Waziri, Mhe. Dkt. Ndumbaro Awataka Wahitimu Kutumia Elimu Zao Kusaidia Jamii

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
May 16, 2020
1,900
944
Waziri, Mhe. Dkt. Ndumbaro Awataka Wahitimu Kutumia Elimu Zao Kusaidia Jamii

Waziri wa Utamaduni Sanaa na Michezo, Dk Damas Ndumbaro amewataka wahitimu wa mahafali ya 42 ya Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kuitumia elimu waliyoipata kufanya tafiti zitakazosaidia kutatua changamoto za jamii zinazowazunguka kupitia maeneo yao ya kazi ama makazi.

Dk Ndumbaro, ametoa rai hiyo Disemba 14, 2023 katika Uwanja wa Majimaji uliopo manispaa ya Songea mkoani Ruvuma, alipohudhuria mahafali hayo kama mgeni rasmi.

“Mlichopata hapa siyo cheti, bali ni elimu ambayo ili iwe na manufaa inabidi mkaitumie kutatua changamoto zilizopo katika jamii kwa kuisaidia na kufanya tafiti zenye tija. Wakati tunaelekea kupata dira mpya ya taifa ya mwaka 2025, katumieni elimu mliyopata kutoa maoni, uzoefu na maono yenu kupitia mijadala itakayowezesha kupata dira makini kwa taifa letu.

Pia, mnapaswa kutumia ujuzi na maarifa mliyopata kuwa wabunifu wa kuziona fursa na kuzichangamkia ili kuzalisha ajira kwa vijana na jamii kwa jumla,” amesema Dk Ndumbaro.

Aidha, amekitaka Chuo Kikuu Huria cha Tanzania kuutumia upekee wake kueneza na kukuza Kiswahili ulimwenguni, vilevile, ametoa rai kwa chuo kushirikiana na Baraza la Kiswahili la Taifa kuhakikisha ufundishaji wa Kiswahili kwa wageni ndani na nje ya nchi unafanikiwa ili kuendana na ajenda mahsusi ya taifa ya kukuza, kueneza na kubidhaisha lugha hiyo katika Bara la Afrika na duniani kwa jumla.
 

Attachments

  • GBUuzbzWkAAwS43.jpg
    GBUuzbzWkAAwS43.jpg
    179.1 KB · Views: 1
  • GBUu0OUXUAAfAWV.jpg
    GBUu0OUXUAAfAWV.jpg
    83.2 KB · Views: 2
  • GBUu0eMW4AAaAvs.jpg
    GBUu0eMW4AAaAvs.jpg
    128.9 KB · Views: 2
  • GBUu1GyWQAAHXcX.jpg
    GBUu1GyWQAAHXcX.jpg
    240.9 KB · Views: 2
Waliomaliza kabla yao ,usomi wao haujaleta positive impact kwenye matatizo yanayoikumba jamii, iweje wao au kimebadilika nini kuwatofautisha na wengine?Ni dhahiri mfumo wa elimu wa nchi hii ni outdated na haufai tena kuutegemea kwamba utaleta suluhu kwenye changamoto za kijamii bali unaongeza changamoto. Waziri hajui anachokiongea ama anaongea kwa mazoea.
 
Back
Top Bottom