”
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingatia misingi hiyo
iliyowekwa na Katiba, Ibara ya 9(1)(c) ya Katiba inaelekeza
kuwa shughuli za Serikali zitekelezwe kwa njia ambazo
zitahakikisha kwamba utajiri wa Taifa unaendelezwa,
unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya wananchi
wote kwa ujumla na pia kuzuia mtu kumnyonya mtu
mwingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, misingi ya maazimio ya
Umoja wa Mataifa; Muswada huu unazingatia uwepo wa
Sheria ya Kimataifa inayotambua haki ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kuhusiana na umiliki wa maliasili.
Aidha, Muswada umezingatia kwamba Tanzania imesaini na
kuridhia mikataba mbalimbali ya Kimataifa ikiwemo Azimio
la Umoja wa Mataifa Namba 523(vi) la tarehe 12 Januari, ..
 
Nchi yetu ina bahati mbaya sana kwa kuwakosa viongozi ambao wana uelewa mpana, wanaoyajua mamlaka yao, wanaoelewa vizuri wajibu wao, wanaoelewa vizuri mamlaka yao yanapoishia, na hasa kwa ujumla, viongozi wanaozielewa vizuri sheria zetu na katiba yetu.

Mkataba wa hovyo wa bandari umetufanya tuwafahamu vizuri viongozi wetu ni watu wa namna gani, na zaidi kufahamu dhamira zao, na uduni wa uelewa wao katika masuala mazito ya kitaifa.

Rais hajatamka lolote mpaka sasa, tunamlaumu kwa kusaini mkataba wa hovyo kabisa usiolinda mamlaka ya nchi, uhuru wetu na wa Taifa letu, na kushindwa kufuata taratibu za mikataba. Mikataba ya uwekezaji huwa haisainiwi na Rais wa nchi, lakini kwenye hili la DP, ambayo ni kampuni, amesaini Rais wetu. Kwenye mkataba wa biashara, pande mbili zinazosaini mkataba huwa zenye nafasi sawa. Kwa hiyo Rais wa nchi yetu amejishusha na kuwa sawa na wawakilishi wa kampuni ya DP. Mkataba kwa upande wetu una sahihi ya Rais Samia, kwa upande wa pili hakuna sahihi ya Rais/kiongozi mkuu wa UAE. Rais amidhalilisha nchi.

Makamu wa Rais Dr. Mpango, kwenye hili kaamua kukaa kimya, na kwenye process nzima amejikalia kimya. Lakini kukaa kimya ni automatic submission. Kwa hiyo hapa, inamaanisha Makamu wa Rais amebariki.

Waziri Mkuu, Majaliwa Majaliwa, ambaye ana historia ya kutokuwa mkweli (wakati watu walipokuwa wanahoji kuwa Hayati Magufuli kwa nini hajaonekana kwa muda mrefu, huku kukiwa na tetesi kuwa anaumwa sana, na wengine wakisema amekwishafariki, Majaliwa alijibu kwa kufoka kuwa Rais Magufuli haonekani, wanaouliza walitaka wamwone wapi? Wamwone Kariaokoo sokoni? Akaeleza kuwa Rais Magufuli ni mzima kabisa, yupo ikulu anachapa kazi, wakati tayari Hayati Magufuli alikuwa amekwishafariki), yeye amejitokeza hadharani kuutetea mkataba huo wa hovyo. Ukiutazama mkataba wenyewe, na maneno anayoyatamka Majaliwa, ambayo hayamo kwenye mkataba, unaona wazi kuwa anaendelea na ile historia yake, kama alivyofanya kwenye taarifa kuhusiana na kifo cha Rais Magufuli. Majaliwa, mwishoni anasema kuwa eti wao viongozi wamesikia hofu za wananchi, lakini wananchi wawaamini vjongozi wao. Yaani wananchi wawaamini viongozi ambao wana historia ya kusema uwongo. Yaani wanaanchi waamini porojo za viongozi wakati wakati mkataba wenyewe upo wazi, na wananchi wana uwezo wa kuusoma, na kuuchambua, na tena baadhi ya wananchi hawa wana uelewa mkubwa maradufu ya viongozi wanaotaka waaminiwe wakati hawaaminiki.

Maswali muhimu kuhusiana na mambo ya hovyo yaliyopo kwenye mkataba ule wa hovyo, Majaliwa hajajibu hata moja, halafu anataka watu wamwini! Sisi wananchi hatujawa wajinga wa kiwango hicho.

Majaliwa anatakiwa ajibu kwa hoja, huku akifanya rejea kwenye mkataba wenyewe:

1) Kwa nini mkataba huu wa hovyo kwa upande wetu umesainiwa na Rais na kwa kwa upande wa pili haujasainiwa na mkuu wa nchi, bali kampuni?

2) IGA huwa kati ya nchi na nchi, je DP ni nchi?

3) Kama DP siyo nchi, na kama ni kampuni, zabuni ya kumtafuta mwendeshaji ilifuata taratibu na sheria za nchi, au haikufuatwa? Kwa nini?

4) IGA iliyosainiwa ndiyo Master agreement, yaani mkataba mama na mkataba kiongozi, na una nguvu ya kisheria, na hairuhusiwi kuuvunja mpaka DP waridhie, analifahamu hilo?

5) Aeleze, kwa kadiri ya IGA, kuna HGA itakayokuwa na uwezo wa kuikiuka IGA? Na hilo limeandikwa wapi kwenye mkataba uliosainiwa na Rais?

6) Nchi kutoruhusiwa kuingia makubaliano na mwekezaji mwingine yeyote ama kujenga, kuendeleza au kuendesha bandari zingine, haoni kuwa ni kuua sovereignty ya nchi?

7) Sheria zetu za fidia ya ardhi zinatamka wazi kuwa anayehitaji kuitumia ardhi, na ardhi hiyo ikawa inamilikiwa na watu au taasisi nyingine, anayeihitaji ndiye anatakiwa kulipa fidia, lakini IGA inatamka kuwa ardhi yoyote ambayo DP ataihitaji, Serikali ya Tanzania ndiyo itakayowajibika kuwaondoa wamiliki wa ardhi na kuwalipa fidia. Kwa nini sheria zetu zikanyagwe kwa sababu ya DP? Kama sheria ni mbaya, kwa nini haijabadilishwa ili kila mwekezaji akitaka kuwekeza, kazi ya kutafuta ardhi kwaajili ya mwekezaji liwe ni jukumu la Serikali?

8) Nchi yetu imewekeza matrilioni ya pesa katika kuijenga, kuiboresha na kuiendeleza bandari ya Dar es Salaam, Majaliwa aoneshe kwenye mkataba, uwekezaji wetu utatupatia hisa ngapi katika uendeshaji baada ya DP kuwekeza kiasi gani? Lakini akumbuke kuwa mktaba na DP unasema DP atakuwa na umiliki wa 100% katika uendeshaji! Yaani sisi uwekezaji wetu umefanywa kuwa ni 0%. Kama tulichowekeza sisi ni 0%, kwa nini DP asipewe eneo akajenge bandari from scratch?

9) Tatizo kubwa la kukosekana ufanisi katika miradi na mashirika yote yanayosimamiwa na Serikali, iwe ni bandari, TANESCO, mamlaka za maji, ATCL, mahospitali, TBS, n.k. ni uwezo mdogo wa viongozi wa Serikali ambao wameyageuza mashirika haya kuwa sehemu za kuwapachika watu kwa misingi ya itikadi za kisiasa, kufahamiana na undugu, na kisha kiyaingilia katika uendeshaji waje. Je, ina maana kila mahali tutawaweka wawekezaji wa nje? Kwaajili ya ufanisi, kwa nini tusiangalie kwanza msingi na chanzo cha matatizo yote ambayo ni uduni, upeo mdogo, ukosefu wa uadilifu na udhaifu wa uongozi wa nchi yetu kwa muda mrefu? Haoni tunapoteza muda kushughulika na matawi wakati shina na miziz ya mti wenye sumu umebakia kama ulivyo?

10) Ni lini JMT ilitangaza kuwa suala la bandari siyo miongoni mwa mambo ya Muungano? Maana bandari za Zanzibar hazijaingizwa kwenye mkataba huu wa hovyo.

11) Kwa nini Mbarawa, ambaye ni Mzanzibari, amekuwa waziri kwenye wizara isiyo ya Muungano? Kwa nini Aisha ambaye ni Mzanzibari, amekuwa katibu mkuu wa Wizara isiyo ya Muungano?

12) Kwa nini uporaji huu wa rasilimali za Tanganyika umefanyika kipindi ambacho wafanya maamuzi wote ni Wazanzibari, tena wengine, kwa kadiri ya artickes of union, hawakustahili kuwa kwenye nafasi ambazo zimewezesha kuporwa kwa bandari ziluzopo Tanganyika?

NB: MAJALIWA AFAHAMU KUWA WANANCHI SIYO TU WANASTAHILI KUSIKILIZWA LAKINI NDIO WENYE MAAMUZI YA MWISHO KUHUSU RASILIMALI ZAO.

WANANCHI HAWATAKIWI KUFUATA MAAMUZI YA VIONGOZI BALI VIONGOZI WANATAKIWA KUTII MAAMUZI YA WANANCHI.
Kwenye hili la bandari anchorman ni kweli ana maanisha?
 
Wananchi tunampa mwongozo PM Kassim Majaliwa, mawaziri pamoja na kiongozi mkuu kuwa wasome hansard hii :

03 Julai 2017​

Dodoma, Tanzania

Bunge lapitisha Miswada ya sheria za ulinzi wa Maliasili za Taifa​

HOTUBA YA WAZIRI WA SHERIA NA KATIBA MH. PROF. PALAMAGAMBA KABUDI



Hansard :
NAKALA YA MTANDAO(ONLINE DOCUMENT)
1
BUNGE LA TANZANIA
____________
MAJADILIANO YA BUNGE
___________
MKUTANO WA SABA
Kikao cha Hamsini na Nane – Tarehe 3 Julai, 2017
(Bunge Lilianza Saa Tatu Asubuhi)
D U A
Naibu Spika (Mhe. Dkt. Tulia Ackson) Alisoma Dua
MWENYEKITI: Tukae, Katibu!
NDG. RAMADHANI ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI:
HATI ZA KUWASILISHA MEZANI:
Hati zifuatazo ziliwasilishwa mezani na:-
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA:
Maelezo ya Waziri wa Katiba na Sheria kuhusu
Muswada wa Sheria ya Mamlaka na Nchi kuhusiana na Umiliki
wa Maliasili wa Mwaka 2017 [The Natural Wealth and
Resources (Permanent Sovereignty) Bill, 2017]
Maelezo ya Waziri wa Katiba na Sheria kuhusu
Muswada wa Sheria ya Mapitio na Majadiliano kuhusu
masharti Hasi katika Mikataba ya Maliasili za Nchi wa mwaka
2017 (The Natural Wealth and Resources Contracts (Review
and Re-negotiation of Unconscionable Terms) Bill, 2017] ...


NDG. RAMADHAN ISSA ABDALLAH – KATIBU MEZANI:
MISWADA YA SHERIA YA SERIKALI
Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana na
Umiliki wa Maliasili, 2017 (The Natural Wealth and
Resources (Permanent Sovereignty) Bill, 2017)
na
Muswada wa Sheria ya Mapitio na Majadiliano kuhusu
Masharti Hasi katika Mikataba ya Maliasili za Nchi, 2017
(The Natural Wealth and Resources Contracts (Review and
Re-negotiation of Unconscionable Terms) Bill, 2017)
(Kusomwa Mara ya Pili)
WAZIRI WA KATIBA NA SHERIA: Mheshimiwa Naibu
Spika, kwa mujibu wa Kanuni ya 86 ya Kanuni za Kudumu za
Bunge, Toleo la Mwaka 2016, naomba kutoa hoja kwamba
Muswada wa Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana na Umiliki
wa Maliasili wa 2017 (The Natural Wealth and Resources
(Permanent Sovereignty) Bill, 2017) na Muswada wa Sheria ya
Mapitio na Majadiliano kuhusu Masharti Hasi katika Mikataba
inayohusu Maliasili za Nchi, 2017 (The Natural Wealth and
Resources Contracts (Review and Re-negotiation of
Unconscionable Terms) Bill, 2017) sasa usomwe kwa mara ya
pili na Bunge lako Tukufu lijadili na hatimaye lipitishe Miswada
hii na kuwa sehemu ya sheria za nchi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kabla ya kuwasilisha
maudhui ya Miswada hii, naomba nianze kwa kumshukuru
Mwenyezi Mungu, mwingi wa rehema kwa kuturuzuku uhai,
kutujalia afya na kutuwezesha kutekeleza majukumu yetu.
Mheshimiwa Naibu Spika, nachukua fursa hii pia
kumshukuru Mheshimiwa Dkt. John Pombe Joseph Magufuli,
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa imani kubwa
aliyoonesha kwangu kwa kuniteua kuwa Mbunge na Waziri
wa Katiba na Sheria. (Makofi)...

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya maelezo hayo
ya utangulizi, naomba sasa kutoa maelezo kuhusu Muswada
wa Sheria ya Mamlaka ya Nchi kuhusiana na Umiliki wa
Maliasili wa Mwaka 2017 (The Natural Wealth and Resources
(Permanent Sovereignty) Bill, 2017) na Muswada wa Sheria ya
Mapitio na Majadiliano kuhusu Masharti Hasi katika Mikataba
inayohusu Maliasili za Nchi, 2017 (The Natural Wealth and
Resources Contracts (Review and Re-negotiation of
Unconscionable Terms) Bill, 2017).
Mheshimiwa Naibu Spika, misingi ya Katiba ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania; Muswada wa Sheria ya Mamlaka
ya Nchi kuhusiana na Umiliki wa Maliasili wa 2017
unapendekeza kuweka masharti yanayohusianisha misingi
iliyomo katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
1977, mikataba na misingi ya sheria mbalimbali za Kimataifa
ambazo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inazitambua
na ama imesaini au kuridhia.
Mheshimiwa Naibu Spika, sheria inayopendekezwa
kupitia Muswada huu ina msingi wake katika Ibara ya 8(1) ya
Katiba ambayo inaweka masharti kuwa Tanzania ni nchi
inayozingatia msingi wa demokrasia na haki ya kijamii na
kwa msingi huo, wananchi wake ndio msingi wa mamlaka
yote ya nchi na Serikali inawajibika kwa wananchi wake.
Ibara hiyo inaeleza kama ifuatavyo:-
“Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ni nchi
inayofuata misingi ya demokrasia na haki ya kijamii na kwa
hiyo: –
(a) wananchi ndio msingi wa mamlaka yote na
Serikali itapata madaraka na mamlaka yake yote kutoka kwa
wananchi kwa mujibu wa Katiba hii;
(b) lengo kuu la Serikali litakuwa ni ustawi wa
wananchi;
(c) Serikali itawajibika kwa wananchi;
(d) Wananchi watashiriki katika shughuli za Serikali
yao kwa mujibu wa masharti ya Katiba hii.” Mwisho wa
kunukuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa ujumla, Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania ikiwa ni nchi yenye uhuru kamili ina
haki na mamlaka ya kusimamia maliasili na utajiri wake. Kwa
msingi huo, Serikali inayo wajibu wa kulinda maslahi ya
wananchi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika
mikataba inayoingia kuhusiana na maliasili na utajiri huo
kama inavyoelekezwa katika Ibara ya 27 ya Katiba ya Jamhuri
ya Muungano wa Tanzania. Ibara hiyo inaeleza kama
ifuatavyo:-
“(1) Kila mtu ana wajibu wa kulinda mali asilia ya
Jamhuri ya Muungano, mali ya Mamlaka ya Nchi na mali
yote inayomilikiwa kwa pamoja na wananchi, na pia
kuiheshimu mali ya mtu mwingine.
(2) Watu wote watatakiwa na sheria kutunza vizuri mali
ya Mamlaka ya Nchi na ya pamoja, kupiga vita aina zote za
uharibifu na ubadhirifu, na kuendesha uchumi wa Taifa kwa
makini kama watu ambao ndio waamuzi wa hali ya baadaye
ya Taifa lao.”
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuzingatia misingi hiyo
iliyowekwa na Katiba, Ibara ya 9(1)(c) ya Katiba inaelekeza
kuwa shughuli za Serikali zitekelezwe kwa njia ambazo
zitahakikisha kwamba utajiri wa Taifa unaendelezwa,
unahifadhiwa na unatumiwa kwa manufaa ya wananchi
wote kwa ujumla na pia kuzuia mtu kumnyonya mtu
mwingine.
Mheshimiwa Naibu Spika, misingi ya maazimio ya
Umoja wa Mataifa; Muswada huu unazingatia uwepo wa
Sheria ya Kimataifa inayotambua haki ya Jamhuri ya
Muungano wa Tanzania kuhusiana na umiliki wa maliasili.
Aidha, Muswada umezingatia kwamba Tanzania imesaini na
kuridhia mikataba mbalimbali ya Kimataifa ikiwemo Azimio
la Umoja wa Mataifa Namba 523(vi) la tarehe 12 Januari, ..
Jamaa wakianza kusoma wakifika tu kwenye hizi mambo wanapata usingizi., kwa sas hakuna aliyeko kwa sirikali anayeweza kusema jambo tukaamin kasema vyema, yaani wote sanaa sanaaa sanaaaa tupu
 
Kitendo cha PM kuendelea kurudia majibu yake ya uongo kwetu kila wakati sijui anatuonaje?

Namuona kama kiongozi aliyechoka kujilindia heshima yake sasa ameamua liwalo na liwe, sijui kwanini muda anaotumia kutudanganya asingemweleza Samia madhara ya uwekezaji wa kihuni alioruhusu ufanyike unaohatarisha uhai wa Tanganyika yetu.
 
Nchi yetu ina bahati mbaya sana kwa kuwakosa viongozi ambao wana uelewa mpana, wanaoyajua mamlaka yao, wanaoelewa vizuri wajibu wao, wanaoelewa vizuri mamlaka yao yanapoishia, na hasa kwa ujumla, viongozi wanaozielewa vizuri sheria zetu na katiba yetu.

Mkataba wa hovyo wa bandari umetufanya tuwafahamu vizuri viongozi wetu ni watu wa namna gani, na zaidi kufahamu dhamira zao, na uduni wa uelewa wao katika masuala mazito ya kitaifa.

Rais hajatamka lolote mpaka sasa, tunamlaumu kwa kusaini mkataba wa hovyo kabisa usiolinda mamlaka ya nchi, uhuru wetu na wa Taifa letu, na kushindwa kufuata taratibu za mikataba. Mikataba ya uwekezaji huwa haisainiwi na Rais wa nchi, lakini kwenye hili la DP, ambayo ni kampuni, amesaini Rais wetu. Kwenye mkataba wa biashara, pande mbili zinazosaini mkataba huwa zenye nafasi sawa. Kwa hiyo Rais wa nchi yetu amejishusha na kuwa sawa na wawakilishi wa kampuni ya DP. Mkataba kwa upande wetu una sahihi ya Rais Samia, kwa upande wa pili hakuna sahihi ya Rais/kiongozi mkuu wa UAE. Rais amidhalilisha nchi.

Makamu wa Rais Dr. Mpango, kwenye hili kaamua kukaa kimya, na kwenye process nzima amejikalia kimya. Lakini kukaa kimya ni automatic submission. Kwa hiyo hapa, inamaanisha Makamu wa Rais amebariki.

Waziri Mkuu, Majaliwa Majaliwa, ambaye ana historia ya kutokuwa mkweli (wakati watu walipokuwa wanahoji kuwa Hayati Magufuli kwa nini hajaonekana kwa muda mrefu, huku kukiwa na tetesi kuwa anaumwa sana, na wengine wakisema amekwishafariki, Majaliwa alijibu kwa kufoka kuwa Rais Magufuli haonekani, wanaouliza walitaka wamwone wapi? Wamwone Kariaokoo sokoni? Akaeleza kuwa Rais Magufuli ni mzima kabisa, yupo ikulu anachapa kazi, wakati tayari Hayati Magufuli alikuwa amekwishafariki), yeye amejitokeza hadharani kuutetea mkataba huo wa hovyo. Ukiutazama mkataba wenyewe, na maneno anayoyatamka Majaliwa, ambayo hayamo kwenye mkataba, unaona wazi kuwa anaendelea na ile historia yake, kama alivyofanya kwenye taarifa kuhusiana na kifo cha Rais Magufuli. Majaliwa, mwishoni anasema kuwa eti wao viongozi wamesikia hofu za wananchi, lakini wananchi wawaamini vjongozi wao. Yaani wananchi wawaamini viongozi ambao wana historia ya kusema uwongo. Yaani wanaanchi waamini porojo za viongozi wakati wakati mkataba wenyewe upo wazi, na wananchi wana uwezo wa kuusoma, na kuuchambua, na tena baadhi ya wananchi hawa wana uelewa mkubwa maradufu ya viongozi wanaotaka waaminiwe wakati hawaaminiki.

Maswali muhimu kuhusiana na mambo ya hovyo yaliyopo kwenye mkataba ule wa hovyo, Majaliwa hajajibu hata moja, halafu anataka watu wamwini! Sisi wananchi hatujawa wajinga wa kiwango hicho.

Majaliwa anatakiwa ajibu kwa hoja, huku akifanya rejea kwenye mkataba wenyewe:

1) Kwa nini mkataba huu wa hovyo kwa upande wetu umesainiwa na Rais na kwa kwa upande wa pili haujasainiwa na mkuu wa nchi, bali kampuni?

2) IGA huwa kati ya nchi na nchi, je DP ni nchi?

3) Kama DP siyo nchi, na kama ni kampuni, zabuni ya kumtafuta mwendeshaji ilifuata taratibu na sheria za nchi, au haikufuatwa? Kwa nini?

4) IGA iliyosainiwa ndiyo Master agreement, yaani mkataba mama na mkataba kiongozi, na una nguvu ya kisheria, na hairuhusiwi kuuvunja mpaka DP waridhie, analifahamu hilo?

5) Aeleze, kwa kadiri ya IGA, kuna HGA itakayokuwa na uwezo wa kuikiuka IGA? Na hilo limeandikwa wapi kwenye mkataba uliosainiwa na Rais?

6) Nchi kutoruhusiwa kuingia makubaliano na mwekezaji mwingine yeyote ama kujenga, kuendeleza au kuendesha bandari zingine, haoni kuwa ni kuua sovereignty ya nchi?

7) Sheria zetu za fidia ya ardhi zinatamka wazi kuwa anayehitaji kuitumia ardhi, na ardhi hiyo ikawa inamilikiwa na watu au taasisi nyingine, anayeihitaji ndiye anatakiwa kulipa fidia, lakini IGA inatamka kuwa ardhi yoyote ambayo DP ataihitaji, Serikali ya Tanzania ndiyo itakayowajibika kuwaondoa wamiliki wa ardhi na kuwalipa fidia. Kwa nini sheria zetu zikanyagwe kwa sababu ya DP? Kama sheria ni mbaya, kwa nini haijabadilishwa ili kila mwekezaji akitaka kuwekeza, kazi ya kutafuta ardhi kwaajili ya mwekezaji liwe ni jukumu la Serikali?

8) Nchi yetu imewekeza matrilioni ya pesa katika kuijenga, kuiboresha na kuiendeleza bandari ya Dar es Salaam, Majaliwa aoneshe kwenye mkataba, uwekezaji wetu utatupatia hisa ngapi katika uendeshaji baada ya DP kuwekeza kiasi gani? Lakini akumbuke kuwa mktaba na DP unasema DP atakuwa na umiliki wa 100% katika uendeshaji! Yaani sisi uwekezaji wetu umefanywa kuwa ni 0%. Kama tulichowekeza sisi ni 0%, kwa nini DP asipewe eneo akajenge bandari from scratch?

9) Tatizo kubwa la kukosekana ufanisi katika miradi na mashirika yote yanayosimamiwa na Serikali, iwe ni bandari, TANESCO, mamlaka za maji, ATCL, mahospitali, TBS, n.k. ni uwezo mdogo wa viongozi wa Serikali ambao wameyageuza mashirika haya kuwa sehemu za kuwapachika watu kwa misingi ya itikadi za kisiasa, kufahamiana na undugu, na kisha kiyaingilia katika uendeshaji waje. Je, ina maana kila mahali tutawaweka wawekezaji wa nje? Kwaajili ya ufanisi, kwa nini tusiangalie kwanza msingi na chanzo cha matatizo yote ambayo ni uduni, upeo mdogo, ukosefu wa uadilifu na udhaifu wa uongozi wa nchi yetu kwa muda mrefu? Haoni tunapoteza muda kushughulika na matawi wakati shina na miziz ya mti wenye sumu umebakia kama ulivyo?

10) Ni lini JMT ilitangaza kuwa suala la bandari siyo miongoni mwa mambo ya Muungano? Maana bandari za Zanzibar hazijaingizwa kwenye mkataba huu wa hovyo.

11) Kwa nini Mbarawa, ambaye ni Mzanzibari, amekuwa waziri kwenye wizara isiyo ya Muungano? Kwa nini Aisha ambaye ni Mzanzibari, amekuwa katibu mkuu wa Wizara isiyo ya Muungano?

12) Kwa nini uporaji huu wa rasilimali za Tanganyika umefanyika kipindi ambacho wafanya maamuzi wote ni Wazanzibari, tena wengine, kwa kadiri ya artickes of union, hawakustahili kuwa kwenye nafasi ambazo zimewezesha kuporwa kwa bandari ziluzopo Tanganyika?

NB: MAJALIWA AFAHAMU KUWA WANANCHI SIYO TU WANASTAHILI KUSIKILIZWA LAKINI NDIO WENYE MAAMUZI YA MWISHO KUHUSU RASILIMALI ZAO.

WANANCHI HAWATAKIWI KUFUATA MAAMUZI YA VIONGOZI BALI VIONGOZI WANATAKIWA KUTII MAAMUZI YA WANANCHI.
Naona umeamua kujifariji Leo. Hivi Bado hamjakubali tu kwamba madili na ufisadi wenu wa bandarini umefika kikomo? Tafuteni kazi zingine ambacho mtakula kwa urefu wa kamba zenu
 
Sovereignty : Adelardus Kilangi on the Principle of Permanent Sovereignty Over Natural Resources


Adelardus Kilangi on the will of States to own the principle of permanent sovereignty over their natural resources ...

To Watch Full video of the presentation presentation / lecture click:

1688812823223.png
 
Naona umeamua kujifariji Leo. Hivi Bado hamjakubali tu kwamba madili na ufisadi wenu wa bandarini umefika kikomo? Tafuteni kazi zingine ambacho mtakula kwa urefu wa kamba zenu
Ni wapi hapa Tanzania ambapo uwekezaji umefanyika na hakuna ufisadi? au DPW ndiyo itakuwa uwekezaji wa kwanza hapa nchini.
 
Ni wapi hapa Tanzania ambapo uwekezaji umefanyika na hakuna ufisadi? au DPW ndiyo itakuwa uwekezaji wa kwanza hapa nchini.
Bora waibe wao au waibiane wao sisi hayaruhusu mana kutakuwa fixed Kodi tinayoipata kutoka kwao regardless kuibiana kwao kuliko tuibiane sisi kwa sisi na Kodi haifiko sehemu husika
 
Bora waibe wao au waibiane wao sisi hayaruhusu mana kutakuwa fixed Kodi tinayoipata kutoka kwao regardless kuibiana kwao kuliko tuibiane sisi kwa sisi na Kodi haifiko sehemu husika
Wewe unaweza kuwa siyo sawa ki akili. Kampuni inalipa kodi baada ya kutangaza kupata faida. Sasa wakishaibiana wanatangaza hasara, hiyo fixed kodi unakwenda kuipatia wapi? Au na wewe ni bendera fuata upepo. Uliwahi kuona fixed kodi wapi kwenye hizo mikataba mnaoingia kama vipofu.
 
Nchi yetu ina bahati mbaya sana kwa kuwakosa viongozi ambao wana uelewa mpana, wanaoyajua mamlaka yao, wanaoelewa vizuri wajibu wao, wanaoelewa vizuri mamlaka yao yanapoishia, na hasa kwa ujumla, viongozi wanaozielewa vizuri sheria zetu na katiba yetu.

Mkataba wa hovyo wa bandari umetufanya tuwafahamu vizuri viongozi wetu ni watu wa namna gani, na zaidi kufahamu dhamira zao, na uduni wa uelewa wao katika masuala mazito ya kitaifa.

Rais hajatamka lolote mpaka sasa, tunamlaumu kwa kusaini mkataba wa hovyo kabisa usiolinda mamlaka ya nchi, uhuru wetu na wa Taifa letu, na kushindwa kufuata taratibu za mikataba. Mikataba ya uwekezaji huwa haisainiwi na Rais wa nchi, lakini kwenye hili la DP, ambayo ni kampuni, amesaini Rais wetu. Kwenye mkataba wa biashara, pande mbili zinazosaini mkataba huwa zenye nafasi sawa. Kwa hiyo Rais wa nchi yetu amejishusha na kuwa sawa na wawakilishi wa kampuni ya DP. Mkataba kwa upande wetu una sahihi ya Rais Samia, kwa upande wa pili hakuna sahihi ya Rais/kiongozi mkuu wa UAE. Rais amidhalilisha nchi.

Makamu wa Rais Dr. Mpango, kwenye hili kaamua kukaa kimya, na kwenye process nzima amejikalia kimya. Lakini kukaa kimya ni automatic submission. Kwa hiyo hapa, inamaanisha Makamu wa Rais amebariki.

Waziri Mkuu, Majaliwa Majaliwa, ambaye ana historia ya kutokuwa mkweli (wakati watu walipokuwa wanahoji kuwa Hayati Magufuli kwa nini hajaonekana kwa muda mrefu, huku kukiwa na tetesi kuwa anaumwa sana, na wengine wakisema amekwishafariki, Majaliwa alijibu kwa kufoka kuwa Rais Magufuli haonekani, wanaouliza walitaka wamwone wapi? Wamwone Kariaokoo sokoni? Akaeleza kuwa Rais Magufuli ni mzima kabisa, yupo ikulu anachapa kazi, wakati tayari Hayati Magufuli alikuwa amekwishafariki), yeye amejitokeza hadharani kuutetea mkataba huo wa hovyo. Ukiutazama mkataba wenyewe, na maneno anayoyatamka Majaliwa, ambayo hayamo kwenye mkataba, unaona wazi kuwa anaendelea na ile historia yake, kama alivyofanya kwenye taarifa kuhusiana na kifo cha Rais Magufuli. Majaliwa, mwishoni anasema kuwa eti wao viongozi wamesikia hofu za wananchi, lakini wananchi wawaamini vjongozi wao. Yaani wananchi wawaamini viongozi ambao wana historia ya kusema uwongo. Yaani wanaanchi waamini porojo za viongozi wakati wakati mkataba wenyewe upo wazi, na wananchi wana uwezo wa kuusoma, na kuuchambua, na tena baadhi ya wananchi hawa wana uelewa mkubwa maradufu ya viongozi wanaotaka waaminiwe wakati hawaaminiki.

Maswali muhimu kuhusiana na mambo ya hovyo yaliyopo kwenye mkataba ule wa hovyo, Majaliwa hajajibu hata moja, halafu anataka watu wamwini! Sisi wananchi hatujawa wajinga wa kiwango hicho.

Majaliwa anatakiwa ajibu kwa hoja, huku akifanya rejea kwenye mkataba wenyewe:

1) Kwa nini mkataba huu wa hovyo kwa upande wetu umesainiwa na Rais na kwa kwa upande wa pili haujasainiwa na mkuu wa nchi, bali kampuni?

2) IGA huwa kati ya nchi na nchi, je DP ni nchi?

3) Kama DP siyo nchi, na kama ni kampuni, zabuni ya kumtafuta mwendeshaji ilifuata taratibu na sheria za nchi, au haikufuatwa? Kwa nini?

4) IGA iliyosainiwa ndiyo Master agreement, yaani mkataba mama na mkataba kiongozi, na una nguvu ya kisheria, na hairuhusiwi kuuvunja mpaka DP waridhie, analifahamu hilo?

5) Aeleze, kwa kadiri ya IGA, kuna HGA itakayokuwa na uwezo wa kuikiuka IGA? Na hilo limeandikwa wapi kwenye mkataba uliosainiwa na Rais?

6) Nchi kutoruhusiwa kuingia makubaliano na mwekezaji mwingine yeyote ama kujenga, kuendeleza au kuendesha bandari zingine, haoni kuwa ni kuua sovereignty ya nchi?

7) Sheria zetu za fidia ya ardhi zinatamka wazi kuwa anayehitaji kuitumia ardhi, na ardhi hiyo ikawa inamilikiwa na watu au taasisi nyingine, anayeihitaji ndiye anatakiwa kulipa fidia, lakini IGA inatamka kuwa ardhi yoyote ambayo DP ataihitaji, Serikali ya Tanzania ndiyo itakayowajibika kuwaondoa wamiliki wa ardhi na kuwalipa fidia. Kwa nini sheria zetu zikanyagwe kwa sababu ya DP? Kama sheria ni mbaya, kwa nini haijabadilishwa ili kila mwekezaji akitaka kuwekeza, kazi ya kutafuta ardhi kwaajili ya mwekezaji liwe ni jukumu la Serikali?

8) Nchi yetu imewekeza matrilioni ya pesa katika kuijenga, kuiboresha na kuiendeleza bandari ya Dar es Salaam, Majaliwa aoneshe kwenye mkataba, uwekezaji wetu utatupatia hisa ngapi katika uendeshaji baada ya DP kuwekeza kiasi gani? Lakini akumbuke kuwa mktaba na DP unasema DP atakuwa na umiliki wa 100% katika uendeshaji! Yaani sisi uwekezaji wetu umefanywa kuwa ni 0%. Kama tulichowekeza sisi ni 0%, kwa nini DP asipewe eneo akajenge bandari from scratch?

9) Tatizo kubwa la kukosekana ufanisi katika miradi na mashirika yote yanayosimamiwa na Serikali, iwe ni bandari, TANESCO, mamlaka za maji, ATCL, mahospitali, TBS, n.k. ni uwezo mdogo wa viongozi wa Serikali ambao wameyageuza mashirika haya kuwa sehemu za kuwapachika watu kwa misingi ya itikadi za kisiasa, kufahamiana na undugu, na kisha kiyaingilia katika uendeshaji waje. Je, ina maana kila mahali tutawaweka wawekezaji wa nje? Kwaajili ya ufanisi, kwa nini tusiangalie kwanza msingi na chanzo cha matatizo yote ambayo ni uduni, upeo mdogo, ukosefu wa uadilifu na udhaifu wa uongozi wa nchi yetu kwa muda mrefu? Haoni tunapoteza muda kushughulika na matawi wakati shina na miziz ya mti wenye sumu umebakia kama ulivyo?

10) Ni lini JMT ilitangaza kuwa suala la bandari siyo miongoni mwa mambo ya Muungano? Maana bandari za Zanzibar hazijaingizwa kwenye mkataba huu wa hovyo.

11) Kwa nini Mbarawa, ambaye ni Mzanzibari, amekuwa waziri kwenye wizara isiyo ya Muungano? Kwa nini Aisha ambaye ni Mzanzibari, amekuwa katibu mkuu wa Wizara isiyo ya Muungano?

12) Kwa nini uporaji huu wa rasilimali za Tanganyika umefanyika kipindi ambacho wafanya maamuzi wote ni Wazanzibari, tena wengine, kwa kadiri ya artickes of union, hawakustahili kuwa kwenye nafasi ambazo zimewezesha kuporwa kwa bandari ziluzopo Tanganyika?

NB: MAJALIWA AFAHAMU KUWA WANANCHI SIYO TU WANASTAHILI KUSIKILIZWA LAKINI NDIO WENYE MAAMUZI YA MWISHO KUHUSU RASILIMALI ZAO.

WANANCHI HAWATAKIWI KUFUATA MAAMUZI YA VIONGOZI BALI VIONGOZI WANATAKIWA KUTII MAAMUZI YA WANANCHI.
Loo umeandika kwa hisia kali sana na ni ukweli mtupu.
 
Back
Top Bottom