Waziri Membe jiandae kukanusha

Waziri Membe jiandae kukanusha

waandishi wetu wapo bize na kambi za urais ndugu

Siyo hilo na WAPINZANI wako wapi tuwaandike kwa maovu.Hebu tuliangalie UHURU na Daily news,hili la kwanza ni gazeti la chama hata siku moja sijawahi kuona wameandika mabaya yanayoihusu serikali ,wameshindwa kabisa kuchanganua kuwa wao ni chama na kama gazeti la chama lingekuwa busy kuya andika maovu au mabaya yanayofanyika serikalini ili kuwapigia filimbi watendaji walioko ndani ya chama.

Ukiangalia DAILY news lenyewe ni gazeti la serikali lakini lipo busy kuandika habari za chama na kuacha habari za kitaifa.Mfano lingekuwa busy kutafuta reports zinazohusu IPTL ili kuistua serikali.
 
Nazungumza nawe Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Benard Camilius Membe. Umekuwa na ari kubwa kukanusha kila suala la Tanzania linalojichomoza kimataifa. Unakanusha kila jambo hasa litangazwalo na vyombo vya habari vya kimataifa.

Ulianza na suala la Malawi kuhusu mpaka wa Ziwa Nyasa. Ukafuata suala la Balozi wa China aliyepanda jukwaa la CCM na kuhutubu. Tena,ukakanusha kuhusu ndege ya Rais wa China kubeba pembe za ndovu. Serikali yako pia ilikanusha kwa nguvu filamu ya Nightmare na uwindaji haramu.

Kubwa linaloisukuma Serikali ni kutangazwa habari zetu nje. Inadaiwa kuwa vyombo vya nje vinatuchafua na vina wivu. Sasa,nina taarifa kuwa kuna waandishi wa kimataifa wametinga Kiteto kurekodi dhahama ya kule. Wanatengeneza Documentary juu ya mauaji yanayoendelea Kiteto kati ya wakulima na wafugaji.

Wameshaanza kazi. Wanaendelea. Wakimaliza watatangaza mauaji hayo katika vyombo mbalimbali vya kimataifa vya habari kwa njia ya sauti na video. Nakuomba Waziri Membe uandae kanusho. Utalitumia punde. Usichelewe.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
You have nothing between your ears. Hatuwezi kujadili stories ambazo ni speculative. Hizo chenji za waliokutuma zitumikie kwa namna nyingine siyo kutuletea stori makengeza.
 
.......hiyo ni post ya kukanusha ukweli kwani nyie hamjui????????
 
Aanze kukanusha kabla hawajaitoa... ili kuwa pre-empty
 
Membe alishakanusha BBC wakati wa scandal ya serikali ya Tanzania kuhusika katika kuwauzia silaha waasi wa Congo, kimsingi alisema anajua kila mwenendo wa kila mfanyakazi wa serikali nzima ya Tanzania na hakuna hata mmoja aliyehusila na biashara hiyo ya silaha.

Unacheza na hiki kimungumtu kinachoitwa Membe wewe?

Ikabidi baada ya siku chache serikali imtume balozi Dr. Mahiga aende kusawazisha kwa kutoa jibu la kueleweka zaidi kwa kusema serikali ya Tanzania haihusiki na biashara hiyo na inachunguza madai kwamba wafanyakazi wake wamehusika kama watu binafsi.

Balozi Mahiga akasema uchunguzi utafanyika, nilivyosikia hivyo nikajua story ishakwisha.

Na kweli sijaisikia tena.
 
Jamani habari za tz. wajameni zangu? mbona tz inaelekea shiomoni? Ina maana raisi Slaa ameshindwa kuendesha nchi? waziri wa mali asili Mh. Mchungaji (mbunge wa Iringa Mjini) vipi mbona hatuoni cheche zako kama ulivyokuwa waziri kivuli? na wewe waziri wa sheria Mh. Lissu hebu wekeni sheria kali dhidi ya mafisadi yote. waziri mkuu Mbowe kuwa mkali.Vipi maji siku hizi dsm yanapatikana? waziri wa maji Mh. Mnyika fanya kazi zako ili CDM ionekane ni tofauti na CCM. Waziri wa fedha ndani ya serikali mpya ni nani? Mwana mpotevu Zitto vipi siku hizi vipi?
 
Hakuna anayeeleweka kwenye hii serikali, kuanzia kwa le profesare hadi viongozi waandamizi
 
Back
Top Bottom